HATARI : Watu 3 mbaroni kwa kuwabeba watoto wanafunzi 34 kwenye gari aina ya NOAH

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262




a7b8e1f35eb6f27a2ac20169a5843782.jpg


Gari aina ya NOAH limekamatwa likiwa limebeba watoto wanafunzi 34 wa shule pamoja na mwalimu wao jumla 35.

31d8aed9863ffb9e8db6cb513ca65bff.jpg


Wanafunzi hao ni wa darasa la pili kutoka shule ya Diamond, Olimpio, Kisutu Maktaba na Bunge gari hiyo imekamatiwa eneo la round about Gerezani wakielekea Vijibweni Kigamboni.

Dereva na wahusika wa gari hilo wanashikiliwa na jeshi polisi kwa mahojiano zaidi.
 
Ni 36 plus driver. Hakika nothing is impossible. Noah ya watu 11 kubeba watu wote hao
 
Watu bhana hiv hata Noah kumbe inabeba watu siyo nilifikiri ni ya kubebea karatasi bhana.
 
Walikaa kama mapera?

Huruma yake iilipitiliza kiwango, hii yote ni kwaajili ya kuwasaidia wawahi shule na kuepukana na manyanyaso ya makondakta au ambao hawana nauli kabisa.

Apewe tu onyo na angalizo maana sidhani kama aliwalipisha.
 
hao watoto hawawez kupandishwa humo bila wazaz wao kukubaliana na huyo dereva so wazaz nao wanahusika juu ya hilo.
ndio matatzo ya kukimbia school bus kisa gharama
 
Hao wazazi wa wanafunzi huwa hawajui watoto wao wapo kwenye hatari na labfa ndio zile za kuchajiwa pesa ndogo na kufurahia mfano ya bia itapatiana pia.

Hili jambo ni aibu kwa wazazi wengi wa Tanzania wasiofuatilia ya watoto wao.
 
Nna noah ila kun kuna siku nlienda mlalo kwa utalii huko lushoto ,nilichoona noa kila kitu inawezeka.
 
image.jpeg
image.jpeg
[HASHTAG]#Habari: Poli[/HASHTAG]
si inawashikilia watu 3 kwa kosa la kuwabeba watoto wanafunzi zaidi ya 34 kwenye gari moja aina ya NOAH jijini DSM jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa watoto hao.
 
Walikaa kama mapera?

Huruma yake iilipitiliza kiwango, hii yote ni kwaajili ya kuwasaidia wawahi shule na kuepukana na manyanyaso ya makondakta au ambao hawana nauli kabisa.

Apewe tu onyo na angalizo maana sidhani kama aliwalipisha.
Nope..huyu ana tenda ya kubeba wanafunzi yani km school bus..
Wanajitetea eti wana noah mbili moja iliharibika /sijui kukamatwa so wakalazimika kuwabeba wanafunzi wao wotebkwa gari moja...unfair
 
Back
Top Bottom