Khaaaa!!Kwahiyo watu wasiwe proud na watoto wao kwasababu tu wanaweza kuharibika?! Kwamba mtu asiwe proud kwasababu kuwa proud hamna maana?!
Kweli tunatofautiana. Utaachaje kuwa proud na kitu unachokipenda?! Mtoto wako mwenyewe uache kusikia fahari jinsi alivyo na afya, jinsi alivyo mjanja, jinsi alivyo na akili, mzuri n.k kisa tu anaweza akaja kuwa mbaya ukubwani?! Unajua hata kitu kinachochangia mtoto kukua vizuri kihisia, kisaikolojia na kiakili ni ufahari anaonyeshwa na wazazi wake?!
Ufahari unaouona online ndo ule ule wa nyumbani na mitaani, tofauti ni kwamba unakuwa shared na wengi. Au hujawahi kukuta mzazi akielezea mtoto wake alivyo hivi au vile, ama watu wakishare ndani ya nyumba vitu vya kijanja na vya akili alivyofanya mtoto wakati mmoja akiwa hayupo. Au hata kwa mawasiliano ya simu kwa waliopo mbali?! It's the same thing sema tu kwa upana zaidi.
Binafsi kama
nyumba kubwa sioni ubaya wowote wa mtu kuwa proud na mtoto wake. Kama wewe una aibu na wakwako jipe all kind of excuses, hata nje usitoke nae ukiogopa kesho akianza kuvuta sigara utajificha wapi.