Hataki nimpe lifti mdogo wake

Hataki nimpe lifti mdogo wake

navin dippe

Member
Joined
May 18, 2015
Posts
47
Reaction score
104
Wana Jf habari za blue monday,

Kuna rafiki wa wife amehamishiwa hapa Dar kikazi, amefikia kwetu wakati akitafuta pa kuishi wamekubaliana na wife akae hapa kwetu mwezi. Ana wiki moja tangu ameripoti kazini kwake, hiyo wiki yote ni mimi ndo nimekua nikiondoka nae asubuhi kwenda kazini maana ofisi zetu wote zipo mjini, tangu Ijumaa wife amenishangaza kunizuia kumbeba huyu mgeni wetu kwenda kazini anataka nimpitishe kwenye dala dala. Sasa mimi niliemtuma akubali kumpokea?

Hivi nitaanzaje kumkatalia lifti wakati nimembeba wiki nzima? Nimepewa ultimatum kwamba tukirudi wote jioni nitaona,
sasa hii wakuu si kutafuta ugomvi bure? Siku zote anadai hawezi kuleta marafiki zake wazuri nyumbani labda wa kuja na kuondoka sasa imekuaje huyu kampokea? Na kwa kweli huyu mtoto kaumbika haswa!

Yaani ni mzuri ajabu, nyonyo kama embe bolibo ananukia marashi wakati wote, yaani kwenye gari hata akishuka harufu ya manukato inabaki kutwa nzima Juzi tumerudi home wife ananivaa chumbani kwamba tumetoka wapi anauliza mbona nakua marashi ya yule dada kumbe wapi hatujafanya chochote, tunaheshimiana mno, anajiheshimu sana huyu binti, ananiamkia asubuhi jioni, tena kwa magoti.

Yaani anaemmiliki huyu binti anafaidi kweli. Wakuu nimuhakikishieje wife kwamba hakuna madhara yoyote yanayoweza kutokea anielewe? Tunabishana usiku chumbani hadi nahisi yule dada anaweza kutusikia. Wakuu kuna mwenye suluhisho hapa nifanyeje? Ananihisi vibaya kumbe mimi sina wazo hilo, nilikua na mchepuko mke wa rafiki yangu alieachishwa kazi ila nimetubu na kuachana nao kutokana na kushindwa gharama za uendeshaji.
 
Tehe wanawake hawajiamini kabisa. Mie kuna shemeji yangu hata kuongea nae sentesi mbili siwezi. Nikizidisha tu wife atanuna siku nzima. Akiwepo usiku funguo za room zinafichwa. Nikishtuka tu na yeye anashtuka yaani we acha tu
 
(Anajiheshimu sana huyu binti, ananiamkia asubuhi jioni, tena kwa magoti)
Mimi mpangaji wangu amehama juzi kuna upande mzima wa nyumba kwa nia dhati kabisa usiaribu ndoa yako mimi nimeamua kujitolea nimpangishe tena miezi miwili free of charge,
Nimemiss sana kuamkiwa usiku na mchana..
 
Inaonekana huyo mwanamke ni chupi mkononi na wewe ni chupi mkononi
ili kusolve tatizo ni kuwatenganisha
 
navin dippe

Naomba nikusaidie kumpeleka na kumrudisha kazini!
 
Last edited by a moderator:
Tehe wanawake hawajiamini kabisa. Mie kuna shemeji yangu hata kuongea nae sentesi mbili siwezi. Nikizidisha tu wife atanuna siku nzima. Akiwepo usiku funguo za room zinafichwa. Nikishtuka tu na yeye anashtuka yaani we acha tu

Mkuu umepigwa pin ile iiii hatari
 
Kwanini mtu uishi kwa mtu tena una kazi? Si bora ukae hotel hadi upate hiyo nyumba.
Pia watu wajipange kabla hawajaenda sehemu
 
Ndoa ni tamu lakini mahusiano na jamii ni MUHIMU, cha msingi badili muda wa kwenda au kutoka kazini, kama ulikuwa unawahi Anza kuchelewa kama ulikuwa unachelewa Anza kuwahi na utengeneze interval naya mgeni
 
Haya bwana navin dippe.....

Naona ni mwendo wa kutunywesha chai tu

Anyway,

Acha nipite hivi ============= > > >



Wana jf habari za blue monday
Kuna rafiki wa wife amehamishiwa hapa dar kikazi, amefikia kwetu wakati akitafuta pa kuishi wamekubaliana na wife akae hapa kwetu mwezi

Ana wiki moja tangu ameripoti kazini kwake, hiyo wiki yote ni mm ndo nimekua nikiondoka nae asubuhi kwenda kazini maana ofisi zetu wote zipo mjini,

Tangu ijumaa wife amenishangaza kunizuia kumbeba huyu mgeni wetu kwenda kazini anataka nimpitishe kwenye dala dala
Sasa mm niliemtuma akubali kumpokea?

Hivi ntaanzaje kumkatalia lifti wakati nimembeba wiki nzima?
Nimepewa ultimatum kwamba tukirudi wote jioni ntaona
Sasa hii wakuu si kutafuta ugomvi bure?

Siku zote anadai hawezi kuleta marafiki zake wazuri nyumbani labda wa kuja na kuondoka sasa imekuaje huyu kampokea?
Na kwa kweli huyu mtoto kaumbika haswa!! Yaani ni mzuuuri ajabu, nyonyo kama embe bolibo ananukia marashi wakati wote, yaani kwenye gari hata akishuka harufu ya manukato inabaki kutwa nzima

Juzi tumerudi home wife ananivaa chumbani kwamba tumetoka wapi anauliza mbona nakua marashi ya yule dada kumbe wapi hatujafanya chochote, tunaheshimiana mno, anajiheshimu sana huyu binti, ananiamkia asubuhi jioni, tena kwa magoti

Yaani anaemmiliki huyu binti anafaidi kweli

Wakuu nimuhakikishieje wife kwamba hakuna madhara yoyote yanayoweza kutokea anielewe?

Tunabishana usiku chumbani hadi nahisi yule dada anaweza kutusikia

Wakuu kuna mwenye suluhisho hapa nifanyeje?
Ananihisi vibaya kumbe mm sina wazo hilo, nilikua na mchepuko mke wa rafiki yangu alieachishwa kazi ila nimetubu na kuachana nao kutokana na kushindwa gharama za uendeshaji

Wakuu amani iwe kwenu,

Mimi ni afisa utumishi kwenye kampuni moja hivi hapa Dar es salaam. Hivi karibuni bodi ilitengeneza nafasi 12 mpya za kazi na kuzitangaza.Viongozi waligawana nafasi nafasi tatu kila mmoja na mimi kuniachia 3.

Huwa inakua hivyo kila tunapoajiri, katika hizo nafasi tatu nilizopewa nilipanga moja nimpe wife ambae amemaliza chuo mwaka Jana, nyingine ni mshikaji wangu ambae aliniandalia pesa na ya mwisho nimpe rafiki wa wife ambae wife
mwenyewe aliniomba. Mimi na wife tulioana akiwa na elimu ya form six hakuweza kuendelea kuna matatizo yalijitokeza, hivyo baada ya kumuoa ndipo nikampeleka chuo baada ya kukaa miaka 3 nyumbani.

Mwaka jana ndio amemaliza, so hivi juzi tukamwita kwa mtihani pamoja na wenzie kama 100 hivi tuliowachuja matokeo yalipotoka akawa amepata 2 ya 50 mi naita sifuri maana nilimuongezea mimi hizo mbili wakati nasahihisha.Bosi wangu akasema niamue nwenywe kama namchukua na matokeo hayo siku wakija auditors jumba bovu litaniangukia ni vyema nikasubiri nafasi zingine. Hivyo wale wengine 11 akiwemo na Rafiki yake wakaitwa kwa kazi

Sasa ndani kuna ugomvi kati yangu na mke wangu anasema ningemchykua hivyo hivyo hata kama kafeli. Nimemwelewesha hataki kuelewa kaninunia wiki sasa, hatuongeleshani tunaamka kama mabubu.Usiku saa ya kulala anavaa suruali za tight mbili na jeans juu na mkanda ndo analala tena kwenye kona ya kitanda.Nikimgusa ni ugomvi anasema ninatembea na rafiki yake niliempa kazi, nikimwelewesha kuwa yule alifaulu mtihani anadai tunamsaliti nyumba haina amani sasa.

Wadau najiuliza maswali kadhaa;
(1) Inakuaje graduate akapata 2 ya 50 kwa maswali ambayo wote tuliyasoma sekondari?
Mengine ya primary school?

(2) Inakuaje mtu anashindwa hesabu za ratio, kuandaa balance sheet, statement of ACC wakati chuo amepita mitihani na Ku graduate au ndo zile degree za chupi? Nalazimika kuwaza hivyo maana hainiingii akilini

Nikijaribu kumuuliza haya maswali anakua mkali anasema hataki maongezi. Kwa kweli nimechoka juzi nilikua naongea na rafiki yake kuhusu huu mgogoro kwa kweli alinifariji vizuri hadi nikafikria kuwa ni bora niwepo nae tu ukichukulia kuwa kwa sasa sipati conjugal rights .

Naomba mwongozo wenu

NB:
Tuna watoto wawili

Kuna rafiki yangu ambae tulikua tumeshibana sana miaka kadhaa iliyopita lakini bahati mbaya urafiki wetu ulitumbukia nyongo na tumechuniana zaidi ya miaka minne Kwa sababu ambazo sijazielewa hadi leo, jamaa alikataza hadi mkewe kujihusisha na familia yangu kumbe jamaa hana kazi mwaka wa nne sasa yupo benchi alifukuzwa kazi.

Kama miezi miwili iliyopita nilikutana na mkewe accidentally, tukapeana contact upya na alikua mjamzito lilinishangaza sana maana kwa maisha yao yalivyokua mazuri haikua rahisi kuamini. Baada ya kumpa kama laki na hamsini hivi jumla nikaanza kumkwepa, haikusaidia akawa ananipigia kwa namba zingine, siku moja akaniomba tuonane katika kuonana akanieleza kwa urefu sana matatizo yao ifuatavyo.

Moja ni kuwa mumewe hajishugulishi na chochote amekaa tu home tangu afukuzwe kazi miaka minne iliyopita.Pili anategemea wazazi ndo wamtumie hela mara kwa mara. Tatu hata ikitokea mtu ameumwa ndani inabidi waombe ombe pesa kwa watu mbali mbali. Nne, anadai hali ni mbaya kuzidi maelezo amekua akimsisitiza aje anione ili nimsaidie maana nipo HR department na jamaa anajua hilo lakini mwanamke akimgusia jambo hilo jamaa ananzisha hadi ugomvi mkubwa hivyo amemuacha tu. Ukistaajabu ya musa utayaona ya firauni wiki kama tatu zilizopita aliniomba tuonane Kinondoni Machi Machi guest house nikashtuka sana, nikamuuliza kulikoni guest akaniambia wewe njoo hapo tukionana bar huwezi jua nani atatuona so tuongee kwa dakika chache then naondoka

Nilipofika alikua jirani na hapo akaja tukaingia ndani, kwa hali ya ujauzito alionao niliamini wazi hatuwezi kufanya chochote, surprisingly alianza kunivua nguo kama wale watu wa wrestling, nilijikuta nimeshindwa kuhimili mhemko na bahati mbaya tukajuana. Sikujua kama jamaa ameoa mwanamke mpenda pesa kiasi kile maana pale pale akaniomba laki moja nikampa elfu hamsini cha ajabu jioni akaanza kunisumbua hamsini iliyobaki.

Nimejiingiza kwenye jambo ambalo limekua mzigo mkubwa kwangu, natoa hela kila siku mbili tatu. Ingawa akiniomba twende guest nakua mdhaifu nashindwa kukataa, kwa kawaida mke wangu akiwa mjamzito huwa hapendi tendo kabisa na style yetu huwa ni moja tu miezi yote ya wote kutazama upande mmoja, ila huyu shemeji huwezi amini mtu ana mimba ya miezi saba kwenda nane anajibinua anakaa doggie hadi mi naogopa.

Nahitaji kuachana nae lakini amekua all over me, anasema anakaribia kipindi cha kujifungua hivyo anahitaji msaada wangu, anaona kuwa tukiachana siwezi kumsaidia kama tulivyo wapenzi. Hivi sasa ananisumbua ada ya mtoto wao wa kwanza ambae kafunga shule, na mimi sina hiyo hela kwa kweli maana mimi binafsi nina watoto watatu, mmoja nilizaa kabla sijaoa hivyo namhudumia mimi. Hili jambo linanishinda kwenye gharama tu.

Kuna mwenye suluhisho hapa nilitatue vipi hili tatizo?




Wakuu,

Kuna binti nilizaa nae mtoto miaka kadhaa iliyopita kabla sijaoa kwa bahati mbaya uhusiano huo haukuweza ku materialise kufikia ndoa nikawa nimeoa mwanamke mwingine yeye hajaolewa hadi sasa nimempangia upande wa nyumba anaishi hapo na mtoto wetu. Tumekua tukisumbuana sana na huyu binti kuhusu matunzo ya mtoto kwa muda mrefu amekua na matumizi mabaya ya pesa nikimpa hela leo siku mbili mbele anaomba tena wakati mtoto anakula shuleni milo miwili jioni ndo anakula nyumbani yeye nimempa mtaji mara kadhaa afanye biashara mtakuja unakatika.

Juzi nimeenda kumuona mtoto nashangaa kulikuta jitu lake hapo, lililala hapo kwenye nyumba ninayoilipia mm na linakula hapo hapo chakula changu, gaya niliambiwa na house girl ninaemlipa mimi mshahara, hii ni kama familia yangu ya pili ninaigharamia kila kitu sasa wakuu hili jamaa lina haki gani ya kuja kula na kulala hapo?

Nikimuuliza mzazi mwenzangu huyo jamaa haishi hapo huwa anakataa anasema anakuja na kuondoka ila mi nina uhakika analalaga hapo Juzi binti kanisumbua wameishiwa hela nikadhani wana emergency nikawatumia laki mbili cha kushangaza usiku wa tatu nikapita pale nikamkuta housegirl na mtoto tu, kumuuliza kulikoni mbona mpo peke yenu akanijibu mama na jitu lake wameenda FM academia iliyokua imekuja kutumbuiza bar ya hapo mtaani.

Ndipo nikagundua laki mbili yangu ndio inayotumika huko maana jitu lake halina kazi na yeye hana kazi.Nikamfuata huko bar nikamtumia sms akatoka nje nilipomuhoji alikua amechangamka na bia akaniporomoshea Maneno makali kwamba namfuatilia sana, kwamba nisimtishe na hicho ki laki mbili nikamuacha nikaondoka zangu.

Tangu siku hiyo nimekata mawasiliano anapiga simu asubuhi hadi jioni sipokei, anatuma sms za kuomba msamaha sizijibu maana nimeshachoka nae sasa wakuu nimekosea kwa uamuzi huu? Pia nauliza nitumie utaratibu gani kuendelea mbele ya safari? Maana nimetaka kumchukua mtoto mara kadhaa lakini mama yake hataki anataka kukaa nae
mke wangu pia huonyesha kukereka ninapomzumzia huyo mtoto hivyo nikapata picha hapendi aje kuishi na sisi.

Nasikitika kulikuta jitu kwenye nyumba niliyonunua, kwenye makochi niliyonunua, kwenye TV niliyonunua mimi limeweka nne likiwa na remote mkononi bila hata aibu halafu halinisalimii. Nitakuja kulitimua humo siku moja.

Msaada wenu please, nishaurini nifanyeje wadau
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom