Kwako Mheshimiwa Raisi Jakaya Mrisho Kikwete,
15, September, 2007
From: Field Marshall ES (Emergency System)
Kwa kawaida, katika nchi kama yetu Tanzania, state organs kama Bunge, Mahakama, na Jeshi, huwa vinatakiwa viwe vimeundwa na katiba yetu kutetea na kulinda the common good na interest ya jamii yetu. Kwa hiyo haki za binadamu na common good, ni complimentary values ambazo wanasiasa na viongozi wetu Tanzania, mnatakiwa kuzielewa na kuziheshimu, ili msije mkajikuta mko upande wa pili wa wananchi, kama vile tatizo linaloendelea sasa hivi la Bunge letu na Mbunge maarufu Zitto, tatizo ambalo linatufanya sisi wananchi wengi kuwa na mtizamo mzito kibin-adam katika kutathmini ajali iliyomkuta Mbunge wa CCM, jimbo la Mchinga hivi karibuni.
Tabia ya yenu viongozi wetu, kuvitumia vyombo muhimu vya state organs kwa kuwa-harass na kuwaonea, au kuwafunga bila ya due process wale wanaoajaribu kuyauliza baadhi ya maamuzi yenu kwa taifa hili, ni tabia mbaya yenye nia ya kutaka kui-reduce nchi yetu ili iwe ni almost the property of predatory elites. Ukweli ni kwamba ni collectivity of persons ambao mna-occupy commanding positions katika some important sphere of social life na ambao mna-share a variety of interests arising from similarities of training, experience, duties na the way of life yenu.
Ili ku-promote interest zenu, huwa mna-seek to cooperate and coordinate, matendo yenu kwa means za corporate organizations, kama vile kamati kuu yaani CC. Interest zenu zinaonekana kuwa articulated in a formal association hasa kwenye political sphere. Ingawa pia mnaanza kuzi-extend interest zenu mpaka kwenye vitengo muhimu kwa jamii yetu, kama ujenzi, afya, na biashara nakadhalika.
Wananchi masikini na walalahoi kama sisi na viongozi wetu kina Mheshimiwa Zitto, huwa hamtualiki ku-take part au kutoa maoni yetu kwenye hayo maamuzi muhimu ya taifa letu, the matter of fact hata public opinion kwenu does not matter. Tabia kama hizi zinaashiria tu kuwa serious reform katika kuandaa system yetu kuanzia ya katiba mpaka ya siasa, hapa nchini kwetu Tanzania inahitajika sasa hivi na tena kwa haaraka sana! Maana wanasiasa wa CC peke yenu historia inaonyesha kuwa hamuwezi ku-accomplish hiii task ya reform, bila ya kutuhusisha sisi wananchi at large, na sio nyinyi kutuwekea agenda kama alivyojaribu kufanya waziri Nagu majuzi, kwa kutuambia kunahitajika mabadiliko ya term za wabunge. Hatuwaamini tena wanasiasa wako na mawaziri wako ambao wengi wao katika kipindi cha mwaka mmoja tu cha madaraka yako, wamekuwa mstari wa mbele kujaribu ku-reduce siasa to a game of lying, corruption, na manipulating sisi wananchi masikini na walalahoi.
Kwa hiyo Mheshimiwa rais, tuki-examine the aforementioned situation with a critical eye, tutagundua kuwa taifa letu lina-present an odd dichotomy kati ya political activists na critical thinkers kama kina Mheshimiwa Zitto, na the common good kwa taifa letu. Ina maana kwamba itakuwa ni vigumu kwetu kama taifa kuwa na peaceful na prosperous society katika situation ambapo viongozi kama nyinyi ambao mnatakiwa ku-stand for the common good, mnaonekana kuanzisha vita vikali dhidi ya sisi wananchi masikini na wawakilishi wetu kama Mtikila, na Mheshimiwa Zitto.
Kwa hayo machache, ninaomba kwa unyeyekevu mkubwa kukumbusha kuwa taifa bila ya kuwaheshimu political activists na critics, kama kina Mheshimiwa Zitto, linakuwa ni taifa lilokufa kisiasa, na sisi Tanzania kama hatujafikia hicho kifo, basi tuko njiani kwa mwendo wa kasi sana kukifikia, Mheshimiwa rais pole sana na ajali ya mbunge wa Mchinga.
Wako Mwananchi aliyekupigia kura ya urais,
Field Marshall ES (Emergency System)