Hatimaye Mbowe atoa ya moyoni kuhusu Halima Mdee

Hatimaye Mbowe atoa ya moyoni kuhusu Halima Mdee

Cicadulina

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2015
Posts
1,006
Reaction score
2,431
“Nilikwenda Nairobi, nikamuita Halima Mdee, akasafiri na Ester Bulaya. Nimekuwa nao siku 7 nikimshawishi Halima anieleze nini kilitokea, aligoma. Nikamuomba aache huo ubunge, nimemtafutia kazi Nairobi na RSA na atalipwa US$15,000 (Shs. 34.9M), Halima akagoma”.

“Halima ananiuma kwa sababu nyingi. Halima nimemtoa chuo kikuu akiwa msichana. Nimempika kwa gharama sana. Ndiyo maana nilitumia juhudi zangu zote hata kuwaita wazazi wake, wamshawishi aachane na ubunge wa damu wa Magufuli, anaharibu career yake, hakunielewa”.

“Nairobi nilipowaita Halima na Bulaya nilikuwa nakutana nao kila siku. Tunakula na kunywa pamoja. Nikimbembeleza Halima aachane na ubunge wa damu, mtetezi ni Magufuli, hayupo. Nikamuomba anieleze nini kilitokea, Hawakuwahi kunieleza hadi naondoka kwenda Dubai”.

“Kama haya nayoeleza hapa kuhusu Halima nadanganya, Halima yupo hapa asimame na aseme kama ni uongo. Akanushe kuwa sikumtafutia kazi NRB na RSA alipwe Shs. 34.9M, au kama sikuzungumza na wazazi wake, au sikumuita NRB kumshawishi aachane na ubunge wa Magufuli”.

“Siyo kazi rahisi kufukuza wanawake 19 ambao umewajenga kwa gharama, wapo wote mbele ya baraza kuu, nitawaomba sasa dada zangu hawa, aliye na jambo la kuzungumza asogee mbele asemee”.

Baada ya hapo mwenyekiti Freeman Mbowe akawaambia wajumbe “nadhani dada zangu wameona hawana kitu cha kuongea na wajumbe wa baraza kuu, mheshimiwa katibu mkuu, sasa nikuombee tuendelee na taratibu za kitaasisi, tusikilize rufaa zao na tufikie maamuzi” Wajumbe wakapiga kura!
 
Shida ni kwamba Mbowe alitaka vijana waondoka kama wakimbizi wa kisiasa kama alivyofanya Lema lakini ikagonga mwamba.

Sasa hakuna haja ya kuwaonea huruma akina Mdee wameshaamua kuchukua hamsini zao na maisha yanaendelea.
Alaaaaa kumbe ni mpango wa kuwa wakimbizi wa kisiasa walio wengi eee?!!🤣🤣

Kuna maslahi mengi angeyapata 🤣🤣

#Siempre JMT🙏
 
Kwani mwisho wa career yake ni ubunge au kasha fikia umri wa kustaafu? Hawezi kwa minika tena kwa chama.
Nashukuru kwa kunieleza kuwa alikueleza mawanda ya siasa zake....👍
 
"Halima akasafiri na Ester Bulaya"....nimeelewa hapo tu, mengine hata sina muda nayo maana najua kila mwanasiasa ana dau lake la kununuliwa! Tukifukua makaburi ya pesa aliyopewa Mbowe na kubadiri gea angani Lowassa kubwa la mafisadi akawa msafi na kugombea urais asilalamike
 
Hata mi nimewaza sana hili
Kwanini baraza kuu halijaangalia kua tulikua kwwnye kupindi cha mpito
Maana mtawala likua ni herode
Nadhani wawasamehe tu bure na mambo mengine yaendelee..!
Wakati wa Herode ilibidi Yesu akimbilie ukumbizini Misri kuliko kukaa kwenye utawala wa Herode mwishowe limuuwe. Tujifunze.
 
Back
Top Bottom