Hatimaye wakili Peter Kibatala kumtetea Gwajima

Hatimaye wakili Peter Kibatala kumtetea Gwajima

safari hii hakuna cha kipalata wala cha nani,asipopeleka vitu vinavyotakiwa watamfuata kwa style ya tanganyika jerk
Siwezi kukupinga kwa sababu Tanzania ni nchi ya kidemokrasia ambayo bado tunatumia sheria tulizorithi toka kwa wakoloni sheria ambazo ukishindwa kulipa kodi ya kichwa walikuwa wanakuja nyumbani na kukucharaza bakola mbele ya mkeo na kuchukua mifugo yako.
 
Shukrani sana,,,mungu ni mwema tutashinda dhidi ya wadharimu hawa
Daa!!! Mungu gani huyo unayemshirikisha kwenye huu upuuzi huyo Mungu ndiyo alimtuma Gwajima amwambie Askofu Pengo anavaa pampers?
 
Binafsi nafaham Gwajima ni magician lakini kwa hili police wanaonekana kutumiwa na chama kinachounga mkono katiba ya 6. Alikamatwa kwa kosa la kumtukana Pengo tunataka ashtakiwe na kuhukumiwa kwa kosa hilo ili iwe fundisho kwa waropokaji wengne. Haya mambo mengine ni kudhihirisha jesh la polis linatumika hovyo.
 
Daa!!! Mungu gani huyo unayemshirikisha kwenye huu upuuzi huyo Mungu ndiyo alimtuma Gwajima amwambie Askofu Pengo anavaa pampers?

wewe msukule usimuingize pengo kwenye huo upuuzi kwani huyo pengo kaishasamehe!
 
Wakili msomi Mallya aliyemsindikiza Gwajima wakati anapewa maagizo ya mdomo na polisi alikubalije? Kweli experience matters.

Plus, wakili atapokeaje maagizo ya kusubmitt documents bila kujiridhisha yanatokana na kifungu kipi cha sheria!
No law no offence. Kuna uzi humu memba fulani alitoa wazo la Gwajima kubadili wakili wengi tuliona hivyo

Mkuu, John Mallya inaonekana bado uzoefu unasumbua kidogo hivyo inasemwa kwamba watu walikuwa wakipima uzoefu kulingana na mwenendo wa hili jambo.

Ni sheria na kufahamu vifungu kwa kina maana makabati ya Kibatala yalojaa vitabu vya sharia ni mengi kuliko ya Mallya.
 
Kama kuna Askofu muoga hapa Tz, basi wa kwanza ni Gwajima!!

Na pia hana uwezo kabisa wa kujenga hoja.
 
Kibatala mtamu kama mcharo. Nadhani gwajima anaandamwa kwakuwa anamuunga mkono Lowasa. Haya mambo ya kuhoji mali zake ni matusi ya kujitukana serikali yenyewe. Kwamba taasisi zake haziko makini
 
Huyu Kibatala mzoefu,Mallya alikuwa anapelekwa pelekwa tu na polisi.Wakiambiwa leta hiki wanapeleka.Kesi ilikuwa kumtukana Pengo hayo mengine yanatoka wapi?Sasa kwa kibatala polisi watatia adabu.Vifungu kwa vifungu tu.

Natamani wamuongeze
T. LISSU. Hapa Polisi hadi watakodi wanasheria kutoka Mkono Advocates!
 
Huyu Kibatala mzoefu,Mallya alikuwa anapelekwa pelekwa tu na polisi.Wakiambiwa leta hiki wanapeleka.Kesi ilikuwa kumtukana Pengo hayo mengine yanatoka wapi?Sasa kwa kibatala polisi watatia adabu.Vifungu kwa vifungu tu.
Victoire fani yako ni ipi?
 
Tutaongeza na kina Majura Magafu! Wapambane kwa vifungu!
Wampeleke mahakamani, hawana mamlaka ya kuhoji hati zozote! Hiyo ni kazi ya Mahakama!
Warudi kutafuta zile silaha zao zilizoporwa vituo vya polisi!
 
Sasa Askofu Gwajima amepata wakili mahiri. Ni kama hakuwa anapata ushauri uliotakiwa. Yule Mallya ilionekana kama anatii tu maagizo ya polisi kwa staili ya 'ndio mzee'.

Kwa Kibatala kitaeleweka. Movie ndio kwanza imeanza.
 
Mkuu Ritz heshima yako, sasa hata kama Gwajima anamakosa ya kutumia hayo maneno makali ya kuudhi, si wamshitaki kwa hilo kosa, haya ya kutakiwa kuleta mapaka hati ya kanisa, bodi ya wadhamini, mchanganuo wa mapato yake na malizake yanatoka wapi etc, yanaingilianaje mkuu>> huoni kuna jambo limejificha hapo, Gwajima kaanza leo kuwa na kanisa??.. Wamuhumuku kwa kosa alilotenda, kama kuna mengine wafungue shauli lingine.. tuwe wakweli mkuu....
Daa!!! Mungu gani huyo unayemshirikisha kwenye huu upuuzi huyo Mungu ndiyo alimtuma Gwajima amwambie Askofu Pengo anavaa pampers?
 
Hiyo barua isiwatishe sana watu msiojua sheria kwa kifupi jeshi la polisi limepewa mamlaka makubwa ya kuchunguza jambo lolote ambalo wanahisi ni la kijinai kupitia sheria ya mwenendo wa mashauri ya jinai kuna vifungi kadhaa vinavyoainisha nguvu zao za kisheria jambo ambalo alipaswa kuwataka polisi ni kwamba mteja wake anakabiliwa na kosa lipi? hapo ndio pa kuanzia na huku akihakikisha kila hatua ya mahojiano anakuwa na mteja wake.
 
Hawa watu wakiamua hata usimamishe Wakili mzuri kiasi gani watakufunga tu nasema Watakufirisi tu...!!

Kikubwa hapa huyo Gwajima awaombe radhi ikibidi awadanganye hata kuwapigia kampeni kanisani kwake, vinginevyo ataokomea nakwambia mkuu jamaa wamedhamiria kumtokomeza na hakika atatokomea ni suala la muda tu, Huu ndio ukweli mchungu..!!

Unakumbuka Amri Kombe alipigwa risasi huku kanyoosha mikono juu kama ishara ya Kusarenda pamoja na kwamba hakushika hata fimbo??

Naam aliitwa Jambazi na akauliwa kama Jambazi..!!! Kisha.waliomuua wamasema ooooh tulukosea tukadhani ni Jambazi...!!!

BACK TANGANYIKA
Unachoongea kuhusu kupotezwa gwajima sio kweli, acha uoga wewe, nchi inaongozwa kwa sheria, angalia sasa baada ya polisi kupata hiyo barua watafanyaje! Hamna kitu! Kwa sababu wamezoea kuwaoshea maboya. Kakobe alikosana nao toka 2000 wamemfanya nini? Hakuna dhambi mbaya kama ya uoga.
 
Jambo lingine la kufahamu Polisi wakisha kamilisha kuchukua maelezo yao ni lazima jalada lipelekwe kwa DPP wanasheria wa serikali ili kusoma na kuangalia katika jicho la kisheria kama kuna kosa ama makosa ya kijinai ili jalada liwasilishwe mahakamani ama kulifunga kama ushahidi haupo.
 
Back
Top Bottom