Hence proved. Mbeya ni kijiji kikubwa

Hence proved. Mbeya ni kijiji kikubwa

Airport ya songwe ipo mbeya na sio mbozi Kuna sehemu kunagawa mkoa wa mbeya na songwe, ukifika Kijiji cha senjere huko ndo mkoa wa songwe unapoanzia
 
Kuhusu hali ya hewa nani alikutuma uje mbeya mwezi huu lazima utapachukia tu, ukitaka kuenjoy njoo mwezi wa 12 hadi wa Saba hapo
 
Huu uzi nimechunguza nimegundua kuwa wanaoitetea mbeya wote ni chawa wa CCM, huenda hizi I'd wa wana CCM huwa ni I'd za mtu mmoja na anatokea mbeya

Haiwezekani chawa wote wa Samia wawe wanatokea mbeya Kuna namna hapa

Ufatilien huu uzi muone chawa wa Samia ndo wanaoitetea mbeya nahisi ni mtu mmoja I'd mingi sana
 
Unakaa dar halafu unaishi sijui tandale sijui manzese

Sasa wewe unaishi au au unasukuma siku tu??

Si bora aliyepo mbeya yeye anaishi maisha mazuri kuliko nyie wa kudandia mwendokasi madirishani
 
Songwe Airport iko Mbeya. Mkoa wa Songwe hauna Airport bali wanatumia Airport iliyoko Mbeya.

Asili ya jina Songwe ni mto unaoanzia bonde la Songwe lililoko wilaya ya Chunya, mto unapita mpakani mwa Mbeya na wilaya ya Mbozi kisha unakwenda wilaya ya Ileje na kumwaga maji ziwa Nyassa
Siku hizi bondeni siyo Chunya tena, Mto Songwe unamwaga maji Ziwa Rukwa
 
Siku hizi bondeni siyo Chunya tena, Mto Songwe unamwaga maji Ziwa Rukwa
Mto Songwe unamwaga maji ziwa Nyasa, na ndio hufanya sehemu ya mpaka kati ya Malawi na TZ kwa pande za ileje.

Watu wanachanganya mambo. Mtu anasikia ziwa Rukwa basi ukimwambia ziwa hilo liko pia upande wa Songwe (zamani sehemu ya Chunya) anakubishia. Hawa ni wale wanaoweza fikiri kuwa ziwa Nyasa lote liko wilaya ya Nyasa.

Kuna Songwe mkoa ambao una wilaya za Songwe, Momba, Mbozi na ileje.
Kuna mto Songwe ambao unaanzia milima ya uporoto huko Mbeya.
Kuna gereza la Songwe na Songwe airport hivi vyote vipo Mbeya.

Napenda ukweli tu and I don't care whether Mbeya is a city or a village.
 
Mto Songwe unamwaga maji ziwa Nyasa, na ndio hufanya sehemu ya mpaka kati ya Malawi na TZ kwa pande za ileje.

Watu wanachanganya mambo. Mtu anasikia ziwa Rukwa basi ukimwambia ziwa hilo liko pia upande wa Songwe (zamani sehemu ya Chunya) anakubishia. Hawa ni wale wanaoweza fikiri kuwa ziwa Nyasa lote liko wilaya ya Nyasa.

Kuna Songwe mkoa ambao una wilaya za Songwe, Momba, Mbozi na ileje.
Kuna mto Songwe ambao unaanzia milima ya uporoto huko Mbeya.
Kuna gereza la Songwe na Songwe airport hivi vyote vipo Mbeya.

Napenda ukweli tu and I don't care whether Mbeya is a city or a village.
Mito Songwe iko miwili. Wa ziwa Rukwa na Ziwa Nyasa.
 
Mito Songwe iko miwili. Wa ziwa Rukwa na Ziwa Nyasa.
Screenshot_20251021_125315_Chrome.jpg
 
Unakaa dar halafu unaishi sijui tandale sijui manzese

Sasa wewe unaishi au au unasukuma siku tu??

Si bora aliyepo mbeya yeye anaishi maisha mazuri kuliko nyie wa kudandia mwendokasi madirishani
Ila uswazi wa Dar ni bora kuliko Mbeya. Uswazi wa Mbeya nyumba zao, yale matofali ni kama tu matope wakayachonga wakayagandisha, uswazi mzima wa kijivu 😂😂
Kuna nyumba Mbeya hadi ukuta unajaa nyasi maana wamejengea udongo ambao bado una rutuba
 
Nimekaa Mbeya miezi miwili sasa, ila nimenyoosha mikono. Mbeya ni likijiji likubwa, picha linaanza kila mtu kajaa vumbi kuanzia usoni hadi miguuni. Huwezi kutembea Mbeya kwa raha, bajaji zina fujo, highway hakuna sheria zinafuatwa, vumbi kama lote. Utapata mtu kapendeza town, ila chini ana soksi, jinsi vumbi linakera!

Ukija kwenye biashara, hawa watu hawana habari na customer service, utachoka wewe mteja....wahehe wanasema 'sindimgaya sida'...vifungashio vyao utalia. Yaani wanafanyia biashara kimaskini, imagine mfuko ulioisha diapers, mama muuza matunda anakupa ndo uwekee matunda. Usiponunua mfuko wako, utalishwa uchafu ufurahi.

Mbeya panasifika Kwa vyakula vingi, ila nimechoka mwili na roho kwasababu menu zao ni ugali na wali kila siku, hapo utawekewa na chainizi, maharage na nyama(nilitafuta mtori, nikaambiwa huku ukipika mtori hakuna wa kununua, ndizi za kupikwa pia siyo kitu utakikuta sana sehemu za vyakula). Au uende sehemu za kitimoto, manake huku mdudu amejaa kila Kona au ule chips na zile nyama choma zao. Kupata matunda yaliyokatwa ni shidaaaaa, nasema ni shida. Ukitaka kula varieties lazima jasho likutoke. Nikaja kuelewa kwanini wakazi wengi wa hili likijiji wanamaumbo ambayo huwezi jua kiuno Kiko wapi, matumbo yao yamejaa wanga hatari, swala la balance diet kwao ni ndoto. Ukionwa unakula matunda laZima uulizwe kama wafanya diet au. Wako na ushamba fulani hivi wakazi wa huku, kwanini Mbeya ni Jiji? Aibu naona mimi.

Mbeya katikati ya mji Ile mitaa ya Mwanjelwa Kuna watu wanapika chips kwa kutumia kuni, basi Moshi unasambaa maduka ya jirani hadi siyo poa, na Watanzania tunajua kuvumiliana, basi majirani wanavumilia. Sehemu imejaa Moshi, unakaaje hata ule chakula? Na kwamba hakuna kiongozi anayeona hiyo shida? Katikati ya mji kabisa?

Hapo sijagusia miundombinu, mipango ya mitaa, majengo yao, ni fujo TU. Halafu vijana wengi wa rika fulani hawaogi, wote wananuka harufu hiyo hiyo....wanaogopa maji hatari. Wakija kupata huduma ofisini unatamani umwambie Kaa kwanza pembeni nitakuhudumia ukiwa umekaa ili Ile harufu yake isijae kwenye dirisha lako.

Kuna mtaa street lights zinawaka kwa sensor, Kuna muda sensor zinafanya kazi, Kuna muda hazifanyi. Usiku wa Giza kabisa taa inawaka sekunde mbili inajizima. Kweli aliyefunga hizi taa ni mzima kabisa?

Baada ya kusema haya, na kwa mpangilio mbovu, niseme TU, Watanzania tunasafari ndefu ya kuishi kwa ustaarabu kwenye miji yetu. Uchafu kila sehemu, noise pollution ndo usiseme, hard waste zimetapakaa kila sehemu. Hatuoni shida?
Am out.
Mkuu Mbeya ndio iko hivyo. Hata mimi mara ya kwanza kuja nilishangaa sana. Ila ukikaa kwa muda unapazoea. Nahisi ndio binadamu tumeumbwa hivyo
Licha ya kuwa watu hawali sana matunda ila at least matunda yapo na ni bei rahisi
Ila ni kweli Mbeya ni mji wa hovyo mno ila kuna mpango wa serikali kujenga mji wa kisasa maeneo ya Nsalaga huenda ukabadilisha muonekano wa jiji letu
Kuna maeneo wamejenga wabongo na yapo vizuri tu, sio kote tumeharibu mfano njoo Iwambi huku fika Maziwa na JB. Watu wanajenga nyumba nzuri
Hata Uyole na Isyesye kuna maeneo watu wamejenga vizuri. Forest pia
Cha msingi ukitaka kujenga usinunue kiwanja sehemu za uswahilini. Tafuta mitaa ya kati au premium. Uzuri wa Mbeya hiyo mitaa ipo. Tafuta kiwanja shusha mjengo wako taratibu. Miaka kadhaa jengo limekamilika unakaa zako kwa amani. Unaachana na pilikapilika za Ilomba, Kalobe, Soweto, Mabatini nk
 
Ukiacha ujenzi wa kutumia tofali za tope jiji la Mbeya, ujenzi wa majiji mengine yote unafanana kabisa hasa makazi ya watu na ofisi za uma, kama ujenzi holela karibu majiji yote Tanzania yamejengwa hivyo. Kuna utofauti mdogo sana wa kimiundombinu kati ya Dar na majiji mengine yaliyobaki hapa nchini hasa kwenye makazi ya watu. Ukitoa majengo ya uma na maeneo ya biashara na viwanda ujenzi mwingine wote uliobaki unafanana maana watanzania wa Dar, Mwanza na Arusha ni walewale.
 
Mwanza, Dodoma, Mbeya, Arusha hivyo vyote ni vijiji vilivyo changamka tu.
Jiji Dar pekee tena la hovyo tu.
Mkuu huwenda ikawa huijui Mwanza na hujawahi fika hivyo unahadithiwa tu. Embu muwe mnatenga bajeti ya kutembea nchi hii hata mara moja kwa mwaka. Tatizo lenu mnaulimbukeni wa kutaka kila jiji lifanane na Dar, kumbuka kila jiji lina upekee wake. For me Mwanza is the best city than all city kulingana na vigezo kama hali ya hewa, geographical location, gharama za maisha, transport, muonekano wake na accessibility kati ya eneo na eneo within a city is very simple. Unaweza kuta mtu anaishi Mbagala Dar au vingunguti kisha anata kujifananisha na mtu anayeisha Katoro Geita.
 
Mkuu huwenda ikawa huijui Mwanza na hujawahi fika hivyo unahadithiwa tu. Embu muwe mnatenga bajeti ya kutembea nchi hii hata mara moja kwa mwaka. Tatizo lenu mnaulimbukeni wa kutaka kila jiji lifanane na Dar, kumbuka kila jiji lina upekee wake. For me Mwanza is the best city than all city kulingana na vigezo kama hali ya hewa, geographical location, gharama za maisha, transport, muonekano wake na accessibility kati ya eneo na eneo within a city is very simple. Unaweza kuta mtu anaishi Mbagala Dar au vingunguti kisha anata kujifananisha na mtu anayeisha Katoro Geita.
Mwanza napajua nimekuwa hapo Mara kadhaa.
Nina ndugu hapo tena wa karibu siyo wa kuunga.
Nimeshapeleka mizigo ya biashara.
Mwanza ni kijiji tu na nyumba za milimani zilizokosa vyoo aibu tupu.
Nina kiwanja pia karibu na SAUTI.
 
Back
Top Bottom