He has done so much for me, I can't tell it all. Narekelema

He has done so much for me, I can't tell it all. Narekelema

Nasiche

JF-Expert Member
Joined
Jun 18, 2019
Posts
291
Reaction score
735
"You've done so much for me, I can't tell it all, narekelema. What shall i render to Jehovah for he has done so very much for me."

Basi buana kuna wakati Mungu anaweza kukutendea kitu katika mazingira ambayo hata hukutarajia. Mazingira ambayo hata hudhani kama Mungu anakaa huko

Nilijua JF ni mtandao tu wa kawaida ambao uwezi kukutana na mtu wa aina flani hivi (kwa akili zangu )
Kumbe Huku nako kuna Mungu na kuna watu wazuri sana .

Nilipoandika bandiko langu la kutafuta mume niliandika kwa sababu nilikuwa na maumivu ,i was not serious siyo kwamba nilikuwa sina uhitaji (nilikuwa ninao sana ) ila nilijua huku siwezi kupata aina ya mtu naemfikiria lakini nikasema liwalo na liwe acha nipost

Nilipoonana naye, ndipo nilijua kuwa hakuwa tu mtu wa kawaida ila alikuwa mwanaume ambaye ameandaliwa kwa ajili yangu (mume wangu )

Aisee tunaelewana na huyu baba hadi natamani kulia kuna saa tunazinguana lakini nashukuru kila mmoja yupo willing kuisaka amani na muda huo huo tunakuwa sawa
Toka nizaliwe sijawahi kuona mwanaume mwenye mapenzi kama wewe, upo very romantic, Kila unachofanya kwangu naona kinamanisha mapenzi , nakupenda mpaka nakupenda tena

asante

Asante asante asante

--------------

Ni Mimi na mpenzi wangu niliempata kupitia jukwaa hili Sasa jamani tushafikisha miezi sita na bado hatujaachana wale mliosema tutaachana mwezi hauishi sijui mna neno gani la kutuambia

Tushapelekana kwa wazazi. Tunategemea kuanza maisha muda wowote kuanzia Sasa je tutakuwa tumewahi

Nishawajua nduguze wengi wazazi na ndugu wa Karibu pia Mimi anawajua baadhi ya ndugu zangu

Kipi bora
Ndoa ya kanisani
Ndoa ya serikali
Sogea tuishi?

Faida na hasara KWA Aina ya ndoa utakayoitaja

Tupo tayari kwa ndoa yeyote kwasasa Mana tunahitajiana, sherehe na manjonjo mengi hatutaki sana kikubwa tunahitajiana sisi tu.

Refer ✓
He has done so much for me, I can't tell it all. Narekelema
 
Back
Top Bottom