tulizoea kuwaita karunguyeye lakini sidhani kama ndo jina sahihi!!
mkuu hivi wanaliwa hawa!!Hilo ndo jina lake sahihi. Tatizo waswahili mnataka vitu vingine tofauti na vile mnavyovitumia. Lugha ni sauti za nasibu, kile jamii iitacho ndicho sahihi. Jina la huyo mnyama ni karunguyeye, kama ana jina lingine basi nalo silikatai ila hili ndilo jina lake
Nungunungu, hegdehog ( kama kidhungu changu ni sahihi kispelling)
Mkuu porcupine wapo huku africa wengi tu. Hawa kwa kiswahili wanaitwa Nungunungu.
Mkuu hao pichani sio Nungunungu, japo ni kweli wanapatikana Africa, ukiwa Moshi na Arusha utawaona wengi tu mashambani na hata karibu na nyumba.
Nungunungu ni mnyama mkubwa kuliko paka na hao pichani hawakui kumfikia domestic cat. Huko kaskazini wanawaita Kalunguyeye na ni wapole sana. Nungunungu
![]()
huyu ndie nungunungu, na unaweza kuona miba yake ilivyo mikubwa na picha ya chini ndio kitu kinaweza kukupata endapo ukimkimbiza nungunungu kienyeji
![]()
Huyo mbwa umbea umemuisha.
Kalunguyeye ni kamnyama jamii ya panya na miba yake haitoki. Ukimgusa kalunguyeye anajikunja kama tairi kwa kujikausha lkn ukimgusa nungunungu yatakupata yaliyompata huyo mbwa.
Miba ya nungunungu hii hapa, wabunifu hutengenezea vito. Miaka fulani nikiwa sekondari nilikuwa na kalamu ya mwiba wa nungunungu
![]()
ha ha ha ha!mkuu nitaning'iniza na mimi mlangoni!!hawa kalungu yeye kwa imani za kwetu ni kwamba wakija hapo nyumbani wankuletea hela ya hatari na hao nungunungu miiba yake huwa tunaitumia kuweka kwenye mlango ili mwizi asiweze kuingia ndani hii ni kwa mujibu wa mila mbofumbofu
mkuu hivi wanaliwa hawa!!
mkuu wakati wamehamia kwako kwa wingi kabla ya kuwindwa na mbwa vipi uchumi wako ulikuwaje na sasa uko vipi!!!
ha ha ha ha!mkuu nitaning'iniza na mimi mlangoni!!
wanaopatikana south America wanaitwa Armadillo mkuu babu lao. Hao nungu nungu/karunguyeye pale Moshi wapo wa kumwaga.
Na nungunungu ni yupi???Hilo ndo jina lake sahihi. Tatizo waswahili mnataka vitu vingine tofauti na vile mnavyovitumia. Lugha ni sauti za nasibu, kile jamii iitacho ndicho sahihi. Jina la huyo mnyama ni karunguyeye, kama ana jina lingine basi nalo silikatai ila hili ndilo jina lake
Pork .....