Aaliyyah
JF-Expert Member
- Mar 20, 2022
- 15,818
- 37,806
😂😂Hili la kukimbiana linatokea mara nyingi kuliko watu wanavyodhania. Mimi nimesimuliwa na msichana mmoja. Anasema baada ya kuwasiliana kwa meseji na email, walipanga kuonana na jamaa sehemu. Msichana alifanya huo huo ujanja i.e. alitangulia mapema sana kabla ya ule mda waliopanga halafu akabana kwa mbali kidogo kwenye kona. Akasema muda ulipofika akampigia na kumwambia yuko njiani hivyo amwekeze alikokaa (kumbe yuko pale karibu anachunguza). Ghafla akaona bonge nyanya fulani lina kitambi kikubwa (sorry kwenye wenye vitumbo) limebana sehemu linampa maelekezo. Alitimua kama ameona koboko!