Hatutaki elimu ya bure ya Lowassa...

utafanya biashara gani na huu ngao wa umeme? Miaka 25 tunalipia richmond sio mchezo.

Inabidi tumchague Lowasa anaweza akaivunja make wengine wote waliobaki kwenye baraza la maamuzi wameshindwa kulivunja na kamwe hawatalivunja isipokua Lowasa.

Nakupa taadhari, ukimchagua mtu yeyote tofauti na LOWASA jiandae kulipia tena 5years kwa Richmond
 

Ww ni hasara kwa familia na taifa
 
watoa mada wengine sijui mkoje hovyo kuliko hovyo yenyewe.
 
ukitumia jina la mgombea urais wa ccm kupita kiasi ni hatari kwa afya yako.
 
We kweli bado ni zero kabsa katka ulimwengu huu,monduli haijawai kuwa nchi na wala hakujawai kuwepo rais wa monduli, Sera ya elimu inayetekelezwa mtwara au kagera ndio hiyohiyo ya monduli,
 

Hivi unachoandika unakifahamu kweli? Chama tawala kinasemaje kuhusu elimu? Elimu ndo shida TZ
 
.. eddy wewe ni zaidi ya mpumbav usijeukanifanya nikapigwa ban Nyangauu weee
 
Last edited by a moderator:
Ndio hatutaki elimu ya bure tunataka elimu ya CCM ya mzazi kuchangia gharama mfano kwa mtoto wa shule ya msingi tuchangie dawati elfu 20, chakula elfu 30, Mlinzi 3000, ukarabati elfu 10 n.k

CCM hoyeeeeeee
 

Safi sana kwa kumpatia ushauri huyo gamba
 
Ndio hatutaki elimu ya bure tunataka elimu ya CCM ya mzazi kuchangia gharama mfano kwa mtoto wa shule ya msingi tuchangie dawati elfu 20, chakula elfu 30, Mlinzi 3000, ukarabati elfu 10 n.k

CCM hoyeeeeeee

Ccm ziiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Kwanza lowasa akili za kujua elimu anazo? Anaweza kuwambia nini wasomi? Wakati hata nusu pg ya hotuba yake kuiweka kichwani hawezi?

Wasomi wapi hao? Wasomi wakubwa Tanzania wakipewa madaraka huishia kuiba kwa pen , mashirika vyama vya Ushirikina mikataba mibovu na ufujaji mwingi wa pesa hufanywa na wasomi mfano mwanasheria mkuu wa serikali si alibariki wizi wa pesa za escrow?
 
Elimu bure Inawezekana kabisa. Kuna mianya mingi ya ukwepaji kodi Tanzania. Pia kuna vyanzo vingi vya kodi havijafanyiwa kazi Tanzania. Mfano ni property tax. Mtu anayemiliki jumba la billion moja lazima awe na uwezo wa kulipia angalau million 100 kwa mwaka. Wenye nyumba za kupangisha hawalipi kodi yoyote wakati watapata hela nyingi kuliko mshahara wa Mfanyakazi aliyelipa pango la nyumba husika.
Mgombea yeyote mwenye kigugumizi cha kupiga vita ufisadi hawezi kufanikisha elimu bure.

Na ieleweke huu msamiati wa elimu bure unatafsiriwa vibaya. Ni elimu inayoggarimiwa na walipa kodi. Si ya bure!
 

Kule kawe juzi kasema atawajali watumishi wote wa umma ataboresha mishshara yao na kuipunguza kodi kubwa wanayokatwa kwenye mishahara yao, inaelekea wewe huwa haufuatilii hotuba za Lowasa umeamua kukariri Tabia za Nape na wenzake ambao kwa sasa wametafuna pesa za kampeni za magufuli kwa fujo kisha nyie mpo busy kuwasaidia wakati wanatafuna mapesa yote peke yao.
 
Funguka basi ndugu yetu, unataka elimu ya bure ya nani?
Kwanza acha kudanganywa na ghiliba za wanasiasa, hakuna elimu ya bure labda waitwe Wakongo au Wanigeria waje hapa ndio watakuwa wanasomeshwa bure. Mtanzania elewa kuwa hakuna elimu ya bure kama ni lazima wananchi walipe kodi ndipo elimu itolewe - hiyo wanayodai itakuwa ya bure.
Ijulikane kuwa ni wajibu wa serikali kukusanya kodi na hiyo kodi iwarudie wananchi kwa namna ya kupewa elimu, afya, miundo mbinu, maji n.k. Haijalishi tunalipa kodi kiasi gani lakini tunahitaji serikali itakayo kusanya kodi na tukaona manufaa ya kulipa kodi, wenzetu kama Sweden naambiwa wanlipa kodi asilimia sitin na tano ya mapato yao lakini hawalalamiki na wanfurahi kulipa kodi kwa sababu inawarudia na huduma wanazopata kutoka kwa serkali yao ni bora kabisa.
Lazima tubadilike na kuwaelewa wanasiasa wetu ati utasikia CCM au CHADEMA watatoa elimu bure, na tulivyo malofa tunapiga vigelegele. Ni lazima wananchi tufike mahali tuidai serikali huduma hizi kwa sababu tunalipa kodi. Na kodi tunayoiongelea hapa sio PAYE tu, mwananchi aelewe kuwa kila unaponunua dukani au sokoni na unapolipia huduma kama umeme, maji, matibabu kwenye hospitali za binafsi kuna kodi humo ikiwemo asilimia kumi na nane ya VAT - Zinduka mtanzania unaghilibiwa eti utapewa elimu ya bure, ni haki ya watoto wetu kupewa elimu na serikali kwani inakusanya kodi.
Wakati huu ni wa kuchagua serikali itakayotumia kodi zetu vizuri ili itoe huduma za jamii zilizo bora na pasipo kututaka eti tuchangie kwa kupangiwa kiwango. Hatukatai kuwa tunaweza kuchangia lakini si kwa kulazimishwa, tutachangia kwa hairi na baada ya kuona kweli serikali yetu imezidiwa na ni lazima tuone kweli imejitahidi nasi tutachangia - iwe ni nguvu zetu na si tulazimishwe kuwa michango ya pesa tu.
Naomba kuwasilisha kwa kuyanyumbulisha haya kwa upendo.
 

Tanzania kuna pesa nyingi inapotelea midomoni mwa wachache hiyo pesa ikiwekewa misingi bora hata huduma bure mahosipitalini itawezekana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…