Hatuombei yatokee lakini ukweli ndio huo

Hatuombei yatokee lakini ukweli ndio huo

mavumbi

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2013
Posts
596
Reaction score
328
Wanabodi:
Rais wa Marekani Joseph Biden ana umri wa miaka 80
Mgombea Urais Kenya Raila Odinga ana Umri wa Miaka 78
Makamu wa Rais wa Marekani ni Mwanamama
Mgombea Umakamu wa Rais Kenya Ni Mwanamama
Mzee Raila Odinga akishinda Urais Mama Karua anakuwa Makamu

Yakitokea kama yaliyotokea Tanzania tutaona mabadiliko makubwa sana

Taifa lenye nguvu duniani kuongozwa na mwana mama tena wa asili ya Uhindini
Jirani zetu watapata fursa ya kujifunza kwa Tanzania

Na maeneo mengi katika nchi mbali mbali wataulizana tunafanyaje siku nyingine?

Given: Kila mtu ana matamanio yake ila wewe na mimi tuna haki ya kutafakari tu endapo.........
na mimi natafakari tu
 
Mkuu wale wenzetu Marekani wamegatua madaraka,hawajampa Rais madaraka yote na ndiyo maana unaona chizi Trump aliweza kuongoza lakini alikuwa akileta kichaa chake anakutana na system inambana,kule hamna mambo ya zidumu fikra za Mwenyekiti bali Kuna zidumu fikra za kitaasisi.

German pia Mama Angel Merkel aliweza kuongoza bila shida,Sasa Afrika kazi ipo,sisi wenyewe hapa tunaomba Mungu mambo yaende vizuri kwa kweli!
 
Ila kumuweka mwanamke nafasi kama hizi ni risk kubwa sana ambayo CCM hawatadhubutu kuirudia tena
Kwani hao Marais wanaume wamefanya nini miaka 60 sasa? Kila ufisadi nchi hii ulifanywa na wanaume.

CCM imechoka hata angewekwa mwanaume ubovu ungeendelea pale pale...
 
Back
Top Bottom