Harusi iliyonigusa Jumamosi hii

Harusi iliyonigusa Jumamosi hii

BEHOLD

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2013
Posts
5,057
Reaction score
10,731
Jumamosi hii nimehudhuria ibada ya ndoa iliyokuwa inafungwa katika kanisa moja hapa Jijini Dar-Es-Salaamu.

Ibada ilienda na ukafika wakati bwana arusi akaambiwa na kasisi kufunua kipande cha shela kinachofunika uso wa bi arusi, kama ishara ya maharusi kuunganishwa rasmi.

Mara baada ya Bi Arusi kufunuliwa uso na kuangaliana uso kwa uso kwa mwenzi wake (Bwana arusi), kilichofuata ni bibie huyo kububujikwa na machozi kwa, maana ya kulia, yasiyokifani kwa takribani dk 5.

Badae ibada ikaendelea.

Akiendelea na mahubiri Kasisi alikiita kitendo kile cha kutokwa na machozi cha bi arusi, kama ishara ya usafi, uadilifu, malezi na makuzi mema, ambayo binti amekua nayo katika kipindi cha maisha yake.

Aidha aliendelea kuwa enzi hizi ndoa nyingi ni kama maonesho au fashion ndio maana imekuwa kawaida kuona ndoa inafungwa na bibi arusi ni mjamzito, bibi arusi kuingia madhabahuni na nguo za aibu akiwa nusu uchi, ndoa nyingi kutodumu maana upendo wa Ki-Mungu haupo tena bali upendo wa vitu na unafki na kadhalika.

Nadhani lipo zuri la kutafakari hapo!
 
Haya basi wataanza kulia madhabahuni maana ndio usafi sasa
 
so machoz ni ishara ya bibi harus bikra??


maana dot com tunaoana watu tuna msururu wa ma x wanajaza yutong.. amemegwa/mega mtaani kwao, chuoni, kazini, kwa ndugu,kazini, kanisani, yaani kila alipowai kuishi ana mtu aliyemmega au kumegwa
 
Mmh kutokwa na machoz ndo ishara ya usafi na uadilifu??😅😅
Au hyo ni nahau umeitafsiri
 
Sasa na make up ilikuwaje.......?.....au walirudia.......?.......
 
Kulia kuna maana nyingi,just imagine mchumba kakupigapiga tarehe kibao kila Sikuanaahirisha harusi, una mtoto nae ,ashakutenda mengi tu,ashakuabisha sana kwenu,je siku anakuoa utaacha kulia machozi?
 
Du! Bado natafuta connection ya kulia na usafi (purity). Analia kwasababu anahofia kinachoenda kutokea honeymoon, analia kwa furaha ya kumpata mume? Analia kwakuwa kapata uhuru toka mateso ya wazazi? Analia akikumbuka alivyotendwa na ndoa haikuwepo au? Just thinking out loud
 
Kulia kunaweza kuwa ni maonesho pia!

Tumbo kutovimba haimaanishi hana mimba!

Kutovimba tumbo haimaanishi hawajazini!

Pengine analia kwakuwa hakutegemea kuolewa na ndio ameitafuta kwa muda mrefu!
Kulia wakati wa harusi ni moja ya fashion ya mabinti walio wengi
 
She was deeply moved labda.
" A time to weep and a time to laugh, a time to mourn and a time to dance" (Ecclesiastes 3:4).
 
Kulia kunaweza kuwa ni maonesho pia!

Tumbo kutovimba haimaanishi hana mimba!

Kutovimba tumbo haimaanishi hawajazini!

Pengine analia kwakuwa hakutegemea kuolewa na ndio ameitafuta kwa muda mrefu!
Kulia wakati wa harusi ni moja ya fashion ya mabinti walio wengi
wengine wanalia kwa kumuonea huruma bwana harusi kwamba kaangia choo cha kichina
 
Ahaaaaa watu na vijicoment vyenu. Ahaaaaa siku ya harusi yangu nitalia ndoo nzima, iwe ni ishara ya kumisi vitu ka jf na kumuhudumia huby. Tena mashoga zangu ntawamis maana nitamisi umbea fulani hivi mwisho nitamis harakati za cdm yaan nahisi ntakuwa busy sana hapa lazima nidondoshe chozi etc ahaaaaa!
 
Kulia si usafi. Yawezekana machozi yalisababishwa na
1. Kapigwa kalenda mwaka wa nane nwishowe kaolewa.
2. Hajiamini kama anaweza kuwa na mwanaume wa hadhi hiyo.
3. Kaachika mara kumi na tisa ya ishirini kabahatika
4. Anahisi kaukata
 
Back
Top Bottom