Hekalu la Spika wa Tz

Hekalu la Spika wa Tz

Halafu tutasikia huyu spika akimaliza muda wake kagoma kutoka kama mzee 6 pale Dar. Mmmmmhh tusubiri tuone
 
Mwisho mtasema rais akakakae nyumba ya kupanga Magomeni :wink2:

Kwani si hata spika wenu to be Tundu Lissu si angependa akae kwenye huo mjengo? au mtauuza? :A S 13:
 
kwanini tujenge nyumba za 1.5b kwa kiongozi mmoja wakati hali yetu ya kiuchumi hairidhishi? kwanini asijengewe nyumba ya angalau 200m hiyo 1.3b tuiweke kwenye vitabu na madawati? tatizo serikali yetu inaishi kitajiri kwa kodi zetu wakati sisi tunazidi kuwa masiki la msingi tujipange kusimamia matumizi ya kodi zetu
 
Hatakaa miezi 6 lazima laana na machoz yetu watz avunjike miguu
 
Hivi si niliskia kuna Hekalu lingine la Spika linajengwa kula Urambo? Hivi nalenyewe limekamilika? Je atakuwa anatumia lipi? La Urambo au hili la Dodoma?
 
JF sasa mmezidi, sasa mnataka Spika aishi nyumba ya namna gani? Mbona hiyo nyumba ya kawaida sana. Ebu leteni thread zenye mashiko wakuu, sio kulalamika tu kila kukicha

Mkuu kaangalie nyumba wanazolala Madaktari na Walimu ndio utajua mantiki ya kuponda hilo Hekala la Spika! Iweje mtu mmoja (Makinda) awe Priority kulika maelfu na maelfu ya Madaktari na Walimu nchini? Na hapo bado sijazungumzia nyumba wanazolala Madereva, Masecretary, Makondakta, Waendesha Pikipiki, Wauza samaki kule ferry, nk.
 
..Hapa tusimlaumu Spika, tulaumu Mfumo uliopo. Mfumo uliopo kisheria ni kwamba ni lazima Kiongozi wa Serikali ajengewe nyumba ya kuishi tena yenye Hadhi yake, ni moja ya Stahili zake whether anataka au hataki ipo kisheria. Hio nyumba hapo (Hekalu!!) imejengwa kwa sababu ni moja ya Stahili zake Spika kujengewa nyumba ya kuishi na Serikali.
..Mwl Nyerere alikataa asijengewe, lakini mwisho wa siku ilijengwa.
 
Architects wamefanya kazi nzuri! Its a beautiful house..
 
Mwisho mtasema Rais akakakae nyumba ya kupanga Magomeni.

Mkuu Maundumula,
Ishu si Rais kwenda kukaa Nyumba ya kupanga Magomeni. Ishu hapa ni kwamba iweje wale wanachi wa Tandahimba, Nkasi, Kiteto, Serengeti, Kibondo, Liwale, nk waishi kwenye nyumba za udongo zilizoezekwa kwa Manyasi yanayovujisha wakati waajiriwa wao wanajenga mahekalu kwa pesa zao??





 
Ni nyumba ya kawaida tu hiyo acheni mambo yenu. Mnapimaje thamani ya Asset kama hiyo ambayo inakaa miaka 40?

Haya tuseme Spika angekaa nyumba ya kupanga yenye hadhi yake kwa mwezi 3,000,000 * 12 = 36,000,000 mwaka ndio mlivyotaka nyie tulipe?
Hadhi! hadhi gani? Spika ni mtu wa kawaida tu! Nyumba ya kifahari haimfanyi awe na akili zaidi! Cheo au hadhi uiitavyo wewe iko kwenye kichwa na sio mali. Kuna watu wanakaa mbavu za mbwa na wana akili zenye hadhi kuliko ufikiriavyo!
Haya ni matumizi mabaya ya fedha za Watanzania! Kwani Adam Sapi alikuwa anakaa wapi? Kwani Samweli Sitta alikuwa akikaa wapi. Kwa nini tusielekeze nguvu zetu kwenye issue nyingine zenye tija! Kuna watoto wanakaa chini kwa kukosa madawati. Brother when you are starting to count 1.5b its not a joke! Tungeweza kutatua matatizo mengi sana ya Watanzania! Hebu waulize wale wamama ombaomba wale wa MEWATA budget yao kwa uchunguzi na matibabu ya wakina mama pale Kilimanjaro sasa hivi! Wangeweza kuacha kuomba omba kama tungeelekeza fedha hizi kujenga nyumba moja tu ya spika. Spika! What the hell!
 
Kwa jinsi serikali inavyolalamika kuwa haina hela za kufanya mambo mbalimbali ya maendeleo pamoja kulipa vimishahara vya "mauti kwa baadhi ya watumishi wake" .......nooh hiyo nyumba ni kufuru na matusi makubwa kwa serikali yetu.
Kama serikali inasema haina hela....basi tuone hata ikiwajengea vigogo wake nyumba zinazoendana na "hali yetu mbaya kipesa"
Watu waache kujifanya eti...nyumba ya kawaida tu hiyo....tatizo tumeishazoea ufisadi!..watu wengi hapa mjini waliojenga majumba kama hayo ni watumishi wa umma na mihela waliotumia kujengea wameipata kifdisadi tu!
 
Kazi kweli,ukizingatia Madakatari walishaongezewa 15,000/= ya posho.kama vipi bunge waliuze ili wapate pesa ya kujiongezea posho.
 
Bi kiriboto Akigoma kuhama? Kama mh. Sitta itakuweje? Watajenga ingine
 
Ni nyumba ya kawaida tu hiyo acheni mambo yenu. Mnapimaje thamani ya Asset kama hiyo ambayo inakaa miaka 40?

Haya tuseme Spika angekaa nyumba ya kupanga yenye hadhi yake kwa mwezi 3,000,000 * 12 = 36,000,000 mwaka ndio mlivyotaka nyie tulipe?

Mkuu umeshawahi kutembelea shule zetu za Msingi? Vituo vya Afya Vijijini? Huko vijijini hali mbaya, Nyie mnaoponda raha mijini nendeni na vijijini ndio utaelewa maana ya gharama la hilo hekalu.
 
kwani kisha pata mkopo maana kuna siku za hivi karibu alikuwa anaomba ridhaa ya raia wake ili akope..
 
Back
Top Bottom