Harufu ya ubwabwa porini

Harufu ya ubwabwa porini

Habari za jumapili wana JF.
Bila kupoteza muda wadau naomba kuuliza,Je ile harufu ya wali (wali nazi) ambayo tunaisikia tukiwa porini au msituni tena sehemu ambayo haina makazi ya watu inatokana na nini?
Cc. mshana jr
Babu alisema huyo ni nyoka anajivua gamba
 
Mara nyingi tu lakn sikuwahi kuprove kwamba ni kweli kuna chatu around.
Upo
Mkuu ukiwa porini ukanusa harufu ya ubwabwa tena ule unanukia kama Thai Jasmine am a Basmati timua mbio hapo kuna bonge la joka. Siyo uwongo hii ni kweli ila nadhan ni kuhusu nyoka alivyoumbwa kibailojia
Mzeeupo copenhagen sehem.gani
 
Katika ulimwengu huu kuna mambo mengi mno ya ajabu, kuna kitu kinaitwa miungu, hawa miungu wamegawanyika katika sehemu nyingi, kwenye mito,milima,mapango na mabwawa. Katika hali ya kupatika kwa harufu ya wali huwa mambo mawili, kwanza ni makazi ya miungu hao pili ni makazi ya nyoka ambae kwa namna moja au nyingine nae pia ni miongoni mwa miungu. Unaweza wakati mwingine ukakuta hata vyungu vya kupikia mahala hapo
Acha shirki
 
Mbio mbio kumbe unamkimbilia mwenye hiyo harufu.

Mambo ya mbio mbio si mazuri.

Unamsindikiza mgeni akapande treni, mnakuta treni inaondoka mnaikimbiza.

Mbio mbio zako unajikuta umepanda wewe treni mgeni wako kaachwa

Unaishia kumrushia funguo asilale nje ww unaenda kulala stendi.
Haaa haaa yaani ndivyo ilivyo, kuna mmoja alikata ticket ya siku inayofuata sasa mwenye kaja kabla ya siku halafu anagombea siti balaa wanakuja wahusika kuangalia tarehe kumbe yeye sio siku ya kusafiri aliona aibu hata sijui kama aliendelea ama laa
 
Haaa haaa yaani ndivyo ilivyo, kuna mmoja alikata ticket ya siku inayofuata sasa mwenye kaja kabla ya siku halafu anagombea siti balaa wanakuja wahusika kuangalia tarehe kumbe yeye sio siku ya kusafiri aliona aibu hata sijui kama aliendelea ama laa
😂😂😂
 
Du jamani siyo nyoka wala majini bali huwa ni harufu ya miti furani hivi tatizo sijui jina ila hiyo miti inatoaga matunda madogo madogo meusi hivi, miti hiyo ikifika mida ya jioni hususani jua kinapozama huwa inatabia ya kutoa hiyo harufu
Ingesha enea mtaani, mua40 mchungu tu na tayari tuko nao kitaa Kisa dawa, sembuse huo wenye harufu ya ubeche, mashetani hayo

Sent from my TECNO LA6 using JamiiForums mobile app
 
Kilimanjaro mogombani ukiona gamba la nyoka lenye vutundu kama net,jua nyoka kajivua gamba,hio huleta hio harufu
 
Katika ulimwengu huu kuna mambo mengi mno ya ajabu, kuna kitu kinaitwa miungu, hawa miungu wamegawanyika katika sehemu nyingi, kwenye mito,milima,mapango na mabwawa. Katika hali ya kupatika kwa harufu ya wali huwa mambo mawili, kwanza ni makazi ya miungu hao pili ni makazi ya nyoka ambae kwa namna moja au nyingine nae pia ni miongoni mwa miungu. Unaweza wakati mwingine ukakuta hata vyungu vya kupikia mahala hapo

kwa hyo unataka kunambia hao miungu ndo wanakuwaga wanapika huo wali kwny hvyo vyungu? tangu lini kiumbe ambacho ni roho kikahitaj chakula?
 
Sasa hivi kuna harufu za viazi vitamu vya kuchoma sijui nayo ni nini? Nipo porini sana sema kuna tambarare pana na baadhi ya mito nasubiri nijue ni kitu gani hiki hii harufu inakolea mno majira ya saa mbili usiku
 
Back
Top Bottom