Odhiambo cairo
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 16,352
- 22,958
Nina uhakika wewe hauishi TanZania na ndiyo maana umeandika utumbo ulioandika, eti uko tayari kufa, unafikiri kuna Mtz ambaye yuko tayari kufa kwa ajili ya fisadi Lowasa? Au hao bodaboda mnaowawekea mafuta na kuwajaza barabarani ndiyo unafikiri watakaposikia risasi bado watabaki kulemazwa na kufa kwa ajili ya fisadi Lowasa na Genge lake ambaye atakuwa amejifungia Masaki aua hata kwenye vila lake Ulaya?
Usichangane mambo, kumbuka TanZania siyo Kenya na wala WatanZania siyo Wakenya, wakenya walipigana na kuuwana kwa sababu kila mtu alikuwa anatetea Kabila lake na alikuwa yuko tayari kufa kwa ajili ya kabila lake sasa Mmachinga wa Masasi awe tayari kufa kwa ajili Mbowe wa kutoka Hai au Mtei wa Tengeru au sijui Tundu Lisi wa Singida kwa lipi?
Kabla kuandika mambo kama hayo jifunze kwanza kidogo Historia ya Dunia labda utaelewa ni mambo gani huwafanya watu wawe tayari kujitoa muhanga na kufa, hakuna Dunia hii aliyetayari kufa kwa ajili tu ya Mwanasiasa ambaye hana uhusiano naye wa karibu kama kikanda, kidini au kidamu!
Kwa kifupi nakuhakikishia hakuna Mtz atakayakaidi agizo la Raisi JMTZ kwa maana hakuna aliyetayari kuumia kwa ajili ya fisadi Lowasa, Mbowe, Tundu Lisu &Co.!
Barbosa unanisononesha kama kweli nawe ni mTz mzalendo, unashabikia upotofu !!?. Yaani leo hii waTz tufanywe kama kuku wa kizungu ???! Tupangiwe matokeo na tufurahi kuwa ndio AMANI ???!. Hapana tena mwambie kipenzi chako Jk chonde chonde asimalizie vibaya . Tunajua angependa mgombea ashinde kwa kishindo kama wakati wake (2005) . Hali ya leo kaisababisha yeye mpaka upinzani umekuwa mkubwa kiasi hicho.
Aache Mungu atupe kiongozi asitulazimishe