Hayati Dkt. Magufuli alikuwa akiwaza nini?

Mbona unataja mabaya tu hakuna mazuri aliyoyafanya km miradi ya serikali kuitekeleza kikamilifu
Kwenye kampeni hatukumdai Ndege,reli na uwanja wa ndege chato,tulimdai maji,dawa hosp, ajira na watumishi walitegemea awatunze vizuri badala yake akawasimanga bila aibu
 
Yeye aliyekufa mnamuona mshamba??
Nyie ambao hamjafa ni wajanja??
Kila mtu na Siku yake,hata ww unayeshangilia kifo Cha JPM,utakufa tu Siku moja.
Kufa ni kwa kila mmoja,sasa kama unajua utakufa kwanini uwatese wenzako kisa madaraka!!!?
 
Kwa jinsi alivyokuwa amejijengea kuogopwa, kusifiwa, kuabudiwa, kusujudiwa ni wazi alikuwa anawaza kuwa Rais kwa vipindi zaidi ya viwili vile vilivyowekwa kikatiba.

Siku moja nikiwa na jamaa yangu mmoja tulikuwa tunamuangalia Magufuli kwenye runinga akiwa nafikiri Dodoma, alikuwa kwenye ibada kanisani kwa jinsi alivyokuwa anasujudiwa na viongozi mle kanisani, unganisha na Matukio ya akina agrey Mwanri na viongozi wengine wa dini walivyokuwa wanamtukuza kiumbe yule.

Siku ile nkamwambia jamaa yangu maneno yafuatayo" Huyu mtu atakufa mungu hawezi kukubali kiumbe chake alichokiumba kipewe sifa anazostahili kupewa yeye muumba" yule jamaa yangu nae uzuri alikuwa mtu wa hofu japo ni mtu nyeti serikalini akasema hata mimi hii tabia inanipa mashaka sana (binadamu kutukuzwa )

Tulimalizia soda zetu tukaagana, siku ambayo msiba unatangazwa rasmi jamaa yangu alinipigia cm akanambia unakumbuka yale maneno yetu? Nkasema ndiyak akasema yametimia, nkamuuliza yapi? Akasema Magu, alipenda kumuita Magu. Amefariki nilishtuka kdg lkn nkasema wacha aende tu!

Nawatakieni kheri ya mwaka mpya!
JPM alikuwa na sifa za Mungu na Kidume kwelikweli
1) Mungu hupenda kusifiwa na kuabudiwa ndo maana kwenye amri yake ya kwanza anajipambanua yeye

2)Mungu anapenda haki na si mnafiki ukitenda baya hata kama ulikuwa inashinda naye kila siku anakutimua mfano alimfurumusha shetani ambaye alikuwa malaika wake mkuu akamshusha Duniani

3)Mungu anafanya kazi bila kuchoka aliumba Dunia kwa siku saba na akapumzika kwa siku moja tu

4)Mungu humwangamiza mtu anayeenda kinyume na maagizo yake mfano alimwangamiza Musa na hakufika nchi ya ahadi

5) Mungu anawapenda viumbe wake wema na wabaya ndo maana anatuma mvua,jua na mwanga na vibaji mbalimbali bila kujali dhambi zetu

6)Mungu akitamka jambo au akiahidi jambo arudi nyuma lazima litimie sio kigeugeu

JPM naye alifuaya nyayo zilezile za Mungu
1)Alipenda kusifiwa na kutambuliwa kwa mchango wake katika Taifa

2)JPM Alipenda haki katika uongozi wake alitembea nchi nzima kusilikiliza masikini na kutatua shida zao wazembe wote wasioshughulikia kero za wananchi aliwatimua kwenye nafasi za

3)JPM alifanya kazi usiku na mchana bila kulala alikuwa anawapigia wasaidizi wake simu hata usiku wa manane na kukupa task ya kufanya

4)JPM aliwaangamiza wote walioenda kinyume na matakwa yake hasa wale wapinga maendeleo yale positive kama wale waliokuwa wanapinga kulinda rasimali za nchi

5)JPM alisimamia maendeleo yanafanyika nchi nzima ndo maana alijenga shule,hospitali,halmashauri,barabara mpaka ileje sehemu ambayo ilisahaulika miaka nenda rudi na kuna boda ya Tz na Malawi

6) JPM alikuwa akiahidi jambo lazima lifanyike na anafuatilia kwa umakini na wale waliokuwa wanakosea anawaambia waziwazi na kuwatumbua hata kama rafiki wa damu mf kitwanga akimtumbua angekuwa na roho yakibinadamu asingeweza He was very best friend

N.B kwa mantiki hii lazima jamii wamwone alikuwa Mungu mtu maana alikuwa na sifa za Kimungu sisi wanadamu wote tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu wachache kama JPM wanasifa za Kimungu ila wengi wetu tumekengeuka na kuwa mashetani wanafiki,vigeugeu na majungu
 
Duh kweli watesi wa magufuli wamemsemasema Sana hii week.mzimu wa magufuli utawapa matatizo katika nyoyo zenu..mtashindwa kwenda kwenye stage ya amani bakini na chukichuki na mfu hivohivo tuone mwisho wake.
Wanasema Magufuli alikuwa larger than life, kwani hata akiwa hana life tena, bado kuna watu lukuki wanamzungumza tu. Alisema mtanikumbuka, ni kweli watu wanamkumbuka sana. Yaani kwenye forum hii tu wiki hii kumeanzishwa threads kama sita za kumhusu Magufuli tu, na hii ni trend ya muda wote tangu alipokuwa hai hadi baada ya kufariki.
 
Kwa hiyo wewe na jamaa yako wakati mnakunywa soda ndio mkatabiri kifo chake, ha ha ha
 
Hamuwezi kupumua pasipo kutaja jina la mwendazake kweli kile kilikuwa chuma tena chuma cha pua. R.I.P my life time presdent.
 
Acheni ujinga, hakuna anemtukuza wale aliekuwa akimtukuza zaid ya heshim na uoga kwa mkuu wa nchi

Ni kweli jamaa alikuwa akiogopeka hiyo sabbu ya ukali wake kwa wazembe na wapuuzi, so hata reactions za viongoz pindi akiwepo huyo bwana lazma ziwe za kusifu na kuogopa ili kumfurahisha bosi na kumpa heshima yake, tofaut na hapo wapinzani muache chuki na Uongo wakipuuzi kama mnahis jamaa alkuwa akiabudiwa bas mtakuwa hamumjui putin, xi jin pin, na kim wa north korea, hawa ndio hufanyiwa hizo munazotaka kutuaminisha kuwa ni sifa na kuabudu maana huko ni full udicteta,.

Nje na hapo, mzee magu alijuwa kuwanyoosha wapumbav mpka leo hamkomi kumuongelea, hiyo ni proof kuwa spana zake ziliwakolea
Amewahi kuitwa yesu na kangi lugola
 
Lengo zuri lililotaka kutimizwa kwa kuua,kutesa,kuteka,kupoteza na hadi kuua wengine ili utengeneze "regase"?#@?!#@*£¢¢¢[]¥√
Ni aibu mtu mzima mwenye akili zake kutojua kuwa kuuwa ni sehemu ya kujenga nchi.
Hata haujui kwamba kila Taifa Lina idara ya polisi, na usalama wa Taifa na bajeti ya vifaa kazi
Rais hazomewi, hanangwi Kama mtu fulani kule kijiweni

Mfano mdogo tu
Baba mzazi akisemwa vibaya unapatwa na hasira!!
Ukimdhalilisha Raisi Kuna makamanda wake ambao wapo tayari kumpambania wanaweza kukutoa roho yako mchana kweupe
 
Ni aibu mtu mzima mwenye akili zake kutojua kuwa kuuwa ni sehemu ya kujenga nchi.
Hata haujui kwamba kila Taifa Lina idara ya polisi, na usalama wa Taifa na bajeti ya vifaa kazi
Rais hazomewi, hanangwi Kama mtu fulani kule kijiweni

Mfano mdogo tu
Baba mzazi akisemwa vibaya unapatwa na hasira!!
Ukimdhalilisha Raisi Kuna makamanda wake ambao wapo tayari kumpambania wanaweza kukutoa roho yako mchana kweupe
Umeandika weye mwenyewe?Itoshe kusema weye ni bumunda.Unaishi nchi gani weye?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom