Wandugu natumai mu wazima.
Ni mwezi mmoja na nusu umepita tangu nifanye maamuzi magumu ya kuachana na baba mtoto wangu.
Ila pia ni mwezi mmoja na nusu wa machungu ya moyo maana nilifanya maamuzi hayo nikiwa bado nampenda ila sikuwa na jinsi kwa maana nilikuwa kwenye mahusiano yenye mateso.
Baada ya kumwambia maamuzi yangu jamaa alikasirika sana na kutishia kutotaka kujua lolote la kuhusu mtoto.cha kushangaza alirudi tena na kuanza kunitishia maisha yangu na ya mwanangu kama tu ataona mimi nina mtu mwingine, na story haikuishia hapo alidiriki kutuma msg kwa mama yangu mzazi kumwambia maneno hayo ya kutisha pamoja na kwamba mama yangu ndio chanzo cha mimi kumuacha kwasababu hakuwahi kumshauri yeye wala mimi.na pia alinitumia msg nyingi za matusi ambayo siwezi kuyaandika hapa.
Hatimaye juzi kanitumia msg kuwa na yeye anamove on hajali kama huyo mtu anampenda au la na tuone mwisho wangu.
kwa kipindi chote hiko sio kama ninaona raha yeye kuhangaika ila na mimi pia nilikuwa naumia na mpaka sasa hivi i wish kungekuwa na miujiza ya kumbadilisha tabia zake. namshukuru Mungu sasa hivi nimezoea na pia cha kushangaza leo katuma fees ya mtoto from nowhere.
Sasa basi, kisa cha mimi kuandika hapa leo ni kwambaa,wakati huo wote kwa muda wa kama miaka miwili kuna kijana ambaye nilikuwa nikimuhadithi matatizo yangu ananishauri na vitu kama hivyo ni rafiki tu wa kawaida na tunaelewana sana, bila kujua yule kijana ananipenda. baada ya kujua tumeachana huyu kijana kazidisha kuwa karibu na anadiriki kunambia mimi ndo mke wake siku zote alikuwa anajua sitolast na baba watoto wangu. afu kaniintroduce kwa kaka zake na sister zake na marafiki, na anapenda kuongelea mambo ya ndoa na jinsi tutakavyoishi pamoja na mwanangu etc, nikisema mi sipo tayari na mahusiano anakasirika mbaya hatoongea siku nzima.
tatizo ni kuwa naona kama yuko too fast na pia ni mdogo kwangu kwa miaka miwili. ni kijana mwenye hekima na busara na mwenye sifa zote za kuitwa baba na mume bora.
naombeni mawazo yenu ya busara wanaMMU
Ni mwezi mmoja na nusu umepita tangu nifanye maamuzi magumu ya kuachana na baba mtoto wangu.
Ila pia ni mwezi mmoja na nusu wa machungu ya moyo maana nilifanya maamuzi hayo nikiwa bado nampenda ila sikuwa na jinsi kwa maana nilikuwa kwenye mahusiano yenye mateso.
Baada ya kumwambia maamuzi yangu jamaa alikasirika sana na kutishia kutotaka kujua lolote la kuhusu mtoto.cha kushangaza alirudi tena na kuanza kunitishia maisha yangu na ya mwanangu kama tu ataona mimi nina mtu mwingine, na story haikuishia hapo alidiriki kutuma msg kwa mama yangu mzazi kumwambia maneno hayo ya kutisha pamoja na kwamba mama yangu ndio chanzo cha mimi kumuacha kwasababu hakuwahi kumshauri yeye wala mimi.na pia alinitumia msg nyingi za matusi ambayo siwezi kuyaandika hapa.
Hatimaye juzi kanitumia msg kuwa na yeye anamove on hajali kama huyo mtu anampenda au la na tuone mwisho wangu.
kwa kipindi chote hiko sio kama ninaona raha yeye kuhangaika ila na mimi pia nilikuwa naumia na mpaka sasa hivi i wish kungekuwa na miujiza ya kumbadilisha tabia zake. namshukuru Mungu sasa hivi nimezoea na pia cha kushangaza leo katuma fees ya mtoto from nowhere.
Sasa basi, kisa cha mimi kuandika hapa leo ni kwambaa,wakati huo wote kwa muda wa kama miaka miwili kuna kijana ambaye nilikuwa nikimuhadithi matatizo yangu ananishauri na vitu kama hivyo ni rafiki tu wa kawaida na tunaelewana sana, bila kujua yule kijana ananipenda. baada ya kujua tumeachana huyu kijana kazidisha kuwa karibu na anadiriki kunambia mimi ndo mke wake siku zote alikuwa anajua sitolast na baba watoto wangu. afu kaniintroduce kwa kaka zake na sister zake na marafiki, na anapenda kuongelea mambo ya ndoa na jinsi tutakavyoishi pamoja na mwanangu etc, nikisema mi sipo tayari na mahusiano anakasirika mbaya hatoongea siku nzima.
tatizo ni kuwa naona kama yuko too fast na pia ni mdogo kwangu kwa miaka miwili. ni kijana mwenye hekima na busara na mwenye sifa zote za kuitwa baba na mume bora.
naombeni mawazo yenu ya busara wanaMMU