Harusi ya kilokole mchango laki wizi mtupu

Harusi ya kilokole mchango laki wizi mtupu

Ukiwa kwenye kamati utatumiwa msg mbili mbili kukumbushwa kikao na mchango kama vile utahusika kwenye uroda! Mimi nachoka.
 
Kuanzia leo sitachangia harusi ya kilokole zaidi ya buku ishirini.
Siwezi changia laki halafu niishie kupewa juisi ya azam na soda,..huu ni wizi mtupu!


Uchangiaji harusi ni kwa ajili ya yote kutafunwa kwenye sherehe? Ulitegemea hata ungetoa million kwenye hiyo harusi ingebadili imani yao na kuweka vileo? Hivi nini maana ya mchango? Na nini maana ya ulokole?
 
Walokole hao naooo....walianzaje kuomba mchango kwa wewe mlevi?
 
waongooooo tu wewe mlevi na walokole wapi na wapi, ulishaona swala na simba wakafungiwa zizi moja
 
mkuu hizo Azam si ni 3000 wakati bia buku 2500 ila mimi nilidhani mchango ni hiari ya mtu kuchangia hapo kama kuna kiwango sio mchango bali ni kulipia entrance fee jambo ambalo linaondoa maana ya harusi na kujumuika kwenye sherehe mimi naona sasa ifike wakati wedding iwe bottle party kila mtu kuja na kinywaji chake na kununua msosi wake anaotaka

Taratibu tutafika. Ebu fikiria wale ndugu waliotoka kijijini waje wanunue chakula kwenye arusi yako. Pia waje na vinywani vyao. Akina mangi waje na mbege kabisa!

Ninacho kiona tutafika mahali tutatuwa kama jirani zetu Kenya. Hamna kuchangisha. Arusi ni issue ya mhusika na familia yake. Fanya kwa uwezo wako na invite watu wachache wa karibu.

Kwa sasa ni too much - mchango wa arusi, send off, kitchen party kwa akina mama, birthday, graduation, kipaimara, jubilee ya ndoa nk
 
Back
Top Bottom