Hebu jamani, mstaarabike muda mwingine...

Hebu jamani, mstaarabike muda mwingine...

Samcezar

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
13,093
Reaction score
22,806
Naandika taarifa hii nikiwa tayari nimeshakasilishwa......
Ipo hivi......Mimi ni kijana wa kiume na fiancee wangu tunaishi maeneo ya tabata kinyerezi kwenye chumba cha kupanga(self contained). Hii wiki iliyoisha fiancee wangu alikuwa amerejea kutoka Arusha kwenye safari ya msiba wa mfanyakazi mwenzao iliyomchukua siku tatu. Nilikwenda kumpokea airport tukarejea home mida kama ya saa mbili na nusu kutoka airport...... dakika si nyingi walikuja wasichana wawili ambao walikuwa wanazunguka kukusanya maoni kuhusu huduma za kibenki chini ya kampuni yao jina limenitoka..........
Sasa hapo maskani kuna mijengo miwili tu......nyumba ya vyumba vinne kubwa na hili geto langu huku nyuma ndani ya fensi...........
Hawa wadada walipomaliza kuhoji wapangaji nyumba kubwa wakaja na mlangoni kwangu.......sasa waifu ile kuwafungulia akashangaa kuwa mojawapo ya wale wadada ni shosti yake walisoma wote primary utotoni.
Bas wale mademu wakaingia ghetto ndani........wakaketi kwenye mito kwenye jamvi maana sina makochi maana ndo kwanza naanza life na wife.....
Sasa wakati hawa manzi wametimba wife alikuwa ana andaa breakfast heavy........maana nilikuwa hata sijapiga tea.......
Basi waif akajiongeza akatoa kitu cha kutosha watu wanne......tukawa tunapiga breakfast.......sasa demu m'mojawapo alikuwa full kuwasiliana na wenzake wengine ambao walikuwa nao wanasugua gaga kwenye kazi yao hiyo hiyo akiwaambia amekutana na waifu ambaye ni shost wao so waje kumpa hi.Muda si muda wakati waif ndio anatoa vyombo na kuvipeleka nje kuosha.....wakatimba mademu wengine watatu so ikawa tupsi ya wasugua gaga watano.
Ghafla hali ya hewa ikabadilika kutoka utulivu 100% hadi utulivu 0% maana ilikuwa ni kelele mtindo m'moja hapo ndani kwa vicheko...mabishano......umbea full majanga........!
Mimi nilikuwa natazama series ya for better for worse ya tyler perry na wife......ambayo tulikuwa tunaicheki kwa utulivu na ukimya wa hali ya juu ukijumlisha na mazingira ya pale maskni eneo zima huwa ni kimya hata ikidondoshwa sindano utasikia mlio.
Sasa hawa manunga yembe wakaanza kunikinai uwepo wao maana hizo story na mabishano zilikuwa ni baina yao hadi wakamsahau waifu na mimi.......
Dakika zikawa masaa tokea saa saa nne hadi saa nane mchana hata dalili ya wao kusepa sikuona ndio kwanza wakawa wanabadili mikao na kujadili mikasa ya mabuzi na mabwana zao huko kazini kwao.......
Waif akanitext akaniambia mbona kama haupo sawa.......ngoja nitafute pozi la kuwasepesha.........nikamwambia waifu angoje kidogo watajishtukia watasepa.......
Kumbuka huo ni muda wa lunch......so waifu akamwita dogo wa boda boda akamnunulie maini.........
Waifu akazama tena jikoni akatoa kitu cha chapati na roast ya maini........tukapiga menyu tena na hawa manunga yembe ........basi tukashiba pale ila "UKAWA" mode ikawa bado ON......yaani utadhani walitumwa kutukomoa kwa kutunyima uhuru wa mimi na waifu kufanya yetu pale room .....
Basi mishale ikatembea hadi saa kumi na moja kasoro jioni. Hapo sijaoga maana ntakosa pozi la kubadili nguo........waifu anahamu na mimi anataka nimpe mambo........ila majanga ni UKAWA ya hawa manungayembe.........
Waifu ikabidi anitext akasema husband bwana me nawazingua wasepe..... basi waif akajifanya ananiomba pesa ya salooni akafumue na kuosha nywele......muda huo huo nikajifanya na mimi nimetumiwa ujumbe na mshikaji ananingojea pub tukajidili biashara......
So nikasimama nikachukua tshirt kabatini maana nilikuwa na tracksuit pants chini na vest kwa juu........sasa yule shost wake aliyekuwa wa kwanza kuja akasuggest waende na waifu saloon.....hawa wengine wawangoje wakicheki t.v then watawakuta wakirejea kutoka saloon.....
Me nkaona hapa kuna dalili kuwa hawa manunga yembe wanataka kukaba hadi penati maana siku nzima tupo nao.......mbona majanga.
Waifu akastukia mchezo akawa mnjanja.......akamwambia kuwa yeye akitoka salooni atakwenda kwa ndugu yake tabata bima na huenda akachelewa au kulala huko huko.............yule nungayembe bila hiyana akauliza na wewe shem utachelewa sana......nikamfix kuwa huyu mshikaji wangu naweza rudi hata saa nane za usiku story nyingi. Ndio ikawa ponea yetu wakafunga virago wakasepa na sisi tukitoka............tukawasogeza hadi segerea stand ili wachukue daladala tukageuza tukarudi geto tukaendelea na mahaba yetu.

Sasa swali langu.......Hivi kuna ugumu gani wa mtu kujiongeza kistaarabu unapoenda kwenye geto la mwenzako.......unashindwa hata kusoma ishara kuwa hapa nawabania wenyeji wangu uhuru wa kufanya yao.........mxeummmmmmm.........yaani mijitu ustaarabu ni zero kabisa these days kazi kuendekeza tamaa na njaa za kiboya aaaaaaaaaaghhh.
 
Best ukawa maana yake ni kukomalia jambo.........
 
Stori ipo kimbea kishenzi alieitunga ni mwanamke mimi nimegundua ivo
 
Kwan uwezi kuandika kua umepanga room Adi uandike self contained????

My dear sweetheart ........unapomuhadithia mtu jambo inabidi kumpa picha ya mandhari........hapo kusema self contained nilikuwa nataka ujue kuwa mazingira ninayoishi yapoje........na wala sio tambo.........ili ujue jinc gani mimi ni mtu wa privacy.......
 
Sijaelewa, inamaana ofisi yao ilishia gheto kwako??? Watakuwa waalimu hao, hakuna wafanyakazi Tz wenye muda wa kurelax kama walimu,

Alafu unasema manunga yembe umejuaje??? Inawezekana hata mkeo akienda kwa watu wanamwita nungayembe.

(a) Hata mimi nilishangaa maana walikuwa bado wanaruti nyingi za kufanya kulingana na mazingumzo yao........ila nadhani walishachoka na majukumu yao......maana wakajitoa ufahamu kabisa.

(b) Ni manungayembe kwasababu mwanamke mwenye kwake huwa hata siku moja hawezi poteza muda kukaa kwa watu bila ratiba maalumu.......kama fiancee wangu hata mara moja huwezi mkuta anarandaranda bila ratiba.......ni huwa utamkuta kalala geto kama hana cha kumkeep busy.
 
sasa mkuu yani umeandika maelezo meeengi hata yasiyo na ulazima....
halafu kuwaita wenzako majina kama hayo mmm haijakaa poa sana...
 
Lugha lugha lugha!Unajua mimi ni mzee umechanganya "style" za lugha hadi nime blow!Fiancee ...halafu wife.Ni kama ninyi mlikuwa watatu mkatembelewa na maembe dodo sijui manungayembe?Jitahidi kuandika lugha ya kawaida tusitumie miwani mkuu.😀😀


Pole mzee.........fiancee ni mchumba.......lakini pia ni mke wangu..........
 
Sijaelewa, inamaana ofisi yao ilishia gheto kwako??? Watakuwa waalimu hao, hakuna wafanyakazi Tz wenye muda wa kurelax kama walimu,

Alafu unasema manunga yembe umejuaje??? Inawezekana hata mkeo akienda kwa watu wanamwita nungayembe.

Maana ndege wafananao huruka pamoja na ukute hata huyo wife wake before nae alikuwa ana tabia ya kuuweka akienda kwenye nyumba za watu
 
sasa mkuu yani umeandika maelezo meeengi hata yasiyo na ulazima....
halafu kuwaita wenzako majina kama hayo mmm haijakaa poa sana...


Kiswahili hicho boss plus nipo sahihi kupita maelezo kuwaita hayo majina
 
Back
Top Bottom