Hatimae Polepole awaangukia Maaskofu

Hatimae Polepole awaangukia Maaskofu



Baada ya maaskofu kuliamsha dude kuanzia kipindi cha Salam za krismasi na salam za mwaka Mpya, hatimae katibu mwenezi CCM ndugu Humphrey polepole amejitokeza na kuwaomba maaskofu waishauri serikali sirini kwani kwa hali ilivyo sasa ni kama wanaidhalilisha, Rais yuko tayari kupokea ushauri na kuufanyia kazi.

My take
Kila shetani ana mbuyu wake ukimya wa maaskofu na mashehe umetuumiza sana kama taifa na sina shaka wameamuka usingizini baada ya Askofu niwemugizi kuelekezewa bomba la moshi, pia salam zangu za pole ziwafikie Clouds Media


Hivi yeye rais hata akiboronga mazima basi maaskofu wayasemee chinichini
 


Baada ya maaskofu kuliamsha dude kuanzia kipindi cha Salam za krismasi na salam za mwaka Mpya, hatimae katibu mwenezi CCM ndugu Humphrey polepole amejitokeza na kuwaomba maaskofu waishauri serikali sirini kwani kwa hali ilivyo sasa ni kama wanaidhalilisha, Rais yuko tayari kupokea ushauri na kuufanyia kazi.

My take
Kila shetani ana mbuyu wake ukimya wa maaskofu na mashehe umetuumiza sana kama taifa na sina shaka wameamuka usingizini baada ya Askofu niwemugizi kuelekezewa bomba la moshi, pia salam zangu za pole ziwafikie Clouds Media


Ukipenda kusifiwa hadharani ukubali kukosolewa hadharani vilevile!. The two things are synchronized!
 
Kupambana na askofu kakobe au kiongozi yeyote yule wa dini inamaanisha unataka kupambana na wananchi maanba wako wengi wanaoamini katika wao. Hivyo inapofika wakati unatakiwa tu uchomwe sindano ili upone jabo inauma inapoingia mwilini
 
Hii ni kama movie ya action .star kakobe na maaskofu wanaoikosoa serikali .upande wa pili magu ndiyo mbabe sasa star wa movie kawachapa wote walijiyokeza coz wameshindwa mapema kwa kushindwa kujibu hoja.tunamsubil atoke mafichoni magu.
 
Wale wapumbavu waliojazana mitandaoni kudhani kwamba kila mtu ataogopa na Usalama wa taifa, basi sasa wajue kwamba dini ni zaidi ya usalama wa taifa lolote. Ingekuwa ni aibu eti maaskofu waogope usalama wa taifa waache kusema.

Askofu katumwa na Mungu na anamuogopa Mungu haogopi jeshi, polisi, mgambo au usalama wa taifa.

Kumbe ni ya kweli lakini yawe ya siri ahsante polepole

Sindano za maaskofu kumbe kidogo zinawaingia kumbe,
Maaskofu ongezeni Cc tafadhali
 
Itafika wakati tutaelewana tu.

Na bado wale wengine hawajaamka.

Shime ongozeni kwa haki na taratibu tuliojiwekea pasi na kuvuruga nchi.
 
Polepole sahau hayo mawazo ya kipagani ya kuwapangia watumishi wa Mungu nini cha kufanya, wao wanaongozwa na Mungu siyo wewe


Baada ya maaskofu kuliamsha dude kuanzia kipindi cha Salam za krismasi na salam za mwaka Mpya, hatimae katibu mwenezi CCM ndugu Humphrey polepole amejitokeza na kuwaomba maaskofu waishauri serikali sirini kwani kwa hali ilivyo sasa ni kama wanaidhalilisha, Rais yuko tayari kupokea ushauri na kuufanyia kazi.

My take
Kila shetani ana mbuyu wake ukimya wa maaskofu na mashehe umetuumiza sana kama taifa na sina shaka wameamuka usingizini baada ya Askofu niwemugizi kuelekezewa bomba la moshi, pia salam zangu za pole ziwafikie Clouds Media
 
Angalau Polepole amejaribu. Hata hivyo kauli yake iliyohusisha maaskofu (na wapakwa mafuta wengine wa kidini?) na itikadi za vyama vya siasa ina kasoro kubwa ingawa ndiyo hasa inayosimamia msimamo wa wana ccm wengi na serikali yao iliyo madarakani. Kwamba kiongozi wa dini anayeonyesha kuunga mkono na itikadi kinyume na ya ccm ni adui wa wana ccm! Hakuna katika kauli yake anaonyesha je yule anayeiunga (tena waziwazi) ccm naye awe adui wa wasioiunga mkono?

Suala la pili analotakiwa kulisemea ni pale makada wa chama tawala wanapojitokeza kutoa kebehi kwa mtu yeyote anayejaribu kushauri yanayoonekana ni makosa ya serikali iliyoko madarakani. Tunaona hata viongozi waandamizi wa serikali wanawaita hao viongozi wa dini vichaa na mashetani! Ni ajabu kwamba yule unayemfikiria yu kinyume na itikadi yako unayoiamini kwako wewe ni shetani wakati kuna wananchi mamilioni wanaona ni kiongozi wao wa kiroho. Lakini pia ususahau ni mabaya hayo hayo yalisemwa huko nyuma (na watu walio kinyume na itikadi ya chama tawala) ndiyo yalimbeba rais aliyeko madarakani!

Tumemsikia hata mkuu wa nchi akitoa kebehi ya wazi kwa anaowaona kuwa ni washindani wake wa kisiasa. Inakuwaje mkuu anaweza kutumia maneno na majina ya kiutani tuliyoyatumia huko mashukeni ya 'ngwini' katika hotuba zake kuonyesha mtu anayekosia takwimu za kiuchumi. Hao 'ngwini' ndio walioko benki kuu, ndio wasaidizi wake kila sehemu ya serikali inakuwaje unawadharau, pengine kwa kuwa tu wewe ulisoma sayansi! Huwezi kuendesha nchi kwa wasomi wa aina fulani tu. Tunategemeana. Na wewe kama kiongozi mkuu unapaswa kuwaunganisha wote ili kila mmoja atimize wajibu wake bila kujiona ni dhalili.

Kisha kuna katabia ambako pia hakafai kamejijenga katika taasisi za umma. Kwamba mtu yeyote anayesema yasiyopendeza masikioni mwa viongozi walioko madarakani wanaandamwa na taasisi hizo tena kwa uwazi. Hii ikiwa na nia pengine ya kudhalilisha na kutia hofu. Hatujasikia serikali au chama tawala ikilikemea hili. Polepole anatakiwa kulisemea hili.

Mwisho niwaombe viongozi wote wawe wa dini au serikali au vyama kujenga utamaduni wa uvumilivu kwa ushauri wa wazi uwe wa kusifia au kukosoa. Huku ndiyo kujenga taifa la uwazi na haki.
 


Baada ya maaskofu kuliamsha dude kuanzia kipindi cha Salam za krismasi na salam za mwaka Mpya, hatimae katibu mwenezi CCM ndugu Humphrey polepole amejitokeza na kuwaomba maaskofu waishauri serikali sirini kwani kwa hali ilivyo sasa ni kama wanaidhalilisha, Rais yuko tayari kupokea ushauri na kuufanyia kazi.

My take
Kila shetani ana mbuyu wake ukimya wa maaskofu na mashehe umetuumiza sana kama taifa na sina shaka wameamuka usingizini baada ya Askofu niwemugizi kuelekezewa bomba la moshi, pia salam zangu za pole ziwafikie Clouds Media

Ni afadhali uishi na joka ndani ya nyumba yako huku ukiwa na dawa ya kuondoa sumu kuliko kuishi na huyu bwana ambaye unajua wazi muda wowote anaotaka anakupeleka kaburini
 
Pamoja na uungwana aliouonyesha polepole lakini bado hawezi kufuta dhambi aliyoifanya Magu. Ili asamehewe anapaswa kutubu mabaya aliyofanya kwa mungu wake na aombe radhi hadharani vinginevyo ataendelea kuipeleka Nchi mahali kusikojulikana huku naye akiwa hajitambui
 
Polepole anazidi kuwagombanisha watu badala ya kuwafanye wawe kitukimoja kupitia itikadi za dini,kwani anasema kwamba kiongozi wa dini akiwa na mwelekeo wa chama Fulani mtu wa chama kingine hawezi kwenda kwake kwa maana ya kwamba wana ccm wawe na maaskofu wao na wana chadema wawe na maaskofu wao kwa maana tu,wote ni wanachama wa chama husika,ameshindwa kuelewa kwamba askofu anaweza kuwa na itikadi ya chama Fulani lakini kwa upande wa dini akawa anawaudumia watu wa vyama vyote,hilo yeye Polepole halioni na kama ameshindwa kuliona hilo vipi ataona ualali wa mwana ccm kumuudumia mwana chadema katika hali ya kawaida? watu wenye mawazo kama ya Polepole hawatufai kabisa katika nchi hii ndio maana sasa hivi inaanza kujitokeza kwamba mwana chadema akipata tatizo kama alivyopata Lisu mwana ccm anashindwa kwenda kumuona na akienda anafikiriwa vibaya, hivyo polepole lazima aonywe mapema kwa huo mtazamo wake
Hivi lile kanisa la pale mikocheni ni la CCM?
 
Back
Top Bottom