Hata wamachinga sasa wanasifia usafi wa mitaa

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,293
12,593
Kwa mara ya kwanza leo nimemsikia kwa masikio yangu mfanyabiashara aliyeondolewa kando ya barabara akisifia usafi ulioaza kujitokeza kandokando ya barabara zetu.

Nilikuwa na rafiki yangu aliyekuwa anauza matikiti ya kukata vipande pale Banana Ukonga jirani na taasisi ya Hali ya Hewa akisifia sana namna sehemu hiyo inavyoonekana sasa baada ya wauza miwa, mananasi na matikiti kufurushwa na Mh. Mkala. "Ni ubishi wetu tu lakini kweli tulikuwa tunayachafua mazingira", alisikika ex mmachinga akisema. nikamuuliza sasa uko wapi na unafanya nini, akasema amerudia kazi yake ya udereva maana leseni ya udereva anayo lakini aliitia mfukoni afanye umachinga.

Nina uhakika kuwa kosa lilikuwa ni serikali kuacha kuwaambia vijana mapema kuwa hapo hapana kwa biashara, sio vijana. Na hata leo vijana wako tayari kuondoka kama watapewa muda wa kumalizia bidhaa zao walizonazo mikononi. Hata wao wanafahamu kuwa walipo sipo ila walikuwa wakisikilizia tu, hatimaye wakajenga mazoea na kuvutia wengine.

Mitaa ikiwa safu CCM isiwe na mashaka 2025.
 
Kututoa barabarani msijione mmeshinda! Tunawavutia kasi tu mtaanz kutuon x-mas senzi kabisa nyinyi
Hapa wewe kizuri unakifahamu na unakitaka. Yaani eti utoke huko kwenu Lupaso na ushamba wako uje uchafue mitaa ya posta picha ya askari watu wakuache eti unatafuta riziki. Kwani sisi tuliozaliwa hapa mjini hatukupaona? Hatuna shida? Kany.. ulale
 
Hakika mji wa DSM umebadilika sana. Angalau mji unaonekana kama Kigali

Dar es salaam sio sehemu wanazopita watalii tu huko mitaa ya Samora na Posta mpya!!! Dar e s salaam ni mitaa hiyo ya Samora pamoja na vitongoji vyake ambavyo mpaka sasa wamachinga wamezagaa na uchafu uko pelepale kama kabla ya zoezi!! Makalla anaogopa kuwatoa wamachinga kwenye viwanja vya wakubwa; akisikia hapa ni kwa Kawawa au Nyerere hapagusi Ingawa Wakazi wa sehemu hizo wanakiuka sheria!!! Huwezi kufanikisha hili zoezi kama mtakuwa na double standards!!! Sheria lazima ziwe kama msumeno kwa kukata kotekote.
 
Sehemu nyingi hawakuondoka, bado wapo palepale. Sehemu kadhaa wanaondoka mchana wanarudi usiku kuweka kambi
 
sehemu nyingi hawakuondoka, bado wapo palepale
sehemu kadhaa wanaondoka mchana wanarudi usiku kuweka kambi
AAA ni sawa, hata nyoka ukimkata kichwa ataendelea kutembea, lakini ni kwa muda tu. Hata machinga unaowaona wapo, hilo ndio teke lao la mwisho.
 
At least hivyo aisee , wanapanga chini , kuliko ule uchafu wa vibanda uliokuwepo barabarani
Kuna haja ya kushuhulika na wanunuzi wanaonunua bidhaa zilizopangwa chini kwenye mavumbi, tope na inzi. utakuta watu wananunua na kula vyakula vinavyouzwa sehemu zenye mavumbi, inzi zisizokuwa na maji tiririka ya kuonyeshea vyombo, matunda na mikono kabla na baada ya kunywa. Maji yaleyale kwenye beseni yanatumika kuoshea vyombo vya wateja wote wanaomaliza na wanaotaka kula.

wakati tunashuhulika na wauzaji tushuhulike na wanunuzi pia wanaonunua mboga, viazi, mihogo, bamia, nk zilizopangwa chini.
 
Kwa mara ya kwanza leo nimemsikia kwa masikio yangu mfanyabiashara aliyeondolewa kando ya barabara akisifia usafi ulioaza kujitokeza kandokando ya barabara zetu.

Nilikuwa na rafiki yangu aliyekuwa anauza matikiti ya kukata vipande pale Banana Ukonga jirani na taasisi ya Hali ya Hewa akisifia sana namna sehemu
Naona palizi imeanza
 
Dar es salaam sio sehemu wanazopita watalii tu huko mitaa ya Samora na Posta mpya!!! Dar e s salaam ni mitaa hiyo ya Samora pamoja na vitongoji vyake ambavyo mpaka sasa wamachinga wamezagaa na uchafu uko pelepale kama kabla ya zoezi!! Makalla anaogopa kuwatoa wamachinga kwenye viwanja vya wakubwa; akisikia hapa ni kwa Kawawa au Nyerere hapagusi Ingawa Wakazi wa sehemu hizo wanakiuka sheria!!! Huwezi kufanikisha hili zoezi kama mtakuwa na double standards!!! Sheria lazima ziwe kama msumeno kwa kukata kotekote.
Umenena vyema,
Ni i uonevu tu
Mfano hapo misheni kota kariakoo pamejaa malori
Hadi barabara hazionekani yaani ni heri ya wamachinga kuliko malorikwa kweli baadooo sanaaa kariakoo mitaa ya narun'gombe, na ndanda na muheza pameoza hapafai
Hembu wahusika wapite hata leo waone vile pameoza
Machinga wameonewa tu
 
Back
Top Bottom