DOKEZO Dar: Viongozi wana mpango gani na usafi wa mazingira? Maeneo mengi ni machafu, hakuna mkakati wa wazi unaotekelezwa

DOKEZO Dar: Viongozi wana mpango gani na usafi wa mazingira? Maeneo mengi ni machafu, hakuna mkakati wa wazi unaotekelezwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
498
Reaction score
785
Dar es Salaam, kama jiji kubwa na kitovu cha uchumi wa nchi, linapaswa kuwa mfano bora wa usafi na upangaji wa mazingira. Hata hivyo, hali halisi inayoonekana mitaani inazua maswali mengi kuhusu uwajibikaji wa viongozi na utekelezaji wa majukumu yao.
IMG-20260506-WA0022.jpg

Katika maeneo kama Makumbusho, Kijitonyama, Sinza na Kawe, Mikocheni ni jambo la kawaida kukutana na mitaro iliyojaa taka, maji machafu yaliyotuama na harufu isiyovumilika. Hali ni hiyo hiyo pia katika maeneo ya Posta na Kariakoo, ambayo ndiyo sura ya jiji kwa wageni wengi sio ajabu kuona maji taka ya chemba na uchafu vikizagaa kwenye maeneo hayo.

Kinachotia wasiwasi zaidi ni kwamba taka zimezagaa katika mitaa mingi bila kuwa na miundombinu ya kutosha ya ukusanyaji na utupaji inayolingana na kasi ya ukuaji wa jiji. Jiji linaendelea kupanuka kwa kasi, lakini mifumo ya usafi wa mazingira inaonekana kubaki nyuma. Hili linaibua swali la msingi: je, mipango ya usafi ipo kweli, au ipo kwenye makaratasi tu?
IMG-20260506-WA0004.jpg

Mbali na taka, pia kuna tatizo la maeneo mengi kuto fyekwa. Kuanzia Temeke maeneo ya ambayo yapo penbezoni mwa barabara, Mbezi Beach, Kimara na meneo mengine majani marefu yamekuwa sehemu ya mandhari ya kawaida. Hali hii si tu inapunguza hadhi ya jiji, bali pia inachangia kuongezeka kwa mazalia ya mbu na hatari za kiafya kwa wakazi. Usafi wa mazingira si suala la mandhari tu, bali ni suala la afya ya umma na ustawi wa jamii.
IMG-20260506-WA0018.jpg

Wengi wanakumbuka kipindi cha uongozi wa hayati Rais Dkt. John Magufuli, ambapo kulikuwa na msisitizo mkubwa wa usafi wa mazingira. Ingawa kulikuwa na changamoto zake, mpango ule ulikuwa na mwelekeo, ulikuwa shirikishi, na ulihamasisha uwajibikaji kuanzia ngazi ya mtu mmoja mmoja hadi taasisi. Leo hii, juhudi kama hizo zinaonekana kufifia, na pengo hilo linaonekana wazi mitaani.

Swali la kujiuliza ni hili: licha ya kuwepo kwa viongozi na wataalamu wa mazingira katika kila wilaya, kwanini bado hatuoni ubunifu wa wazi na hatua madhubuti za kuboresha hali ya usafi? Je, tatizo ni ukosefu wa rasilimali, usimamizi dhaifu, au kutopewa kipaumbele kwa suala hili?
IMG-20260506-WA0010.jpg

Ni wakati sasa kwa viongozi kuwajibika na kuweka mikakati inayoonekana na kupimika. Wananchi pia wana wajibu wa kushiriki, lakini uongozi thabiti na mifumo madhubuti ni msingi wa mabadiliko. Bila hatua za makusudi, Dar es Salaam itaendelea kupoteza hadhi yake na kuhatarisha afya za wakazi wake.
IMG-20260506-WA0019.jpg
 
Suma ndio wamechukua tender nzima ya usafi hapo wa kumwambia sijui ni nani!
 
Usafi ni jambo la asili sana hakihitaji elimu ya darasani.. Kama kiongozi ni mchafu by nature hata mazingira yake hayawezi kuwa safi
 
Viongozi wetu wamekuwa wanyama sana, hawajuhi kwamba uchafu kama huo unasababisha seriikali inaingia gharama ya matibabu sababu watu wanaugua magonjwa mengi. Nenda mitaa ya kunduchi utaona watu wavyotirisha maji taka mtaani. Mfano soko la samaki la kunduchi ni chafu hata sijuhi serikali inakuwa inafanya nini. Pia maeneo ya kunduchi lilipo hilo soko, zile nyumba za watu waliovamia wakajenga pwani sijajua ni kwa nini wasiondolewe. Hayo ni maeneo prime kama hayo yaanachwa watu wanajenga ovyo ovyo panaonekana ovyo tu.
 
Dar es Salaam, kama jiji kubwa na kitovu cha uchumi wa nchi, linapaswa kuwa mfano bora wa usafi na upangaji wa mazingira. Hata hivyo, hali halisi inayoonekana mitaani inazua maswali mengi kuhusu uwajibikaji wa viongozi na utekelezaji wa majukumu yao.
View attachment 3584508
Katika maeneo kama Makumbusho, Kijitonyama, Sinza na Kawe, Mikocheni ni jambo la kawaida kukutana na mitaro iliyojaa taka, maji machafu yaliyotuama na harufu isiyovumilika. Hali ni hiyo hiyo pia katika maeneo ya Posta na Kariakoo, ambayo ndiyo sura ya jiji kwa wageni wengi sio ajabu kuona maji taka ya chemba na uchafu vikizagaa kwenye maeneo hayo.

Kinachotia wasiwasi zaidi ni kwamba taka zimezagaa katika mitaa mingi bila kuwa na miundombinu ya kutosha ya ukusanyaji na utupaji inayolingana na kasi ya ukuaji wa jiji. Jiji linaendelea kupanuka kwa kasi, lakini mifumo ya usafi wa mazingira inaonekana kubaki nyuma. Hili linaibua swali la msingi: je, mipango ya usafi ipo kweli, au ipo kwenye makaratasi tu?
View attachment 3584510
Mbali na taka, pia kuna tatizo la maeneo mengi kuto fyekwa. Kuanzia Temeke maeneo ya ambayo yapo penbezoni mwa barabara, Mbezi Beach, Kimara na meneo mengine majani marefu yamekuwa sehemu ya mandhari ya kawaida. Hali hii si tu inapunguza hadhi ya jiji, bali pia inachangia kuongezeka kwa mazalia ya mbu na hatari za kiafya kwa wakazi. Usafi wa mazingira si suala la mandhari tu, bali ni suala la afya ya umma na ustawi wa jamii.
View attachment 3584511
Wengi wanakumbuka kipindi cha uongozi wa hayati Rais Dkt. John Magufuli, ambapo kulikuwa na msisitizo mkubwa wa usafi wa mazingira. Ingawa kulikuwa na changamoto zake, mpango ule ulikuwa na mwelekeo, ulikuwa shirikishi, na ulihamasisha uwajibikaji kuanzia ngazi ya mtu mmoja mmoja hadi taasisi. Leo hii, juhudi kama hizo zinaonekana kufifia, na pengo hilo linaonekana wazi mitaani.

Swali la kujiuliza ni hili: licha ya kuwepo kwa viongozi na wataalamu wa mazingira katika kila wilaya, kwanini bado hatuoni ubunifu wa wazi na hatua madhubuti za kuboresha hali ya usafi? Je, tatizo ni ukosefu wa rasilimali, usimamizi dhaifu, au kutopewa kipaumbele kwa suala hili?
View attachment 3584514
Ni wakati sasa kwa viongozi kuwajibika na kuweka mikakati inayoonekana na kupimika. Wananchi pia wana wajibu wa kushiriki, lakini uongozi thabiti na mifumo madhubuti ni msingi wa mabadiliko. Bila hatua za makusudi, Dar es Salaam itaendelea kupoteza hadhi yake na kuhatarisha afya za wakazi wake.
View attachment 3584515
Mhii yaani wewe naona ni mgeni hapa mjini au.nchi ya Malawi
 
Ukitaka kujua ustaarabu wa jamii fulani kwanza angalia mazingira wanayoishi hapo utapata picha zima ya hiyo jamii.
 
Hakika Dar ni chafu mno, mitaa ya Kariakoo imefurika maji taka yanayotililika ovyo.

Mtaa wa Lindi, kuanzia Livingstone mpaka Shaurimoyo ni mchafu mno.
Cha kushangaza kwenye eneo hilo kuna kituo cha daladala kinachohudumia zaidi ya watu alfu 30,000 kwa siku.

Eneo hilo lina maji taka yasiyokauka muda wote wa mwaka, lakini kuna msongamano mkubwa wa watu na biashara ya vyakula inafanyika mahali hapo kwa amani.

Kipindupindu kikivamia jiji zima litakumbwa na vilio.
 
Ni wakati sasa, Jiji ama Halmashauri kuajiri kampuni binafsi kushughulikia taka/usafi

Ikionekana mtu unafanya biashara na eneo lako likawa chafu, mwenye hiyo biashara awe anawajibishwa

Kingine Watanzania tujifunze ustaarabu, Watanzani wengi hatuna ustaarabu kwenye mambo ya usafi/mazingira

Ukitaka kujua hilo, supermarket kama Mlimani city, hadi wameajiri watu mule vyooni kwaajili ya kufanya usafi mara baada ya mtu kumaliza kupata haja

Hii ina maanisha kwamba kuna wenzetu wanaweza kwenda kupata haja, wakasahau hata kuflush choo chake, ama akashindwa hata kulenga shimo la choo 🙌

Wale ambao tumebahatika kusafiri nje ya Nchi, tutakuwa tumeona utofauti wa sisi Wabongo na jamii nyingine
 
Back
Top Bottom