Hatimae Polepole awaangukia Maaskofu

Hatimae Polepole awaangukia Maaskofu

Kiburi mwisho wake siku zote ni MAANGAMIZI (destruction).

Akina Polepole wasimsemee huyu bwana, yeye ni mtu mzima na ana uwezo wa kujieleza. Mbona anapofyatua kauli zake chafu chafu na za kibabe hufanya mwenyewe? Kwa nini hili la kutubu amegeuka bubu? Mimi nasema aje hadharani kwa mbwembwe na jeuri ile ile kisha aseme "samahani, nimekosa 1, 2,3......" Na baada ya hapo, aonyeshe kwa vitendo na mwenendo kuwa ni kweli amejuta/ametubu na sasa ataenda kwenye njia za haki.

Kutubu ni maneno na mwenendo, naomba akina Polepole wasubiri kidogo anyooshwe.
 
Niwaombe Maaskofu, Mashehe, Maimamu na Wachungaji wote wasisikilize ombi la bwana Polepole. Ni mtego mbaya maana kwa tabia za serikali yetu ya sasa ilivyo unaweza ukajengewa chuki ya siri, kisha ukapotezwa kwa siri vilevile. Ni heri ushauri wa hadharani ili pindi ikijengwa chuki ya hadharani, mtoa ushauri unaweza ukapata kinga ya umma hadharani.
Tafadhalini mkumbuke kuwa sumu haionjwi kwa ulimi!!!
 
Mkuu swala la ukuta ni la kikatiba na mambo ya kikatiba yanapelekwa mahakamani sio kuandamana.Katiba ibara ya 30 imeweka wazi,kama magufuli afuati katiba hujaambiwa uandamane umeambiwa uende mahakamani.sasa mahakamani hamjaenda mnataka kuandamana kweli?Na ule ukuta ungekula vichwa ving sana
Ni kweli ule ukuta ungekula vichwa vingi sana kwa sababu hata sasa tumeona vichwa vingi vya watanzania vikiliwa na walewale tuliowapa kura tukidhani wako timamu kumbe ni wala vichwa!!!
Hata Viongozi wa dini inadaiwa hawana hadhi ya kukanyaga Magogoni, sasa huo ushauri watautolea wapi, barabarani?!!! Polepole anachekesha sana, eti upitishwe kwake ndipo aupeleke Ikulu!!!!
 
Kwani Pengo huwa nyinyi kina Polepole mnatazama kama nani ? Kadrinali au mwanachama wa Lumumba ?
 
Sijaelewa ishu ya kuungama inaingilianaje na tofauti ya itikadi za kisiasa kati ya muungamaji na mchungaji..
 
SIRINI? Haipendezi, inatakiwa iambiwe hadharani wananchi wajue.Ikiwa sirini mwanachi gani atajua serikali yake imeambiwa kitu na askofu wake? Mambo ya sirini hufanyika sirini
 
Polepole, mchungaji akienda kuombea Mkutano wa Chadema tayari ni Chadema? Kwahiyo Shekh wa Mkoa wa dar es Salaam ni CCM? Pengo ni CCM?

Haya turudi kwa aliyo yasema, nini kakobe katereza, Katiba inaruhusu Vyama kufanya Siasa, kwanini imezuiliwa? watu kupotea na Kupigwa Risasi, hilo nalo ni kawaida kwa CCM? kwahiyo sasahivi wakosoaji dawa yao ni risasi?

Polepole, Ubabe haujawahi kujenga taifa lolote, mmeambiwa kukaa kimya kwa Watanzania msitafsiri Amani, msilewe mpaka Watanzania wakajua mmelewa.
 
Nadhani hata shetani anajifunza kwa sizonje na jopo lake coz mhh
Wakati wa kubana demokrasia haikuwa sirini iweje mtake kukosolewa sirini?
 
Polepole ameongea vizuri japo ni kisiasa!
Yule katibu mkuu wizara ya mambo ya ndani ya nchi inafaa ajitafakari kama kweli anatosha kuendelea kuwepo hapo alipo!
Vitisho na uhuni au tabia za kihuni za kutishia kuzifuta taasisi za kidini aziache kabisa.Yule ni mchumia tumbo akae kimya kabisa.
Ingependeza Rwegasira akawasaidie vijana huko DRC Congo!
 


Baada ya maaskofu kuliamsha dude kuanzia kipindi cha Salam za krismasi na salam za mwaka Mpya, hatimae katibu mwenezi CCM ndugu Humphrey polepole amejitokeza na kuwaomba maaskofu waishauri serikali sirini kwani kwa hali ilivyo sasa ni kama wanaidhalilisha, Rais yuko tayari kupokea ushauri na kuufanyia kazi.

My take
Kila shetani ana mbuyu wake ukimya wa maaskofu na mashehe umetuumiza sana kama taifa na sina shaka wameamuka usingizini baada ya Askofu niwemugizi kuelekezewa bomba la moshi, pia salam zangu za pole ziwafikie Clouds Media

Hivi wale viongozi wa Dini walioomba kukutana na Rais JPM toka mwaka juzi walishajibiwa? Nakumbuka ilikuwa kipindi cha sekeseke la operesheni UKUTA.

Nakumbuka wakati huo JPM alikuwa amepania kweli kweli kumwaga damu ya watanzania wanachama na wapenzi wa CHADEMA. Viongozi wa Dini walijitokeza kutaka kuweka mambo sawa, wakawaomba CHADEMA watulie, na wakaomba kukutana na JPM. Mpaka leo hilo halijafanyika, na ilibidi CHADEMA watumie busara tu kubadili gia ili UKUTA uendelee kwa njia nyingine. na kweli. mpamabano kati ya CHADEMA na serikali ya JPM umeendelea kwa namna mbalimbali na sura mbalimbali.

Imefikia wakati Viongozi wa dini wameona kwamba mambo hayaendi sawa. Alijitokeza Askofu NiweMugizi, akatoa rai yake. Serikali ikagadhabika na kumtisha kwa kumhoji uraia wake. alipoanza kujibu kwa kutumia Zaburi, na kusisitiza msimamo wake, JPM akajifanya yeye msanii, akampigia simu huku akijifanya kwamba wale waliomhoji uraia wamekosea. Thubutu yake! nani anaweza kujaribu kuhoji uraia wa Askofu, tena wa Kanisa Katoliki, ambaye husimikwa kwa uwakilishi wa Serikali Kuu, ni nani anayeweza kuthubutu kumhoji uraia bila taa ya kijani kutoka juu kabisa?

Maaskofu walipozidisha mashambulizi kipindi cha Krismasi, Serikali ikawatisha tena kwa kutishia kufuta makanisa. yule Katibu mkuu wa wizara ya mambo ya ndani alifikia hatua kusema ni marufuku viongozi wa dini hata kusifia Serikali! Naona ikaonekana sasa wale Maaskofu makada wa CCM watafanyaje kazi zao? ikabidi jamaa arekebishe kauli. kusifia ni sawa. kukosoa hapana! Ni uchochezi!!

Ilipokuja nyundo ya Kakobe, Serikali ikakunja ndita. Je, Kakobe afunguliwe mashitaka ya uchochezi? Mmmhhh... hiyo haitalipa in the long run. hebu TRA jaribuni kumdhibiti kwanza. hapo hapo, wakati tunajipanga, hebu wewe Babu Seya njoo kwanza Ikulu unywe Juice na kupiga picha na JPM. hiyo ni kubadili ukurasa ili watu waongelee mengine kwanza.

Ni upuuzi tu. Haiwezekani kukiuka haki za raia wako halafu ukategemea kustawi, ukategemea Amani iwepo. Amani ni tunda la Haki. ni Haki tu ndio itaiokoa Serikali ya JPM kutoka minyukano kama hii. ukandamizaji kama huu wa kuvipiga faini vyombo vya habari, ni mbinu za KIFASHISTI ambazo hazitafualu asilani.

Maaskofu waongee sirini? upuuzi gani huu? na mpaka maaskofu wanaongea, ujue kuna mengi wamevumilia. lakini umefika wakati sasa imetosha. Enough!
DAWA NI KUTUBU!!
 
Hatuwezi kukubali udikteta hata kina Hitler ,Nguema ,Mobutu nk hawakuwakemea viongozi wa dini.
 
Back
Top Bottom