Bodi ya Mikopo (HESLB) kuna tatizo gani na makato yetu ya Mwezi Januari 2023?

mpasta

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
917
1,997
Niende kwenye hoja Moja kwa moja. Nikiwa ni mnufaika wa mkopo wa HELSB,
Nilianza kulipa deni langu mwaka 2009 mpaka kufika 2014 nikawa nimemaliza deni langu lililoletwa kwa muajiri wangu.

Ghafla mwezi Septemba mwaka 2022 nikaona muajiri wangu ameanza kunikata deni upya tena kubwa kuliko deni langu halisi la mwanzoni. Nilipoenda kufuatilia na salary slips zangu za malipo wakaniomba samahani kuwa wamenibambikia deni la mtu mwingine ila Ile mwaka 2014 kuna deni nilibakiza.

Sikutaka majibizano nao nikakubali yaishe. Sasa nikaanza kukatwa na muajiri wangu baadae nikatafuta pesa pembeni nikalipa kwa control number. Sasa nafuatilia barua ya kuonyesha nimemaliza mkopo wangu ili nikampe muajiri wangu asitishe makato hawana majibu yanayoeleweka. Wanasema hazina hawajawapa bodi pesa za makato ya mwezi Januari 2023.

Binafsi siamini kama kweli hazina wanaweza kukata pesa ya mtumishi halafu wasiwasilishe sehemu husika kwa wakati.

Tunaomba bodi mtupe majibu ya kueleweka, mnawatesa watumishi ambao wameshamaliza mikopo yenu ya ngumi ya ndoige ya mandonga inayobadilika badilika kila wakati.

Tukipiga simu zenu za huduma kwa wateja hazipokelewi, zinaita mpaka zinakata
 
Niende kwenye hoja Moja kwa moja. Nikiwa ni mnufaika wa mkopo wa HELSB,
Nilianza kulipa deni langu mwaka 2009 mpaka kufika 2014 nikawa nimemaliza deni langu lililoletwa kwa muajiri wangu.

Ghafla mwezi Septemba mwaka 2022 nikaona muajiri wangu ameanza kunikata deni upya tena kubwa kuliko deni langu halisi la mwanzoni. Nilipoenda kufuatilia na salary slips zangu za malipo wakaniomba samahani kuwa wamenibambikia deni la mtu mwingine ila Ile mwaka 2014 kuna deni nilibakiza.

Sikutaka majibizano nao nikakubali yaishe. Sasa nikaanza kukatwa na muajiri wangu baadae nikatafuta pesa pembeni nikalipa kwa control number. Sasa nafuatilia barua ya kuonyesha nimemaliza mkopo wangu ili nikampe muajiri wangu asitishe makato hawana majibu yanayoeleweka. Wanasema hazina hawajawapa bodi pesa za makato ya mwezi Januari 2023.

Binafsi siamini kama kweli hazina wanaweza kukata pesa ya mtumishi halafu wasiwasilishe sehemu husika kwa wakati.

Tunaomba bodi mtupe majibu ya kueleweka, mnawatesa watumishi ambao wameshamaliza mikopo yenu ya ngumi ya ndoige ya mandonga inayobadilika badilika kila wakati.

Tukipiga simu zenu za huduma kwa wateja hazipokelewi, zinaita mpaka zinakata
Hii Bodi imekosa ubunifu. Inashindwa kuwakata wale wale wanufaika wake ambao hawajaamza kukatwa!

Badala yake imeamua kurejesha makato kwa watu waliomaliza deni, kwa kuwabambikia deni jipya, na lisilo eleweka!

Yaani unamuandika mdeni wako deni! Mfano milioni 7,800,000/=!!! Unamkata kwenye mshahara wake mdogo, mpaka deni linaisha!! Baada ya miaka kadhaa, unarejesha tena makato! Unamuuliza kulikoni? Anasema eti ulikuwa hujamaliza kulipa retention fees, lakini pia umepigwa penati!!

Hivi huu si uhuni!!
 
Back
Top Bottom