Harusi kuanza kulipiwa kodi

Harusi kuanza kulipiwa kodi

Kwahyo kila atakayekuwa anaatend aruc na yeye atapashwa kulipa kodi?

Kumbuka mfanyakazi anagenerate income while haruc zinafanya expenditure ambzo znakuwa zimeisha lipiwa kodi. Sasa utakataje kodi kwenye expenditure?

Wakatwe kodi ma mc...na watoa huduma wote wa siku hiyo...
 
NAFIKIRI itakuwa kama hivi:

1. Kumbi zote za sherehe zisajiliwe.
2. Wamiliki wa kumbi sharti mwanzo mwezi wawasilishe TRA list ya sherehe zote zinazotarajiwa kufanyika ndani ya mwezi huo.
3. Sherehe yoyote itakayofanyika kwenye ukumbi usiozidi sh. 700,000/= hakuna kodi.
4. Ukumbi wa sh. 700,001/= au zaidi kodi 100% ya bei ya ukumbi au 18% ya budget ya sherehe, whichever is higher.
5. Maafisa wa TRA kutinga ukumbini kabla ya sherehe kuanza na waandaji waonyeshe vifuatavyo kwa uhakiki:
a. EFD ya ukumbi
b. EFD ya Caterer
c. EFD ya Vinywaji
d. EFD ya MC
e. EFD ya Mpambaji
f. EFD ya mpiga picha
g. EFD ya gari za kukodi
i. EFD ya saloon
n.k
Mnaonaje hapo? Bila shaka meanza kupapenda

Mfano:
Bajeti sh. 20,000,000/=
Ukumbi sh. 2,500,000/=

Kodi:
(a) 18% = 3,600,000/= au ukijitahidi kudanganya kuhusu bajeti, unaenda kwenye (b)
(b) 100% ya Hall = 2,500,000/= au ukijifunza kuacha makuu, utafuta ukumbi wa 1,500,000/=, unahamia (c)
(c) 100% ya Hall = 1,500,000/=

Teh tehe, serkali haijatoka kapa
 
Kifo,msiba na kuzika vyote hivyo ni majonzi wakati harusi ni sherehe na anasa..!kila mtu ata kufa ila siyo kila mtu atafanya harusi..Harusi ni uamuzi binafsi wa kufanya starehe..!

Harusi ndio chanzo cha wewe kuwapo hapa ...ukianza kuiangalia hii kama starehe uono wako ni mduchu sana.
taifa imara linajengwa na familia sio na watoto wa mitaani...
katika vyanzo vyote vya kodi ndio wachumi wetu wafikirie arusi ...tuna kazi kubwa sana....tutasubiri sana
badala ya kutuambia watafanya nini kwenye madini na gas ..wanakuja kuleta hoja hizi za kuwakamua raia.hili siis kama waislam ni ushetani na tutalipinga halina faida yoyote kwa taifa...
 
Mimi nafikiri hapa serikali iangalie kwa jicho la pili hizi ni hela za michango ya watu ambao tayari hela hizo wanazozichanga zimepita katika makato mbalimbali ya kodi kulingana na kila mchangiaji aanavyoweza pata kipato chake kupitia vyanzo vyao walivyo navyo.Sion sababu ya kukata kodi ya ongezeko la thamani kwa kuwa hiyo siyo biashara kabisa ni eneo la huduma ya jamii ambao wameamua kumwezesha mtu/jamaa/rafiki yao ili afanye sherehe kwa tukio la kuoa/kuolewa.Wale wanaotoa huduma ndani ya sherehe hizo kama vile kumbi za sherehe/chakula/video &still picture wote kwa ujumla wao wanalipa kodi ya ongezeko la thamani( VAT) na kama hawalipi najua ni kwamba bado serikali inaweza kuwabana walipe kodi hiyo.Kwa mtu ambaye ni wamwisho na nirahisi kumpata ambaye ahami labda ukumbi avunje.So huyu abanwe kwamba watoa huduma wote wahakikishe wameacha kodi ya ongezeko la thamani kama hawana namba ya utambulisho ya mlipa kodi(TIN) na wale ambao wana TIN wanatakiwa wanapotoa huduma watoe legal receipt ambayo itatoza kodi kwa kiasi ambacho gharama ya malipo ya huduma wanazo toa.Hawa wote wakilipa kodi inavyostahili sidhani kuna sababu ya kutoza kodi michango ambayo haiendi kuzalisha faida yoyote .Sidhani kwamba ni sahihi
.Tatizo lilopo watoa huduma wengi niwatu ambao wanakuwa kama hawatambuliki kisheria.Ni wachache ambao wanakuwa kwenye makundi ya kampuni.Hapa nikuweka muongozo kwa wenye kumbi za sherehe,kwamba wahakikishe watoa huduma wanakuja kutoa huduma ktk kumbi zao wakabidhi nakala ya risiti za kisheria ikionyesha malipo ya vat ya gharama halisi ya huduma walizolipwa tofauti na hapo wasiwaruhusu kutoa huduma.Ikitokea wakawaruhusu wao wenye kumbi wawajibishwe kulipa kodi ambayo hakulipwa na mtoa huduma. Hayo ni mawazo yangu wadau.MUNGU ibariki Jamhuri ya Muungano Tanzania na viongozi wetu wote wa taifa mpaka wa nyumba 10 bila kujali itikadi ya vyama vyao.Amen!
 
haa haa watu watapunguza kasi ya harusi maana zilizidi.
 
Mheshemiwa Raisi kama unasoma mawazo yetu.Nakuomba kupitia waziri wa fedha ,wa ziri wa sheria na katiba pamoja na watengeneza sera za za vyanzo vya mapato. Waulize Mamlaka ya mapato kodi za ndani ni watoa huduma wangapi wanaotoa huduma ambao wanafahamika,walisha wahi kutoa huduma katika sherehe zao/ndugu/familia zao wanawatambulika kama wanajua ni walipa kodi na wanalipa kodi ya ongezeko la thamani.Yani hawa watu hawalipi kodi kabisa na hata wenye kumbi wana leseni za biashara na wanatambulika kama walipa kodi hawalipi inavyostahili.Leo maharusi wanaenda ukumbini kufanya biashara au watoa huduma ndiyo wanafanya biashara na kupata faida.We have to look this matter very close.Waambie Mamlaka ya mapato watimize wajibu wao kwa walipa kodi ambao wanapaswa kulipa kodi wakiwa wanatoa huduma kwenye sherehe zote.Waambie wasijaribu kuintroduce vyanzo ambavyo upande wa shiling ambao ni watoa huduama hawalipi.Leo gari inabeba mzigo kwenda hapa ndani ya Tanzania/Njee ya tanzania hawatoi receipt kabisa.Inatakiwa wakitoa huduma watoe basi legal receipt na na hawa ndiyo matajiri tena wana misamaha ya kodi nyingi tu,leo walala hoi wanachanga hela zao wanataka wakatwe kodi?Waambie wakupe orodha ya watoa huduma ambao wao wana wafahamu na wenye kumbi za sherehe zote Dsm tu, uone kodi wanazolipa nadhani utakasrika sana. Hakuna maana kupunguza payee (Pay as well)kuwa 9% alafu unachukua kodi kwa mtindo mwengine mpya.Vyanzo vya mapato vipo kwenye mafuta na
ges na madini.Leo kama serikali itaamua tu pikpik zote zilipe annual fees ni chanzo kikubwa sana cha mapato.Na ikasema annual fees za vyombo vya moto vitatozwa automaticaly kupitia bidhaa ya nishati ya mafuta ya petrol/diesel yanapoingia.Serikali hapa itapata mapato ya kutosha kwa mfano kila ltr mmoja ikatoza tsh 50 itapata mapato mengi sana kuliko maana hapa hata vyombo ambavyo havina annul fees kwakuwa vinatumia nishati ya mafuta vitakuwa vinachangia pato la taifa.Siyo kujaza
folen ya ya watu wanao renew raod license na kuover work mtandao na kuwalipa Max malipo hela nyingi ambazo hazina tija kabisa nikupoteza pato la taifa.
 
Serikali wakate tu kodi pia watazame kwenye nyumba za kupanga nako nijipu kubwa kuna watu wenye nyumba wanatoza kodi in term of dollar wakati wao hawalipi kodi serikalini.
 
Tunavyokwenda wanaweza wakadai kodi hata kwenye michango ya rambi rambi
 
Ni lazima au hiyari kuchanga katika harusi ya mtu mwingine?
Usipochanga inakua lawama, sasa kukata mzizi wa fitina bora zisiwepo au zipungue michango ipungue.
Ndoa ni wewe na mkeo harusi haihusiki wala haina maana, ukioa fuata taratibu kama islamic hakikisha shekhe yupo, kam mkiristo hakikisha viongozi wa kanisa wamefungisha ndoa yenu na kama ndoa kiserikali hakikisha umefanya zile taratibu mara hakimu et al....
Hizo pesa zinazosalia weka miradi na mkeo maisha yaende mbele
 
Tunavyokwenda wanaweza wakadai kodi hata kwenye michango ya rambi rambi
Hii ni income tax? Au nini kwa sababu tayari vendors wengi wa harusi wana efd machines wanalipa vat.
 
Zaidi ya 90% ya wachangiaji wa hii mada hawajaisoma hii habari kwenye gazeti lililoandika hii story. #Only in Tanzania
 
Nani kasema zilichangwa?, jenga hoja kwanini harusi iwepo usianzishe hoja kutokana na hoja zangu tena arguments zako za kitoto kweli
Harusi inakuwepo kwa sababu anayefanyiwa harusi na wanaowezesha (wachangaji) wamekubali hali hiyo kwamba imo ndani ya uwezo wao, na hawavunji sheria yoyote ya nchi. Sasa kama hupendi kufanyiwa harusi au kuchanga harusi ya mtu, bado uko sahihi kwa sababu jambo lenyewe ni la hiyari na halilazimishwi au kuzuiwa na sheria yoyote
 
Harusi inakuwepo kwa sababu anayefanyiwa harusi na wanaowezesha (wachangaji) wamekubali hali hiyo kwamba imo ndani ya uwezo wao, na hawavunji sheria yoyote ya nchi. Sasa kama hupendi kufanyiwa harusi au kuchanga harusi ya mtu, bado uko sahihi kwa sababu jambo lenyewe ni la hiyari na halilazimishwi au kuzuiwa na sheria yoyote
Vema lakini tukirudi kwenye umuhimu bado siuoni ni kama anasa tu au sawa na kuandaa sherehe isiyo na tija.
Maneno yangu sio msahafu wanaopenda sherehe waendelee mimi binafsi NEVER
Tena nachukia sana hizi sherehe katika maisha yangu, kuna mijitu hata mtoto wa jirani yake afaulu hasaidii hata shilingi mia ila akisikia harusi mbio mbio kariakoo kununua nguo na kutoa michango ya harusi.
 
Inabidi nifunge Harusi mwaka huu tuu sasa, naona tunaaribiana Honeymoon bure hapaaa
 
Back
Top Bottom