Harambee za Lowassa zinakera

MWALLA

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2006
Posts
16,952
Reaction score
10,510
Binti yangu amechapwa bakora kisa sijamlipia 5000= ya harambee ya lowasa hapa wilayani kwetu...
Imeniuma sana mtoto wangu kupewa adhabu wakati mzazi nipo. Je hiyo adhabu ndio uwe mchango wangu wa harambeee hiyoo ya Lowassa

Vilevile nashindwa kuelewa huyu Lowassa yeye ni mbunge wa Monduli.Sasa kuja huku Temeke kufanya kampeni hizo eti tuchangie halafu yeye atoe zake aunganishe na zetu .. Kwanza atueleze anazitoa wapi mbunge huyuu?

Vile vilee huku Temeke yupo mbunge wetu iweje sasa yeye awe kama msindikizaji tu badala kuwa ndio mgeni mkuu apokee huo mshiko wa Lowassa? Badala yake Lowassa ndio kafanywa mgeni mkuu... Shame!!!

Kampeni za Lowassa zilianzia makanisani baadae misikitini now! Zimehamia mashuleni tena tunaambiwa ni lazima kutoa hiyo harambee la sivyo mtoto hasomi shule.

Jamanii... Jamani... Wananchi wenzangu.. Hebu tusaidiane hili.. Kweli mwanangu afukuzwe shule kisa sijatoa 5000= ya harambee ya Lowassa?
 
sasa unataka uletewe maendeleo na nani? Maendeleo inabidi uhimizwe tena elfu tano tu!! hongera Lowasa kutuhimiza katika maendeleo..go go go...
 
TAREHE 26 OCT LOWASA MBUNGE WA MONDULI (SIYOWAZIRI MKUU MSTAFU NI WAZIRI ALIYETIMULIWA NA KIKWETE KWA MANUFAA YA NCHI) NDIO MGENI RASMI ANAKUJA KUFANYA HARAMBEE ST ANTONI SEC SCHOOL mbunge wetu WA TMK yeye anakuja kama mgeni mualikwa this is SHAME!!!!!!!!
 

Umezoea kufanyiwa changia maendeleo ya elimu ya mtoto wako muda wa kuja kumchafua Lowasa JF ungeutumia kutafuta hiyo pesa.
 
sasa unataka uletewe maendeleo na nani? Maendeleo inabidi uhimizwe tena elfu tano tu!! hongera Lowasa kutuhimiza katika maendeleo..go go go...


PUMBAFUUUU....... Yaani mnaendekeza kumbeba fisadi serikali ipo wapi hiyo siyo kazi yetu kuchangia harambee za kipuuzi kwani michango ya shule tunaielewa lkn sio michango kama hii.. ya kampeni za kutaka urais tu
lowasa hawezi kuteuliwa kuwa rais kwa style anazotumia.. hela zake tunakula kama kawaida ila ajuee hawezi kuwa rais wa chi hiii atabaki kuwa mbunge wa monduli kwa huruma ya wamasai wake.

JK alishafunguka zamanii kuhusu lowasa kwamba hafai hata kwa kulumagia. TAMBUA HILO WSE MBURULAAA..
 
mwache arudishe kdogo pesa alzotuibia. Lakin urais hatumpi.

kabisaaaaaa... Kwanza alizochukua zinatosha.. Amekuwa waziri miaka 2 tu kaleta richmond hebu tumpe nchi tuone atakavyokomba.. Nyoooooooo!!!! Hapewi mtu hapa...
 
Huyo ndio JANGA LOWASA

Acheni akili za kitoto na kuungana mkono kwenye mambo ya kijinga,ebu muulize amechangia harusi ngapi tena zaidi ya hiyo pesa ya bia mbili kwa return ya kupigiwa makofi kikaoni lakini buku tano inamfanya aende kununua vocha na kuja kumsema mchangia maendeleo ya nchi.Shame on you Misukule
 

wewe humjui lowasa weweeee!! Tuliza makalio yakooo hapoo ulipo
 
Ebu ficha ujinga wako muda wa siasa za majitaka umepitwa na wakati watanzania watamchagua mchapakazi na yule atakaewaletea maendeleo mengine baadae.
 
You spy on me?? Go go go go!!!! Hahahahaaaaaa!!!
 
wewe humjui lowasa weweeee!! Tuliza makalio yakooo hapoo ulipo
Hatuko hapa kujuana lakini hata wewe ninawasiwasi na uraia wako mtanzania halisi hana tabia na kulia katika kuchangia maendeleo ya taifa lake.Utakuwa ni muhamiaji haramu.

 
Na bado hamjachapwa. Mpeni urais muone. Mpaka familia italiizwa bakora kurudisha hela anayotoa kujenga makanisa.
 
Ieleweke kuwa kiongozi yeyote mwenye kutaka kuwaletea maendeleo watu wake si lazima asubiri aingie ikulu.Lowasa anaongoza kwa vitendo na wenye akili timamu wanamtambua.
 
Mimi nadhani hawa viongozi wetu kuna wakati masuala mengine hawayafahamu wapambe wao wanawadanganya
 
kweli mfa maji haachi kutapa tapa, watanzania hawachagui mtu kuwa rais, wanachagua mgombea wa c.c.m tu so ombeni ccm wasimsimamishe kama mgombea wao coz wakimsimamisha tu, ndo atakuwa rais wenu

my take: msisahau ule mfano wa kabaila wa kwenye bible ambaye kuna watu walikuwa hawamtaki awatawale kwa kigezo cha anakusanya asipotawanya, anavuna asipopanda n.k, cku alipopata ufalme wakabaki wanang'aang'aa sharubu tu
 
sasa unataka uletewe maendeleo na nani? Maendeleo inabidi uhimizwe tena elfu tano tu!! hongera Lowasa kutuhimiza katika maendeleo..go go go...

usiwe kama umetoka mirembe, anacholaumu yeye ni kupigwa binti yake kwa kosa la mzazi.

soma uelewe sio unakurupuka tu.!
 
kabisaaaaaa... Kwanza alizochukua zinatosha.. Amekuwa waziri miaka 2 tu kaleta richmond hebu tumpe nchi tuone atakavyokomba.. Nyoooooooo!!!! Hapewi mtu hapa...

Mwala usiwe na akili Kama jina lako maendeleo lazima uchangie sio kulalamika hovyo kama Dr Kikwete anavyo lalamika na kusahau alicho ongea, jaribu kutizama nani alieleta iptl na Richmond ndio alieileta hakuna mpenda maendeleo kama Mh Edward Ngoyai lowasa nenda wilayani kwake uone acheni uzindaki shukuru mwanao atapata madawati na vitu vya muhimu shuleni pole sana
 
sasa unataka uletewe maendeleo na nani? Maendeleo inabidi uhimizwe tena elfu tano tu!! hongera Lowasa kutuhimiza katika maendeleo..go go go...

usiwe kama umetoka mirembe, anacholaumu yeye ni kupigwa binti yake kwa kosa la mzazi "kama lipo"

soma uelewe sio unakurupuka tu.!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…