Miss Halima
Senior Member
- Aug 4, 2026
- 168
- 374
Chelsea wameweka thamani ya pauni milioni 100 (sawa na shilingi bilioni 400) kwa Pedro Neto iwapo klabu hiyo itaamua kumuuza winga huyo Mreno katika dirisha hili la usajili.
Pedro mwenye umri wa miaka 26 amekuwa akivutia vilabu kadhaa kutoka Premier League na nje ya England, huku Al Hilal ya Saudi Arabia ikihusishwa kwa kiasi kikubwa na mchezaji huyo wiki hii.
Hadi sasa, hakuna ofa rasmi iliyowasilishwa Chelsea kwa ajili ya Pedro, lakini viongozi wa klabu hiyo wanafahamu kuwa kuna timu zinazomvutia.
Chelsea imefikia thamani hiyo baada ya kuona bei kubwa zinazowekwa kwa mawinga wengine katika soko la usajili. Yan Diomande amejiunga na Real Madrid kutoka RB Leipzig kwa ada inayoweza kufikia pauni milioni 120, huku PSG ikimthaminisha Bradley Barcola kwa zaidi ya pauni milioni 100, ambaye pia amekuwa akihusishwa na Liverpool.
Pedro alijiunga na Chelsea mwaka 2024 akitokea Wolves kwa ada ya pauni milioni 54
Pedro mwenye umri wa miaka 26 amekuwa akivutia vilabu kadhaa kutoka Premier League na nje ya England, huku Al Hilal ya Saudi Arabia ikihusishwa kwa kiasi kikubwa na mchezaji huyo wiki hii.
Hadi sasa, hakuna ofa rasmi iliyowasilishwa Chelsea kwa ajili ya Pedro, lakini viongozi wa klabu hiyo wanafahamu kuwa kuna timu zinazomvutia.
Chelsea imefikia thamani hiyo baada ya kuona bei kubwa zinazowekwa kwa mawinga wengine katika soko la usajili. Yan Diomande amejiunga na Real Madrid kutoka RB Leipzig kwa ada inayoweza kufikia pauni milioni 120, huku PSG ikimthaminisha Bradley Barcola kwa zaidi ya pauni milioni 100, ambaye pia amekuwa akihusishwa na Liverpool.
Pedro alijiunga na Chelsea mwaka 2024 akitokea Wolves kwa ada ya pauni milioni 54