Hamad Rashid vs Freeman Mbowe=mt kilimanjaro vs kichuguu

huwezi kuolewa na upingane na mumeo, hapo ndoa haipo. Cuf bara haipo
 
Mbowe ni tatizo kubwa kwa Chadema. Huyu jamaa ni CORRUPT sana. Kama Chadema wataendelea majukumu makubwa ya chama, basi kuna hatari Chadema kitakuwa kama NCCR, au TLP.
 
...Wana JF lazima tukumbuke falsafa ya "vita vya panzi furaha ya kunguru". Hakuna haja ya Mbowe (Freeman) wa CHADEMA na Rashid (Hamad) wa CUF kuanzisha mapambano ambayo mwishowe watakayefaidika ni CCM. Mdahalo umeshafanyika, na matokeo yake yasiwe kama mchezo wa "kutupiana lawama = blame game". Nadhani ni wakati muafaka wapinzani (wa kweli) kufikiria ya kesho kwa kuwa "we cannot reverse the past but we can learn from it".



Mbowe na Hamad watakaposhutumiana na kupoteza muelekeo wa kisiasa katika kuleta mujtamaa na muafaka murua wa upinzani hatima yake ni kuuwa moyo wa kuendeleza mapambano dhidi ya kupatikana kwa demokrasi halisi. Wapinzani wote: CHADEMA, CUF, TLP, NCCR - Mageuzi, na UDP wenye wabunge wafanye yafuatayo:
  1. Waungane, waache tofauti zao - kwa vile tofauti zao zitainemeesha CCM;
  2. Wasimamie majukumu yao ndani ya BUNGE kama timu moja kwa mujibu wa ahadi zao walizozitoa kwa wananchi;
  3. Wapiganie kupatikana KATIBA MPYA;
  4. Wapige vita aina zote za ufisadi wa kimfumo na wa ndani ya mfumo; na
  5. Waunde upinzani imara bila ya kuathiri mujtamaa wa maendeleo vyama vyao.
Kama vyama vya siasa vilivyopo kwenye upinzani vikitaka kupoteza muelekeo wa kisiasa basi havina sababu ya kuuendeleza mpasuko uliyopo. Mpasuko uliyopo utatoa fursa kwa CCM kutumia nyufa zilizopo na kuvibomoa kwa urahisi kwa vile vyama vinaundwa na watu na watu hao ndiyo haohao wanaoweza kutumika katika kuleta sintofahamu na songombingo za kisiasa.

CHADEMA na CUF kama vyama makini wana wajibu na ni haki kukaa chini kutafakari hatma ya upinzani badala ya kutupiana lawama. TAHADHARI: Chadema na CUF wasipofanya hivyo kuna kila sababu ya kupoteza uwakilishi wao kwa umma na hii itakuwa hatari kwao kwa kuwa watapoteza uungwaji mkono kwenye mapambano dhidi ya ufisadi wa kimfumo na wa ndani ya mfumo unaofanywa na CCM.
 
Huu mdahalo niliupinga kwa sababu CDM na CUF wangeweza kumalizana wenyewe. Lakini kama matokeo ya mdahalo ni kuwaleta pamoja na kutoa hofu zao, basi huu mdahalo utakua na tija.

Mimi nilivyoona, Mbowe ameshindwa katika huu mdahalo....Rashid anaongea kwa mifano na ameonyesha anauzoefu mkubwa kuliko Mbowe...anayebisha na abaki kubisha.

Wakifanikiwa kuunda mpinzani na vyama vingine, kuna umuhimu wa kuwa na kiongozi wa upinzani mwenye uzoefu na upeo mkubwa kuliko Mbowe.

1) Mbowe anasema ni vita vya kila mtanzania lakini kwenye bunge amewabagua vyama vingine vya upinzani based on speculations.

2) Mbowe anajaribu kuonyesha kuwa CUF sio chama cha upinzani kwa sababu wameunda serikali ya pamoja na CCM znz

3) Rashid anampa shule Mbowe na anaonyesha vile vyama vya upinzani vinaweza kuunda serikali ya pamoja bila kuwa na matatizo...ametoa mfano wa uingereza. Amejibu speculation za Mbowe za kwa sababu CUF wameunda serikali na CCM zanzibar basi sio wapinzani tena

4) Mbowe anaongelia katiba ambayo kila mtu anajua ina takiwa kufanyiwa marekebisho...Rashid anasema kulilia katiba hakujaanza leo...Mowe anakubaliana naye.

5) Rashid anatoa msimamo kuwa yuko tayari kuunda kambi ya upinzani bila kubagua...Mbowe hoi!

6) Rashid anaonyesha unafiki wa Mbowe kuwa aliongea naye kuhusu kuunda kambi ya upinzani lakini akijua kuwa anatatizo la CUF kuunda serikali ya pamoja zanzibar...Mbowe hana jibu!
 
Tuangalie kwa mtazamo wa taifa zaidi,chadema imejikita bara na imespread maeneo tofauti imepata wabunge huku ccm ikichukua sehemu kubwa zaidi,CUF ZNZ tena Pemba tu,ccm Unguja.sasa nafikiri CUF itazamwe kama ya upande fulani ambao imepata umaarufu wa mkumbo mkumbo tu.Ni kweli wapemba wengi kwa akili zao na fikra huru wamekubaliana na mustakabali wa CUF?au Unguja wengi wao CCM? Je hapa haitupi mashaka kidogo kuwa kinachopiganiwa ZNZ sio siasa tunazozijua bali ni ushindani wa makundi kwa itikadi wa sehemu wanazotoka na si itikadi za vyama kwa maendeleo ya taifa kwa ujumla?ukiwasikiliza CUF na CDM vizuri katika swala la kuunda kambi ya upinzani bungeni,kama unapendelea upinzani ueendelee kukua sidhani kama utakubaliana na CDM kuishirikisha CUF achilia vyama vingine ambavyo vilishaonyesha wazi kuegemea upande wa ccm.

Kwa vile maamuzi ya muungano wa upinzani bungeni ni wa hiari kwa CDM kuwashirikisha wengine tuwaache waamue kwa utashi wao,na CUF wasilalamike kwani CDM wanayo haki ya kisheria na wao CUF hawawezi kuidai popote nafasi hiyo.Wasubiri uchaguzi ujao kama watabahatika tena kuipata nafasi hiyo.

mkuu,baada ya 1/11/2 010 niliweka thread hapa kuionya chadema isiungane na vyama mamluki wakidhani ni wapinzani wakatokea wabishi wakasema mimi ni mbinafsi na mchokozi,hata nilipoeleza hawakutaka kusikia. Bahati nzuri chadema wakaenenda vivo ivo kwa kuwaengua cuf ambayo ni nusu upinzani na nusu serikali! Kwa watu makini wataelewa kuwa wapinzan wengine ni mamluki. Chadema naiomba tena,isikubali makubaliano na cuf,tofauti na hapo watawavuruga!
 
Mbowe ni mtoto mdogo tu katika historia ya Zanzibar
Chadema musitulilie sisi bali lilieni na bunge la tanzania ambalo limewakosesha haki zenu za kupiga kura,na haki nyengine za msingi,sisi zanzibar tunalilia na baradha letu la wawakilishi kwani ndio lenye maamuzi yote wakisema tuitishe kura ya maoni juu ya muungano tukisema noo basi tumeuvunja,tukisema serikali tatu basi tutahakikisha serikali tatu zimekuwa au tumevunjaa muungano.

unahaibisha ID, che guevara? Sasa umeandika nini kwenye mchango wako juu? Sijui kama na wee unajielewa!
 
Tafuta magazeti mengine zaidi ya MwanaHalisi halafu ndiyo utajua kuwa CUF ina wabunge kutoka mikoa gani kabla ya kuandika madai ya utumbo ya hapo juu. Umefunga milango ya akili yako ndiyo maana ufahamu wako wa mambo ya siasa yamejifunga kiasi cha kutoa madai ya utumbo!

ina wabunge kutoka pwani,lindi, mtwara na zanzibar,yani pwani na visiwani tu! Ambapo 99.56% ni wabunge wa dini moja tu!
 
huu mdahalo mimi nimeufatilia toka mwanzo mpka mwisho tuweweke ushabiki mbali kabisa kumsimamisha mbowe katika mdahalo ule ilikua haifi kabisa kwa sababu zifuatazo moja mbowe miaka mitano iliyoisha hakuwepo bungeni na maswali mengi yaliyoulzwa pale yalikua yanahusu ushiriki wa upinzani bungeni na mikakati waliyotoka nayo huko nyuma yaaani bunge lililopita pili mbowe hana ukongwe wa historia ya siasa kiasi cha kuweza kujibu hoja ipasavyo tofauti na hawa waliowahi kukaaaa serikalilini muda mrefu ndio maana alikua anatoka nje ya swali muda mwingi sana, tatu alitakiwa pembeni akae na mtu kama zitto au halima mdee aliyekuwepo bungeni mwongo uliopita siyo tundu lissu hana jipya ni kama mbowe tu.
 
Nilifuatilia kwa makini saana mdahalo ulowakutanisha mbunge wa wawi mh hamad rashid kiongozi wa kambi ya upinzani isiyo rasmi na mbunge wa hai mh freeman mbowe ambaya ni kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni.Ukiacha ushabiki wa vyana Hamad Rashid alionesha uelewa mkubwa mno wa kile alichokuwa akikieleza zaidi ya mwenzake mbowe ambaye alikuwa akizungumza hoja ambazo hakuelewa nini msingi wake au amelishwa.Ni kama mtu aliyekaririshwa halafu akakuta kitu tofauti.Hamad alijibu maswali kitaalamu na kiufundi ambapo mbowe alikuwa akilalamikia cuf juu ya katiba(kama vile wameiweka wao) na kuuliza maswali ya jf yasiyo na kichwa wala miguu.Hakuonesha umakini ila udhaifu na kiasi cha kuzua naswali mengi namna kambi ya upinzaji chini ya uongozi wake hali itakuwaje.
Ukweli mbowe siasa bado,aendelee kujifunza kwa wanasiasa wakongwe.
Mdahalo umeonyesha Hamad Rashid usiku ule alikuwa kama mlima kilimanjaro na freeman mbowe kama kichuguu,kiasi ilimfanya mwenyekiti wa mdahalo awe anaingilia kati kumnusuru mbowe kiasi kilichopelekea mashabiki wa cuf waingilie kati kiasi cha kutaka kupelekea mdahalo uvunjike.
Ilikuwa kama watu walioandaa mechi katika uwanja wao,refa wao,kikombe chao, mwisho wanapigwa mabao na wanabaki na mshangao.
ni mtazamo tu

Ushauri wangu kwa CDM ni kuwa wasihangaike na vyama vingine vya upinzani. Mimi Kama mwananchi najua kati ya vyama vyote ni chama gani kipo kwa maslahi ya sisi wananchi. NCCR, UDP, na TLP tunavijua kabla na baada ya uchaguzi. Ndio maana husikii viongozi wa vyama hivyo wakitoa matamko kuipinga CCM kikweli kweli. CUF ngome yao ni Zanzibar, huku Bara wameshindwa kukubalika toka 1995 na ndio maana kwa muda wote huo imekuwa kupata nafasi za ubunge huku bara ni kazi nzito saana. Chadema ni wananchi ndio waliokupeni nguvu ya kuwa na wabunge wengi safari hii toka watano wa 2005 hadi 25 2010, idadi ambayo kwa mujibu wa katiba inatosha kuifanya CDM iunde kambi ya upinzani bla kumshirikisha NCCR, CUF, UDP or TLP. Kama ilivyo kwa CCM katiba inawapa haki ya kuunda serikali bila kushirikisha vyama vingine. Iwapo katiba inawapa haki CCM kuunda serikali bila ulazima wa kushirikisha vyama vingine, kwanini hatuoni ukweli huo unaotolewa na katiba kwa Chadema??? Na hasa ukizingatia hivyo vyama tunavyosema CDM iungane navyo kuunda upinzani???. Sote tumemsikia Mrema wa TLP akisema wazi kuwa haoni kiongozi kama JK, je huyu kweli inafaa uungane naye??? Kwa kumfurahisha nani??? Chadema nawaomba muwe makini saana, kama katiba inawaruhusu kuunda kambi ya upinzani bila kuungana na vyama vingine, ningeomba muendelee na kuunda kambi hiyo bila kuwashirikisha wengine. Fanyeni hilo kwa lengo la kujiandaa kushika serikali hapo 2015. Fanyeni hili baraza la mawaziri kivuli mtakao wapanga kama tuition ya mzigo kamili wa kuendesha serikali hapo 2015. Achaneni na CUF, TLP, NCCR, na UDP. Kama ambavyo wananchi wamewapa majimbo mengi mwaka huu 2010, basi mkiifanya vizuri kazi yenu kama upinzani katika bunge na hasa mkijipambanua vizuri nini mnachokisimamia kwa ufanisi wa wananchi basi tegemeeni 2015 mtapata uongozi wa nchi. Chagueni ajenda chache mzisimamie bungeni na ikishindikane mzilete kwa wananchi. Chukueni ajenda kam Katiba mpyaa, Tume huru ya uchaguzi, na Mgombea binafsi. Ni hoja chungu saana kwa serikali hivyo uwezekano wa kuzipinga bungeni ni mkubwa, na ninyi mkizileta kwa wananchi zitakuwa ndio daraja ya kuwaingiza kwa idadi kubwa bungeni 2015.
Nawakilisha
 
Ukweli siku zote UTABAKIA KUWA UKWELI... Na USHABIKI SIKU ZOTE UTABAKI KUWAUMIZA NYOYO WENYE NAO! Ijulikane wazi Tanzania itabaki kuwa Tanzania na Watanzania wake.
 
Hakuna haja ya kuungana na CUF, wengi wa wabunge wanatoka Pemba, hawana cha kupoteza mjengoni Dodoma, siasa zao wafanyie Baraza la mapinduzi zanzibar, wabunge wachache wa chadema waliwasha moto kwenye bunge lililopita, endelezeni moto ule ule, Huyu HR aliongea kwa hasira sijui alikuwa anatishia nyau!!, just ignore them.. endeleeni na kazi
 
Kwa ujumla wake nilifuatilia kwa makini sana mdahalo ule....lakini Hamad Rashid ambaye siku zote amekuwa akionekana ndiye mhimili mkubwa wa CUF Katika Kujenga hoja zenye mashiko siku ile alikuwa kama amepagawa na hakuwa kama HR ninayemfahamu ingawa baadae yaani mwishoni mwa mdahalo alionekana kurudi taratibu ktk hali yake ya kawaida yafuatayo ndiyo yaliyompa HR Hard Time katika kujieleza:-
1.CUF imeloose sana popularity hususani Tanzania bara.
2.Wananchi wengi hawafurahishwi na kinachofanywa na cuf ktk kipindi kifupi tu cha bunge lililopita kwa kupigia kura wagombea wa ccm katika wakilishi mbalimbali bungeni na hata kitendo cha H.Mnyaaa kujitoa dk za mwisho ktk kugombea nafasi ya unaibu speaker ili apate kura za ccm ktk uwakilishi wa SADC
3.Wanachama wengi wa CUF hususani vijana wa bara hawapendezwi na jinsi wanavyoburuzwa na wapemba kama yeye na kulaani kitendo cha wabunge wa CDM Kutoka nje wakati wao pia wengi wana makovu ya uchaguzi mpaka leo mfano Temeke, Tandika, Buguruni, Lindi, Tanga Mjini nk
Ndiyo maana mdahalo mzima ulimuelemea na kufikia kuongea vitu vya uongo kama eti baadhi ya wabunge wa CDM hawakutoka bungeni na pia kwamba eti CDM haikuwashirikisha vyama vingine vya upinzani ktk kuunda kambi ya upinzani bungeni kitu ambacho F.Mbowe alikikanusha palepale kwamba walim-approach Mrema na bahati mbaya Memose Cheyo alikuwa keshasafiri.
Kwa ujumla wake wote waliongea vizuri japo HR alionekana kuelemewa mno na jazba pamoja na uzushi
 
Haya wanachadema, tusijekimbiana humu, kuna watu wamekimbia humu baada ya uchaguzi huu huu wa juzi!!! be realistic, think twice, stay focused, think about nation, forget about udini na ukabila, au kubaguana kwa hali yoyote, ishi na adui yako kwa akili!!! CDM common wake up!!! tumewachoka sasa!!
 
Nilijua wanaccm humu jf watasema ninayo yasikia lakini ukweli ni kwamba mbowe alimfunika vibaya mamuluki kwa point zifuatazo.
1. Kwa kanuni za bunge chadema inaruhusiwa kuunda kambi ya upinzani bila kutishwa wala kuingiliwa na mamluki yeyote
2. Kwa cuf kuwa nusu serikali nusu upinzani siyo rahisi kukurupuka kuwahusisha kwenye kambi ya upinzani
3. Cuf walisusia serikali ya zanzibar 1995, 2000, 2005 yet waliunda kambi ya upinzani anashangaa nini chadema kuunda
4. Kususia hotuba ya rais chadema hawajavunja kanuni yoyote ya bunge wala shria yoyete ya tanzania ila walicheza krata yao vizuri kuibua mjadala wa katiba mpya, na tume huru ambavyo cuf wameshindwa kuvitekeleza.
5. Ilikuwa aibu na uelewa mdogo kwa hamad kuleta mambo ya udini kwenye mdahalo eti niliongea na ndesamburo akaniambia eti cuf sisi wadin bullllllllllllshit hamadi
6. Inaonesha wazi kuwa hamadi ameumia million 200 alizokuwa akipatiwa kama kiongozi bungeni
7. Hamadi alishindwa kufafanua ikiwa cuf inalenga serikali ya umoja wa kitaifa mbona hawajashirikisha vyama vyote zanzibar katika ndoa yao?
8.hamadi alishindwa kufafanua atawezaje kuwa mpinzani wakati yeye ni sehem ya serikali
9. Hamdi amaeshindwa kuelewa kuwa mabadiliko ndani ya bunge hayawezikani bila pressure ya umma nje ya bunge -kwakuwa ndani ccm imejaza mbumbumbu wapiga makofi
10. Kwa ujumla mbowe was cool and hamdi alikuwa na hasira saana hadi pale walipoitwa ccm wakataka kupiga ngumi
hongera rosemary mwakitwange

Mkuu umesema sawa sawa na kwa kweli ulifuatilia mdahalo ule vizuri kama mimi. Inaoneka cuf walikuja kwa vita, ndiyo maana hata Hamad alipandwa na hasira, halafu mashabiki wao pia nao wakapandwa na hasira. Mimi nilishangaa sana. Jambo la uhakika ni kuwa cuf haiwezi kuwa chama cha upinzani huku bara tena.

Kwanza bunge la muungano kimsingi linajadili mambo ya bara kwa kiasi kikubwa, sasa wao wanatoka Pemba karibu wote, lini watakuwa na uchungu na mambo yetu ya bara? Mimi napendekeza Chadema wawapuuze kabisa kabisa sisi tuangalie tu ukombozi wa Tanganyika yetu na wao waende tu visiwani wwakawasaidie CCM kutawala.

Pilli wakubali wasikubali muafaka wao na CCM umewatupa nje ya upinzani kabisa, na ndiyo maana kwenye chaguzi ndani ya bunge wamewaunga mkono ccm kwa asilimia mia. Jamani tuwahurumie tu haiwezekani kabisa kuwa kinyume na ccm, wakikaa humo mjengoni wenyewe wanafikiri wako Zanzibar kwenye muafaka.

CHADEMA MWENDO MDUNDO WATANZANIA WANAWAANGALIA NYIE NA NYIE PEKE YENU KAMA VINARA WA MAPINDUZI YA KWELI.
 
kwenye ushabiki elimu haifui dafu ila ukweli rashidi alionyesha upeo kuliko freeman.......

alionyesha upeo gani, anajisifia kuua watu zanzbar, wameshirikishwa singo na ccm wanadhani albam ni yao. sera na ilani zinazotekelezwa na serikali ni za ccm cuf wamewachuuza wazenji wakafa, wanachofia madaraka kwa maalim seif. ovyoo!
 
Back
Top Bottom