realMamy
JF-Expert Member
- Apr 28, 2024
- 5,058
- 11,926
Hasira. Kuna maana nyingi ya neno hasira na mojawapo ni Ile inayoeleza kuwa ni hali ya moyo wa mtu ulioumia au kujeruhiwa,hivyo huweza kusababisha hasira.
Inakuja pale mtu anapohisi amedhalilishwa, amedanganywa, amenyang’anywa haki, au mtu kavunja ahadi yake.
Ni kitu fulani kinacholeta utambuzi kuwa "hapa nimefanyiwa kitu kibaya".
Shida inaanza pale hasira ikikataa kutoka moyoni Wiki, Miezi, Hadi Miaka. Ndipo inapoacha kuwa hasira inageuka kuwa mzigo.
Hasara pia ni kila kitu unachopoteza ukiwa umebeba huo mzigo. Unapoteza amani yako, usingizi wako, afya yako, fursa zako, na hata watu wazuri walio kukaribu nawe leo.
Kwa lugha nyepesi Hasira ukiibeba muda mrefu, inageuka kuwa hasara.
Madhara ya Kuiweka moyoni Muda Mrefu
1. Unajiumiza Mwenyewe
Yule aliyekukosea anaweza kusahau. Wewe bado unachemka. Presha inapanda. Kichwa kinauma. Unafikiri unamlipiza, kumbe unajihukumu wewe mwenyewe kila siku.
2. Unajifungia Milango
Mtu mwenye hasira haamini mtu mpya. Fursa mpya ikipita, haioni. Kwa sababu moyo uko kwenye jeraha la zamani.
Unakuwa umeamua kuishi jana ndani ya leo. Unacheka kwa mdomo, lakini moyo haupo hapo. Hiyo ni hasara kubwa sana.
Ushauri: Acha hasira Kwa Ajili Yako.
1. Kubali halafu achilia.
Sema "Nimeumia. Ni kweli". Baada ya hapo jiulize: "Kubeba hii leo kunanisaidia nini?" Ukiona ni hasara tu, achana nayo
2. Zungumza.
Mweleze rafiki 1 unayemwamini. Au andika kwenye daftari. Hasira ukiitoa unasahau.
3. Samehe
Huwasamehe kwa sababu wanastahili. Unasamehe kwa sababu wewe unastahili usingizi mzuri. Unastahili kuishi bila mnyororo.
Neno la Mwisho
Hasira ni hasara kubwa.
Inakuja pale mtu anapohisi amedhalilishwa, amedanganywa, amenyang’anywa haki, au mtu kavunja ahadi yake.
Ni kitu fulani kinacholeta utambuzi kuwa "hapa nimefanyiwa kitu kibaya".
Shida inaanza pale hasira ikikataa kutoka moyoni Wiki, Miezi, Hadi Miaka. Ndipo inapoacha kuwa hasira inageuka kuwa mzigo.
Hasara pia ni kila kitu unachopoteza ukiwa umebeba huo mzigo. Unapoteza amani yako, usingizi wako, afya yako, fursa zako, na hata watu wazuri walio kukaribu nawe leo.
Kwa lugha nyepesi Hasira ukiibeba muda mrefu, inageuka kuwa hasara.
Madhara ya Kuiweka moyoni Muda Mrefu
1. Unajiumiza Mwenyewe
Yule aliyekukosea anaweza kusahau. Wewe bado unachemka. Presha inapanda. Kichwa kinauma. Unafikiri unamlipiza, kumbe unajihukumu wewe mwenyewe kila siku.
2. Unajifungia Milango
Mtu mwenye hasira haamini mtu mpya. Fursa mpya ikipita, haioni. Kwa sababu moyo uko kwenye jeraha la zamani.
Unakuwa umeamua kuishi jana ndani ya leo. Unacheka kwa mdomo, lakini moyo haupo hapo. Hiyo ni hasara kubwa sana.
Ushauri: Acha hasira Kwa Ajili Yako.
1. Kubali halafu achilia.
Sema "Nimeumia. Ni kweli". Baada ya hapo jiulize: "Kubeba hii leo kunanisaidia nini?" Ukiona ni hasara tu, achana nayo
2. Zungumza.
Mweleze rafiki 1 unayemwamini. Au andika kwenye daftari. Hasira ukiitoa unasahau.
3. Samehe
Huwasamehe kwa sababu wanastahili. Unasamehe kwa sababu wewe unastahili usingizi mzuri. Unastahili kuishi bila mnyororo.
Neno la Mwisho
Hasira ni hasara kubwa.