Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 1,658
- 4,866
Kitu pekee kinachofanya Makundi ya Palestina yaonekana ya Kigaidi hususani kwenye umoja wa mataifa na nchi za magharibi ni namna yanavyofanya mashambulio.
Kundi la Hamas lilipaswa kupiga kambi za jeshi na maneno yenye dhana za kijeshi ili kujiwekea uhalali wa kufanya mashambulizi. Kitendo cha Hamas kupiga risasi raia na kuwaua, na wengine kuteka nyara na mashambulizi mengine ya moja kwa moja kwa raia ni kosa la kigaidi, hivyo na kupelekea kundi hili kupewa jina la kigaidi.
Hotuba ya waziri mkuu wa uingereza amesema hawa jamaa sio freedom fighters au wapigania haki bali ni terrorists kutokana na matukio ya kushambulia raia. Nchi ya Marekani nayo imesema Hamas ni magaidi kutokana na namna wanavyoua raia.
Israel yeye katumia Akili sana hili asiitwe gaidi na maadui zake, badala yake wengi wanampongeza kwa kujitetea. Mfano, kabla hajafanya mashambulizi makubwa huko Gaza, aliwaonya na kutoa taarifa kwa raia yeyote aliyeko Gaza kuama eneo hilo, yani hakutaka kufanya mashambulizi ya moja kwa moja kwa Raia, jambo ambalo wengi wanaona ni la kiungwana kwa sababu vita ya Israel anapigana na Hamas na si raia wa palestina. Tofauti na kundi la Hamas ambalo lenyewe linalenga moja kwa moja raia.
Popote pale Duniani uwezi kupata support ya 100% kama unapiga raia moja kwa moja, ndio maana hata nchi za uarabuni zinashindwa kuingilia vita kwa sababu za Hamas kupiga moja kwa moja raia ambayo ni kinyume na sheria za Dunia.
USHAURI: Hamas kuishinda Israel mnapaswa kutumia Akili na si kupiga piga hovyo na kuwateka raia, mkifanya hivyo mtafanya mataifa mengine yazidi kuiunga mkono Israel na mwisho wa siku Israel itazidi kuwa na nguvu zaidi na ushawishi. Ikumbukwe nchi ya Israel inaruhusu uraia pacha, hivyo raia wa Israel wengi mnaowaua na kuwateka pia ni raia wa nchi nyingine, hivyo mtakuwa mnazipa morali nchi nyingine nazo kuiunga mkono Israel. Mfano raia wa Tanzania wawili hawajulikani walipo, hiyo ni go ahead moja kwa moja ya Tanzania kuiunga mkono Israel kwa sababu Hamas wameteka au kuua watanzania, japo Bongo nyoso haiwezi kutoa kauli. Hivyo hivyo nchi nyingine nazo mkiua raia wake. Israel hapa alijitoa kwenye kuua raia, yeye hasa hasa anatungua magorofa matupu yani safisha mji na kambi za Hamas tu, jambo linalompa mashiko.
Kundi la Hamas lilipaswa kupiga kambi za jeshi na maneno yenye dhana za kijeshi ili kujiwekea uhalali wa kufanya mashambulizi. Kitendo cha Hamas kupiga risasi raia na kuwaua, na wengine kuteka nyara na mashambulizi mengine ya moja kwa moja kwa raia ni kosa la kigaidi, hivyo na kupelekea kundi hili kupewa jina la kigaidi.
Hotuba ya waziri mkuu wa uingereza amesema hawa jamaa sio freedom fighters au wapigania haki bali ni terrorists kutokana na matukio ya kushambulia raia. Nchi ya Marekani nayo imesema Hamas ni magaidi kutokana na namna wanavyoua raia.
Israel yeye katumia Akili sana hili asiitwe gaidi na maadui zake, badala yake wengi wanampongeza kwa kujitetea. Mfano, kabla hajafanya mashambulizi makubwa huko Gaza, aliwaonya na kutoa taarifa kwa raia yeyote aliyeko Gaza kuama eneo hilo, yani hakutaka kufanya mashambulizi ya moja kwa moja kwa Raia, jambo ambalo wengi wanaona ni la kiungwana kwa sababu vita ya Israel anapigana na Hamas na si raia wa palestina. Tofauti na kundi la Hamas ambalo lenyewe linalenga moja kwa moja raia.
Popote pale Duniani uwezi kupata support ya 100% kama unapiga raia moja kwa moja, ndio maana hata nchi za uarabuni zinashindwa kuingilia vita kwa sababu za Hamas kupiga moja kwa moja raia ambayo ni kinyume na sheria za Dunia.
USHAURI: Hamas kuishinda Israel mnapaswa kutumia Akili na si kupiga piga hovyo na kuwateka raia, mkifanya hivyo mtafanya mataifa mengine yazidi kuiunga mkono Israel na mwisho wa siku Israel itazidi kuwa na nguvu zaidi na ushawishi. Ikumbukwe nchi ya Israel inaruhusu uraia pacha, hivyo raia wa Israel wengi mnaowaua na kuwateka pia ni raia wa nchi nyingine, hivyo mtakuwa mnazipa morali nchi nyingine nazo kuiunga mkono Israel. Mfano raia wa Tanzania wawili hawajulikani walipo, hiyo ni go ahead moja kwa moja ya Tanzania kuiunga mkono Israel kwa sababu Hamas wameteka au kuua watanzania, japo Bongo nyoso haiwezi kutoa kauli. Hivyo hivyo nchi nyingine nazo mkiua raia wake. Israel hapa alijitoa kwenye kuua raia, yeye hasa hasa anatungua magorofa matupu yani safisha mji na kambi za Hamas tu, jambo linalompa mashiko.