Hatimaye CHADEMA kuanzisha media zake

Hatimaye CHADEMA kuanzisha media zake

Bila kujali matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu, ili kukijenga zaidi chama na ili tuweze kupambana vizuri zaidi na chama kama CCM katika chaguzi zijazo, tunahitaji kuwa na vyombo vyetu wenyewe vya habari kama vile magazeti,Television,Radio na pia tuwe na walau mtandao mmoja wa kijamii ambao utakuwa ni Forum huru kwa wananchi wa vyama vyote kuutumia.

Nashauri hivi kwasababu nimegundua kuwa tunahitaji kuwa na media zetu wenyewe ili tuweze kupambana ipasavyo na hawa wenzetu wenye uwezo wa kuteka media kwasababu ya uwezo mkubwa wa kifedha waliona.

Chama kinaweza kuandaa mkakati ikiwa ni pamoja na kushirikisha wananchi kupitia Harambee mbali mbali,kutafuta wafadhili na njia zingine zitakazofaa kufanikisha mkakati huu.

Utekelezaji wa mipano mingine unaweza kuwa ni wa muda mfupi kama vile kuanzisha Forum na mingine inaweza kuwa ni ya muda mrefu kama vile kuwa na Televisio kwani mpango huu unaweza kuwa ni wa gharama zaidi lakini naamini hakuna kinachoshindikana.

Hata hivyo,kabla ya kufikiri kuanza utekelezaji wa mipango hii,CHADEMA lazima sasa wajipange kuwa na jengo lao wenyewe kama Makao Makuu ya Chama.

Itapendeza zaidi kama watafikiri kujenga jengo la gorofa mbili mbili au tatu na hata zaidi kama wataweza na baadhi ya floor wakazipangisha ikawa ni mradi endelevu wa chama na hela watakazozipata zikatumika kuanzisha hizo media pamoja na kuendesha shughuli nyingine za chama.

Naamni tumechelewa tena sana tu ila wazungu wanasema, "better late than never".

Narudi,uchaguzi ukiisha,bila kujali tumeshinda au tumeshindwa,tuanze kufikiria uchaguzi wa 2020 na mbinu zake.

CHADEMA, as a political party,we need transformation;more important,we need to invest for the better future of our party.

Fund raising kila mwaka wa uchaguzi haipendezi na watu watatuchoka na watuona hatuna mipango ya kujiendesha kwa fedha zetu wenyewe zaidi ya kutegemea ruzuku na michango mbalimbali.

CHADEMA, sasa tufanye Fund Raising kwa ajili ya kujijengea uwezo wa kiuchumi na si tena kwa ajili ya kujiendesha kama chama.
 
hiyo redio siipatii picha matangazo ya bilicanas na tanzania daima yatakavyopewa kipaumbele.. makala zote kumsifia mbowe
 
Hiyo radio ni ya chadema au ni ya Mbowe na familia yake? Kama ni ya chadema kwa nini iitwe kilimanjaro media group?
 
Habari jf
Nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu, kwanini vyama vya siasa Tanzania havina vituo vya Television?

Kwa taarifa nilizonazo toka kwa kada mkongwe wa CHADEMA nikwamba wako mbioni kuanzisha TV yao kama kitega uchumi cha chama..
Hii imekaeje wadau?
Nawasilisha.
 
Siamin kwan nimemis sana uhuru wa habar coz kma kwl kiongoz wa nnchi anasema kila cku kwamba yy ni kiongoz wa watanzania walio chin na anatumbua live kwa nn na yy asiweke waz kukosolewa live?
 
Habari zilizonifikia na za kuaminika ni kuwa Mchakato wa Cdm kuanzisha vyombo vyake vya habari uko kwenye hatua nzuri.
Vyombo hivyo vitakavyojulikana kama Chadema media kwa kuanza wataanza na Radio na tayari CDM wameshasainishana mkataba na kampuni ya TTCL ili ku lease spaces za transmission ya mawimbi yao.

TTCL ndio kampuni pekee tanzania yenye facility za nsmna hiyo ambapo Radio karibu zote nchini za serikali, vyama na watu binafsi hu lease spaces kwa ajili ya transmission.

HONGERENI CHADEMA!

UPDATES
Ukweli halisi wa habari hii baada ya kufuatilia kwa kina ni kuwa Bwana Mbowe kupitia kwa Mke wake Bi Lilian Mtei ndio wanaoanzisha redio yao na kwamba media yao itaitwa Kilimanjaro Media Group. Michakato ya kwenda TCRA na TTCL imeshafanyika tayari.


Sasa hiyo itakuwa media ya CDM au ya bw. na bibi mbowe???????
 
Back
Top Bottom