Ukitaka kujua mwisho wa ubaya ni aibu ni pale unapodhani ukimweka mwenzio ndani siku zitasimama au maisha hayatoendelea.
Mlisema wakalie krismas segerea wakala na wapo salama.
Mkasherekea wakae ndani hadi mwaka mpya na wamevumilia na Sasa 2019 hii hapa.
Natumai ipo siku mtawaona wakitoka uraiani na watawakuta amjapiga hatua kwa lolote badala yake kila mtakapowaona au mtakapokuwa mkitafakari kuhusu wao mtaumia na kudhoofika kimwili.
Nitake kuwatakia mwaka mpya mwema na ukawe mwaka wa kumshinda mtesi wetu kwa kuutafuta Uhuru uliotekwa na watu wachache wasiokuwa na hofu ya Mungu mioyoni mwako.
Kama Kuna kuzaliwa Basi Kuna kifo na Kama Kuna madaraka pia Kuna kustaafu,Kuna kutawala na mwisho ukatawaliwa.
Sent using
Jamii Forums mobile app