Dr. Slaa amekiri kuwa mchungaji Gwajima ni rafiki yake,mchungaji Gwajia hali kadhalika. Inapotokea marafiki wakaanza kuumbuana mbele za watu, ujue watu hawa wote wawili wana tatizo. Mchungaji, mara nyingi husikia siri nyingi za watu hasa waumini wake. Ikitokea mchungaji anasema juu ya muumini wake aliyemsaidia kibinadamu au kiroho mbele za hadhara ujue mchungaji huyu anapungukiwa na taaluma ya kichungaji na hafai kuchunga kondoo wa Mungu.
Biblia takatifu inasema vita vyetu si vya mwili na nyama bali vya roho. Mchungaji Gwajima anayasema haya ili kulipiza kisasi kwa yale aliyoyasema Dr. Slaa kuhusu yeye, lakini Biblia takatifu inasema' kisasi ni cha Bwana'.
Ukitafakari kwa makini kiini cha kufarakana kwa marafiki hawa tena wote wa UKAWA, ni ujio wa Edward Ngoyai Lowasa.
Siyo hawa wawili tu bali kuna makundi mengine mengi ndani ya ukawa yanatofautiana. Kwa watu wanaoona mbali wao wawili si maadui bali adui yao ni Lowasa kwa kuwa amekuja kuwafarakanisha. Hapa ndipo palipohitaji busara ya hali ya juu kutambua ni nani hasa adui yao badala ya kusema sijui Josephine sijui Dr. Slaa, sijui Gwajima.
Kama Gwajima kweli ni mchungaji wa kiroho, Roho wa bwana angemfunulia kabla hata kumkaribisha Lowasa. Angemuonya kiroho kuwa huyu anayekuja, haji kwa mema, anakuja kuwafarakanisha mtu na rafiki yake, mtu na mkewe nk nk. Gwajima anasema kazi ya mchungaji ni kuwapatanisha waliofarakana lakini anasahau kuwa hata yeye anafarakana. Mfarakani atawapatanishaje wafarakani.
Lugha wanayoongea wagomvi ndiyo hiyohiyo anayeongea mpatanishi, atafanikiwaje kuwapatanisha wengine? Mchungaji mwema ni yule anayeleta maneno matamu mahali penye maneno makali, analeta amani mahali penye vita. Katu hawezi kua mchungaji kuchochea moto wa mafarakano
Gwajima anasema walinzi wa Dr. Slaa ni walinzi wake, mpishi wa Dr. Slaa ni wa kwake. Kwa namna ya kujisifu, lakini Biblia takatifu inasema unapotoa kwa mkono wa kulia, mkono wa kushoto usijue. Ni mchungaji gani asiyeijua hata biblia kitabu kitakatifu anachotumia kuwafundishia waumini wake?
NEC ya CCM katika maamuzi yake Dodoma ilikata jina la Lowasa asigombee uraisi kwa tiketi CCM kwa sababu iliona ni mchafu. Ukawa, wakasema wao watamsafisha. Matokeo yake uchafu wa Lowasa umeanza kuwatafuna wana UKAWA tena kuanzia kwa viongozi wao wa kidini.
Harufu mbaya ya Lowasa imemrukia Gwajima, Dr. Slaa, Mbowe Tundu Lisu na itaendelea na wengine mpaka itakapowatafuna wote. Wanasaikolojia wanasema Akheri ukakaa kimya, watu watadhani unazo busara hata kama huna, kuliko kusema neno lisilofaa ukajianika ulivo mtupu kichwani.
Kirusi cha Lowasa anachoishi nacho kwa matumaini amekihamishia UKAWA