Hatimaye wakili Peter Kibatala kumtetea Gwajima

Hatimaye wakili Peter Kibatala kumtetea Gwajima

Wakili msomi Mallya aliyemsindikiza Gwajima wakati anapewa maagizo ya mdomo na polisi alikubalije? Kweli experience matters.

Plus, wakili atapokeaje maagizo ya kusubmitt documents bila kujiridhisha yanatokana na kifungu kipi cha sheria!
No law no offence. Kuna uzi humu memba fulani alitoa wazo la Gwajima kubadili wakili wengi tuliona hivyo
 
Hawa watu wakiamua hata usimamishe Wakili mzuri kiasi gani watakufunga tu nasema Watakufirisi tu...!!

Kikubwa hapa huyo Gwajima awaombe radhi ikibidi awadanganye hata kuwapigia kampeni kanisani kwake, vinginevyo ataokomea nakwambia mkuu jamaa wamedhamiria kumtokomeza na hakika atatokomea ni suala la muda tu, Huu ndio ukweli mchungu..!!

Unakumbuka Amri Kombe alipigwa risasi huku kanyoosha mikono juu kama ishara ya Kusarenda pamoja na kwamba hakushika hata fimbo??

Naam aliitwa Jambazi na akauliwa kama Jambazi..!!! Kisha.waliomuua wamasema ooooh tulukosea tukadhani ni Jambazi...!!!

BACK TANGANYIKA
 
Hii issues Gwajima hatoki....imekula kwake...!!!
 
kwa huu uelekeo muda wowote polisi watafuta kesi
 
hakuna sheria yeyote inayowapa polisi mamlaka ya kumlazimisha mtu kutoa maelezo mbele yao na kuleta vielelezo. kwanza wanafanya hivyo kwa kosa gani? la kumtukana pengo ndio watake hadi hati za kanisa? hizo zinahusiana vipi na kutoa lugha ya matusi? wakili wa gwajima alilala sana, amewaachia polisi kumchambua gwajima wapendavyo na kibatala kama asingeingilia kati walikuwa wanaenda kummaliza kabisa wakati hawana nguvu kisheria kufanya hivyo. kibatala aibisha hao maccm na ninaomba tundu lisu naye atie timu hapo. hawa ccm waonevu sana.
 
Utamu upo hapo. Peter Kibatala ni kichwa cha sheria pale Mzumbe University walimpika vizuri huyu jamaa na hapa Pengo na Kova wake lazima walale mbele

Wala usimuingize Pengo, Pengo hajamshitaki mtu yeyote juu ya hilo, ni Kova na Abubakari wake wanajuana wenyewe huko.

Naona polisi wanataka kuchukua na majukumu ya TRA kufuatilia kama mapato na matumizi ya Gwajima yanameet vigezo vya kisheria.Sitarajii polisi kujibu barua hiyo maana watajifunga.

Natarajia Kamanda Kova kuonywa na IGP juu ya mikanganyiko hii isiyozingatia uweledi
 
Hapo sheria na sio ubabe wa police

Haya mambo ya polisi kweli ya ajabu!!! Sasa kutoka kwa Pengo mpaka mali zake na hati zake, Jamani tunaelekea wapi?Wenye kujua sheria teteeni hii ni dhuluma ya uwazi, nafuu itoke polisi iende mahakamani ambayo itakuwa kesi kati ya Polisi na Gwajima. Gwajima achukue tahadhari kuhusu mstakabali wa maisha yake.
 
Hii imekaa vizuri...,maana mtu anaamua kuingiza kinyongo chake cha siku nyingi katika tuhuma tofauti. Ni muhimu kuwa na watu kama kina Gwajima na Mtikila ili kuweka sawa mambo taifa ama kiongozi anapokwenda mrama.
 
Pengo hana wafuasi.Wakatoliki tunaongozwa na taratibu za kanisa sio matakwa ya mtu.
Pengo nje ya kofia,fimbo na mavazi mengine hana ufuasi wowote.
Hamna mtu wa kumpigania Pengo kama Gwajima.

Pengo aliishayasamehe yote na hajaripoti polisi juu ya hilo.

Mshtaki wa Gwajima anamfahamu Kova tu
 
Si mkubali Gwajima lakini kwa lile ambalo police walitaka wamfanyie sio haki Kosa ni kumtukana Pengo hayo mengine police walikuwa wanataka nini..!? nimefurahi sana kuona kibatala kaingia hapo ushindi ule kwa Gwajima
 
Utamu upo hapo. Peter Kibatala ni kichwa cha sheria pale Mzumbe University walimpika vizuri huyu jamaa na hapa Pengo na Kova wake lazima walale mbele

Katika wanasheria nguli wa Tanzania Peter Kibatala ni nani?
 
Huyu Kibatala mzoefu,Mallya alikuwa anapelekwa pelekwa tu na polisi.Wakiambiwa leta hiki wanapeleka.Kesi ilikuwa kumtukana Pengo hayo mengine yanatoka wapi?Sasa kwa kibatala polisi watatia adabu.Vifungu kwa vifungu tu.

Hahahaha hapa ubabaishaji ndo huwa unaishia!
 
Back
Top Bottom