Khantwe
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 59,409
- 119,108
Ramadhan Mubarak
Kuna kipindi cha televisheni huwa naangalia kwa jirani yangu mama Imma. Wale wenye ving'amuzi vya startimes kuna channel inaitwa St swahili.... Basi bwana siku ya Alhamisi na ijumaa kuna kipindi kinarushwa kinaitwa ANIKWA
Kwenye hiki kipindi kunakuwa na watu wawili wanaoshea mpenzi inaweza kuwa wanawake wawili au wanaume wawili, wanaandaa kitu kama fumanizi bila mhusika anayewachanganya kujua ila wenyewe wanakuwa wanajua kinachoendelea.
Aisee huwa kunatokea viroja vya kufa mtu, wengi wanaokutwa na maswahibu hayo ni wanaume, huwa wanakuwa na reaction tofauti....mwingine anaweza kutimua mbio, mwingine anachagua mmoja anambembeleza na kuondoka nae.
Kuna huyo mmoja aliniacha hoi akawaambia mimi nina mke na watoto watatu naomba msinisumbue mwingine anakuwa dilemma hajui achague yupi.
Huwa kila siku najiuliza hivi kitu kama hiki kikifanyika hapa kwetu kwa hawa kaka zangu wabongo yule dada anayetangaza kile kipindi wangemteka au ipo siku angechezea kichapo heavy maana kaka zangu kwa kuhusudu michepuko hawana mpinzani, mbaya zaidi hawakubali kuwa ni kosa yaani wanaona ni haki yao na ni hawatakiwi kuhojiwa wala kulaumiwa kwa hilo
Naomba nirudi kwenu wadau, ungekuwa wewe unafanyaje? Ghafla bin vuu unaona umekutanishwa na wapenzi wako wawili mbele ya makamera utafanyaje? Je huyo mpenzi aliyekuletea hayo makamera utaendelea naye? Wewe unaweza kutumia njia hiyo kumuanika mpenzi wako unayehisi anakusaliti? Na ukishamuanika unaendelea nae au ndio kwa heri?
Uzi tayari
Kuna kipindi cha televisheni huwa naangalia kwa jirani yangu mama Imma. Wale wenye ving'amuzi vya startimes kuna channel inaitwa St swahili.... Basi bwana siku ya Alhamisi na ijumaa kuna kipindi kinarushwa kinaitwa ANIKWA
Kwenye hiki kipindi kunakuwa na watu wawili wanaoshea mpenzi inaweza kuwa wanawake wawili au wanaume wawili, wanaandaa kitu kama fumanizi bila mhusika anayewachanganya kujua ila wenyewe wanakuwa wanajua kinachoendelea.
Aisee huwa kunatokea viroja vya kufa mtu, wengi wanaokutwa na maswahibu hayo ni wanaume, huwa wanakuwa na reaction tofauti....mwingine anaweza kutimua mbio, mwingine anachagua mmoja anambembeleza na kuondoka nae.
Kuna huyo mmoja aliniacha hoi akawaambia mimi nina mke na watoto watatu naomba msinisumbue mwingine anakuwa dilemma hajui achague yupi.
Huwa kila siku najiuliza hivi kitu kama hiki kikifanyika hapa kwetu kwa hawa kaka zangu wabongo yule dada anayetangaza kile kipindi wangemteka au ipo siku angechezea kichapo heavy maana kaka zangu kwa kuhusudu michepuko hawana mpinzani, mbaya zaidi hawakubali kuwa ni kosa yaani wanaona ni haki yao na ni hawatakiwi kuhojiwa wala kulaumiwa kwa hilo
Naomba nirudi kwenu wadau, ungekuwa wewe unafanyaje? Ghafla bin vuu unaona umekutanishwa na wapenzi wako wawili mbele ya makamera utafanyaje? Je huyo mpenzi aliyekuletea hayo makamera utaendelea naye? Wewe unaweza kutumia njia hiyo kumuanika mpenzi wako unayehisi anakusaliti? Na ukishamuanika unaendelea nae au ndio kwa heri?
Uzi tayari