Kama aliyajua hayo aligombea ya nini? Huko nyuma uliletwa uzi kama huu, nakumbuka nililalamika sana kuhusu hawa vijana mnaowapa madaraka wakati wanashinda maofisini kwenye malaptop sijui matwiter, mafacebook na sijui miwhatsapp. Hiki chama hapa kilipofikia ni kutokana na amshaamsha iliyoendeshwa nchi nzima mara baada ya uchaguiz wa mwaka 2010 na kumi. Kulikuwa na operesheni nyingi sana nchi nzima, kwa kiasi kikubwa operation hizi zimezaa matunda kwa watu kukipenda chama na kwenye uchaguzi huu wa serekali za mitaa majibu tumeyaona.
Leo hii mnampa kijana madaraka anaishia kukaa ofisini, hatuoni hamasa. Kwahiyo hamasa mnangoja iletwe na wazee kama akina Slaa!? Tunaomba cdm watambue kwamba sisi wengi sio wanachama wao bali ni washabiki, kwahiyo kama hamna amshaamsha hatutakuwa na muda kuwafagilia kwani tunaona tutawapa madaraka mtuletee mambo yaleyale ya kiccm, mtu akipewa madaraka hataki hata kuja kuonana na wanachi anashinda ofisini sijui anafanya maresearch kwa google huko ofisini. Hatuna muda wa kuremba sisi na hao macheckbob mnaowapa madaraka. Tunataka majembe ya kazi, au unadhani tutawapa nchi wakati mnawapa madaraka watoto wa mama? Tunataka kijana akipewa madaraka anaingia front anasambaza elimu ya uraia na kuongeza wapiga kura zaidi sio anabweteka ofisini kujifanya msomi wakati hatuoni input yake.
Watu wamebaki wanamponda Lema hapa sijui hana elimu sijui nini. Lakini nenda Arusha, akiitisha mkutano nyomi ya wapiga kura. Wakati wa uchaguzi wa marudio ya udiwani hakwenda bungeni bali alisimama bega kwa bega kutetea viti vyote vikapatikana. Wakati wa uchaguzi wa serekali za mitaa alikuwa anapita mitaani kuhasisha watu na mikutano mingi alikuwepo. Majibu yake tumeyaona cdm toka asilimia sijua tano 2009 ya viti leo wako almost 50/50 na ccm. Hayo yote kafanikiwa kwa kwenda kwa watu na kuwahamasisha, au mnadhani yeye hajui hayo mafebook? ama hana ofisi? Nyie mwacheni tu huyo kijana apake perfume na kuvaa macheni hapo ofisini muone kama mtamuona mpiga kura yoyote. Mnafanya utani nyie, ndio hao wasomi kila siku tunaambiwa wajiunge cdm?