Wabongo mlivyo wanafiki, aki lost hapa mtaanza kuponda sasa hivi anatumia mnasema acheni atumie si za kwake? Najua mshikaji bado ni kijana mdogo sana na hiyo cash ina mzuzua na ukizangatia kwa mtanzania kwa umri kama wake kuwa na fedha nyingi kiasi kile ni nadra sana au naweza kusema yeye ndio wa kwanza..
Jamani mshaurini vizuri sio kumpa sifa za kijinga na mtanzania mwenzetu
Duh!
hapa dogo akiingia na jokate kudadadeki....
shori jokate hapo anauwazia mkwanja tu....
lol kudadadeki later kidogo hasheem na shori wake jokate wakasepa....viti vyao vikiwa na watu wengine....
JokateUkiacha Bils, Thabeet pia amekuwa akitembelea viwanja vingine vya dar karibu kila usiku ikiwemo Nyumbani Lounge kwa Lady JD na Mafian kwa Kimbau. Huko amekuwa na tabia ya kuingia nyuma ya counter na ku-serve vinywaji kwa wateja bure yeye mwenyewe na bili yote hulipa yeye. Alionekana akifanya kufuru hizo huku akiwa ameambatana na girlfriend wake, Jokate.
Amefanya nini tena?Jokate
Leo ni siku ya kufukua makaburi ya JokateJokate
WAtu mna upeo wa kuona mbali.Mimi ningemshauri Hasheem arudi Texas na kufanya mazoezi ya summer ya kati ya Yao, Olujuwon au Mutambo badala ya kutanua bongo kwa sasa. Ukweli ni kwamba kiwango chake kimeshuka kiasi kwamba timu ya Rockets inafikiria kununua contract yake. Hii ni kwamba wanamlipa pesa ya kumtoa kwenye timu. Hii sio nzuri kwani timu nyingine hazitaweza kumsajili mchezaji wa hivyo. Mimi ninajua Hasheem anao uweza wa kupandisha kiwango chake lakini ni mvivu na anapenda sifa badala ya game. Anaweza kupata pesa nyingi kwa miaka iliyobakia kwenye mkataba lakini ni lazima uelewe kwamba wewe bado ni mdogo na hiyo pesa bila kuwekeza vizuri na makodi ya marekani na ma agent utaishiwa mika 10 ijayo na huwezi kufanya kazi. Achana na marafiki ambao hawakuambii ukweli na tafuta vijana waliotulia kama kaka zako hapa Texas wakushauri bila kujali unawapa nini.
WAtu mna upeo wa kuona mbali.
Wengi wamepotea kwa kuendekeza umalaya.Starehe mwisho wake mbaya!!
Natamani kama angelipata muda wa kusoma ulichokiandika kwa wakati ule miaka zaidi ya 10 iliyopita. Ulikuwa ushauri wenye kila kitu, kuonya wapi atateleza na kupendekeza suluhisho. Kwa mara ya kwanza naona JF comment iliyokuja kuwa utabiri uliotimia. Wakubwa ni wakubwa tu, wameshaona mengi wasikilizwe wanaposhauri na uzuri ni kwamba ulikuwa huko huko USA so ulikuwa ukishauri sio kwa kubabia bali kwa uzoefu halisi wa huko.Nashukuru nilikuwa na mimi nasishi Houston lakini hakusikiliza sasa anahaha bure. Mengi nayo ongea hapa mtandaoni yanatimia