BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,283
Aaache upuuzi wake huyu Chakubanga. Hakuna mahali popote pale ambapo katiba imesema Rais akosolewe kwa siri. Yeye kuwadhalilisha Watanzania na kuwateka, kuwatesa na kuwaua sawa lakini yeye akikosolewa hadharani KOSA.
Akatubu tu mara moja hakuna jinsi.
- Akatubu mara moja na aachane na sheria zake kandamizi zote zifutwe mara moja. Sheria kandamizi kuhusu habari na mtandao zifutwe. Magazeti yaliyofungiwa yafunguliwe mara moja
- Watwambie Watanzania alipo Ben Saanane na Mwandishi wa Mwananchi. Kama wako hai waachiwe mara moja na kama wamewaua maiti zao wakabidhiwe familia zao au waonyeshe makaburi yao.
- Majina ya Watanzania ambao miili yao iliokotwa ufukweni yatangazwe hadharani haraka sana na tuambiwe sababu za kuuwa kwao.
- Vyama vya siasa viruhusiwe mara moja kufanya shughuli zake za kisiasa nchini na kutoingiliwa na yeyote yule iwe wakuu wa mikoa, wilaya au polisiccm
Akatubu tu mara moja hakuna jinsi.
Baada ya maaskofu kuliamsha dude kuanzia kipindi cha Salam za krismasi na salam za mwaka Mpya, hatimae katibu mwenezi CCM ndugu Humphrey polepole amejitokeza na kuwaomba maaskofu waishauri serikali sirini kwani kwa hali ilivyo sasa ni kama wanaidhalilisha, Rais yuko tayari kupokea ushauri na kuufanyia kazi.
My take
Kila shetani ana mbuyu wake ukimya wa maaskofu na mashehe umetuumiza sana kama taifa na sina shaka wameamuka usingizini baada ya Askofu niwemugizi kuelekezewa bomba la moshi, pia salam zangu za pole ziwafikie Clouds Media
