Hatari ya mafanikio - CHADEMA/UKAWA & Lowassa


Shida iko hapa Watu wa CHADEMA/Lowasa siku zote wanawaza yaliyoikuta KANU ndiyo yataikuta CCM kitu ambacho hakiwezi kutokea kwa maana tuna mazingira tofauti (Kenya na TanZania)!
Hivyo basi kitu pekee ambacho Bw.Lowasa na watu wake wanaweza kufanya ni kutumia fedha nyingi walizo nazo au kwa kifupi kununua washabiki ili wawachague na hapa ndipo tatizo litakapokuja kwa maana ni watu ambao hawasukumwi na sababu za Kiitikadi ideology, imani ya kidini, au kiethnic bali wanasukumwa tu kupewa pesa sasa mtu wa hivi siyo hatari sana na anaweza kukugeuka wakati wowote ule na hapo ndipo Dola ya CCM itakapocheza kwani mfumo wa fedha TanZania uko chini ya Serikali na unaweza kudhibitiwa wakati wowote!

Ngoja nikuulize swali dogo tu kwa mfano Serikali wakisema kesho Bw.Lowasa ana kesi ya kujibu kuhusu Richmond hivyo anatakiwa afike mahakamni Bw.Lowasa atafanya nini? Unafikiri kuna Mtz kutoka Karagwe au Tunduru atakayeingia barabarani kupinga kushitakiwa kwa Lowasa na awe tayari kuumia na kufa hata baada ya kuona wenzake wachache walioumizwa na Polisi?

Kuhusu Marekani, Uchina na Ulaya nilichomaanisha ni kwamba TanZania ni kipenzi cha Wazungu na mpaka sasa hivi hivyo kama Serikali ikimkamata Bw.Lowasa na kumfungulia mashitaka Wazungu au Wachina hawawezi kuingilia swala la escrow Wazungu waligoma kwa sababu fedha zao ndio zilizoibwa na walizitaka lkn siyo kwa sababu ya fedha za Mtz!

Hivyo kwa kifupi Bw.Lowasa hana uwezo wa kuwa Raisi wa JMT nje ya CCM na kama anaamini hivyo atakuwa siyo intelligent man kama mnavyomdhania kwanza hata watu hana kwa maana kama angekuwa nao tungeona maandamano nchi nzima pale tu alipokatwa jina lkn mimi nilikuwepo mitaani hata hao waliokuwa wanamshabika walivyosikia amekatwa wote wakahamia kwa Magufuli na kuendelea kunywa bia!

Sasa hii ni tofauti na Kenya, Raila baada ya Kibaki kutangazwa mshindi tayari Wajaluo wote wakaingia barabarani, sasa ni kwa nini?
Ni sababu ya ethnicity ambayo Bw.Lowasa hana zaidi ya fedha ambazo hata nyingi siyo zake na usifikiri CCM hawajui chanzo cha hizo fedha wanajua na swali ni Je, hawa wanaotoa hizo fedha wako tayari kugombana na Serikali na mfuomo wake wote?
 
 
Kama nia nikushika dola kwa kutumia watu wahalifu,! Mi sidhani kama watanzania wanaweza kukubaliana na wazo Hilo. Namimi sidhani kama tumefika huko

Uhalifu upi? Toa ushahidi hapa jamvini
 
Mi naamini chadema makini haiwezi kumkaribisha Lowasa na timu yake. Itakuwa ni panya walewale kwenye jezi za upinzani.
 
 

Kuna Mfumo uliojengwa ambao unazuia demokrasia kuwepo hapa tz na mifumo hiyo imejengwa na Ccm, siku ccm ikianza kutenda kufanya kazi za siasa, namanisha ikigundua mipaka ya serikali na chama hakika tz itakuwa nchi yenye demokrasia pana. Ningeandika mengi ila device nayotumia ni kikwazo. Naamini hata mtoto wa shule ya msingi anajua tz hakuna demokrasia ila akina sisi tunaonufaika na uwepo wa ccm tutajizigusha hapa na kusifu ujinga wa kila aina.
 
Siasa ya tanzania imekosa mashiko. Hivi ni kweli ukawa wameamua kumpokea lowassa out of nowhere. Pumba tupu.

Mkuu Sabari, siasa si rahisi kama unavyoichukulia, ni ngumu kuliko fizikia, ukiweka bayana msimamo wako na misingi ya msimamo huo tutaweza kujadiliana zaidi,
 

Mkuu Mathias, binafsi naunga mkono Lowasa kwenda ukawa ila bado sishawishiki kuwa agenda yake kuu ni kuwaondolea watanzania umasikini, ukitaka kumwelewa mwanasiasa usisikilize maneno yake, soma matendo yake!
 
Haya nitajie huko kwenye Demokrasia unakokuongelea halafu pia tukueweke kwenye lens kama tulivyoweka demokrasia ya TanZania kwenye lens pia!

Juzi kikwete pale uskandnavia kazuiliwa kuingia ila hapa tz mgombea wa chama anazurura na ndege ya serikali na taasisi zinazosimamia demokrasia zipo kama vile hazijui kinachoendelea halafu mtu hapa unakuja unasifia vitu visivyokuwepo. Ccm ikigundua mipaka ya chama na serikali hakika tz itakuwa nchi yenye demokrasia na tutapiga maendeleo kwa kasi ya ajabu.
 
Kama nia nikushika dola kwa kutumia watu wahalifu,! Mi sidhani kama watanzania wanaweza kukubaliana na wazo Hilo. Namimi sidhani kama tumefika huko

Mkuu Bob G, nia si kushika dola, lengo la kwanza linatakiwa liwe kuiondoa CCM, kama alivyosema mchangiaji mmoja hapo nyuma katika hili tuwe tayari kwenda mbali. Lowasa ni mbaya lakini hawezi kuwa mbaya kwa maendeleo ya nchi hii kuliko CCM, lazima tumchague shetani mmoja ili kufanikiwa na shetani mwenye afadhali hapa ni Lowasa.
 
Ilikuwa rahisi zaidi Lowassa kupitishwa na CCM kuwa mgombea kuliko kushinda urais akiwa UKAWA.
Sipendi kuamini kuwa CDM waliomtuhumu Lowassa na CCM yake leo hii watamuona Lowassa anafaa kugombea hadi ujumbe wa nyumba kumi.
Katika siasa lolote laweza kutokea lakini CDM haiwezi kumpokea Lowassa na kubaki salama.
Hivi wanahitaji zile "mbinu " za Lowassa akiwa CCM ili washinde?
Watakuwa tofauti gani na ufisadi wanao piga vita?
 
Mkuu umeokwa povu sana, ushauri wa bure tu dont take politics serious utakufa na kihoro wenzio wanacheka pembeni
 


Very interesting analysis....dah safi sana..nimekuelewa!!
 
Mkuu umechambua vizuri sana na umeeleweka vema.
Big up sana.
 
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...ya-mafanikio-chadema-ukawa-and-lowassa-5.html

Mkuu Frederick Barbarosa, nakubaliana na wewe kuwa wafuasi wa Lowasa si wengi kama anavyotaka tuamini na hilo nimelielezea kwenye andiko langu. Pia na kubaliana na wewe kuwa wengi wao ni opportunists hawaunganishwi na Ideology yoyote wala dini waka kabila, of course wanaunganishwa na maslahi binafsi na ndio maana wengi hawatatoka CCM kumfuata lakini kwa vile ni opportunist watakuwa tayari kuihujumu CCM toka ndani wakiamini kuwa akipita malengo yao binafsi yatafanikiwa. Walioko kwenye dola ni hivyo hivyo, hawataacha ajira zao kumfuata lakini watafanya hujuma wakiwa huko huko ndani ila tu watafanya kwa namna ambayo hawatataka kujulikana. Jua jambo moja, watu hawa wanaamini Lowasa akiwa raisi hata kupitia UKAWA maslahi yao yatalindwa vizuri zaidi kuliko CCM ikishida kupitia Magufuli.

Swala la Lowasa kushitakiwa kuhusiana na kashfa ya Richmond baada ya kutoka CCM halitatokea, wanaojua siasa wanafahamu fika kuwa hiyo itakuwa ni CCM kujipiga risasi mguuni alafu ikataka kushiriki marathoni. Kikwete anajua siasa hawezi kufanya such a wrong political move.
 

Lowasa ikitokea serikali hii ya ccm ikamchukulia hatua akiwa nje ya ccm ndiyo hapo wananchi tutakapojua kuwa ndani ya ccm kuna wezi wengu tu ila hawachukuliwi hatua sababu wako ccm. Na ukweli ndiyo utathibitika kuwa serikali ya ccm inawalinda wezi badala ya kuwachukulia hatua kisa tu wako ccm. Mimi naisubiri sana hiyo ya serikali kumchukulia hatua Lowasa kama atahamia upinzani ndipo nitajua kuwa serikali hii ya wezi na mfumo ndiyo unawalinda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…