Hamad Rashid: Hakuna haja ya Serikali tatu

Hamad Rashid: Hakuna haja ya Serikali tatu

Serikali ya Zanzibar wana bendera yao.. Wimbo wao wa taifa.. Raisi wa Zanzibar ana uwezo wa kugawanya mikoa na wilaya.. Watanganyika wana haki pungufu ya kumiliki ardhi Zanzibar ila Wazanzibar wana haki kamili ya kumiliki ardhi Tanganyika.. Na sasa wanataka wapatiwe haki yao ya kutambuliwa uraia wao.. Jeshi lao na kuwa na sarafu zao.. Halafu bado mnapigia upatu serikali mbili..??
 
Ukipanda UPEPO basi ujue utavuna DHORBA. Pole sana Ahali yangu Ba Hamad.

Masikini wee naona hadhi yako ilivyoporomoka kama Naila Jidawi.
 
Ana haki ya kikatiba kutoa maoni yake..au mnadhani nyinyi ndo mnahaki miliki yakutoa mawazo yenu??
Hakuna anayemkataza asitoe maoni yake. Elewa.

Tatizo ni kuwa haingii akilini kiongozi wa Zanzibar aje kutoa maoni ya kuwazuia Watanganyika wasiwe na serikali yao huku Wazanzibari wana ya kwao.

Tatizo jingine Wazanzibari anaowawakilisha zaidi ya asilimia 60 (kufuatana na tume ya Warioba) wanataka muungano wa mkataba, hapa tunamuona HR akiisaliti majority ya Wazanzibar wakati huohuo yeye Mzanzibari anataka kuwapangia asilimia 60 ya Watanganyika ambao wanaitaka Tanganyika yao!
 
Hivi kwanini tusitengane tuu
Wazazibar walishatishia sana wanataka Serikali yao hawataki MUUNGANO
Naomba huyu Mwneyekiti KIFICHO ndio awe Spika
na ili kiongezwe kipengele cha KUTENGANA
hakuna cha
  • Serikali 3
  • Serikali 2
  • Serikali 1
  • Tuuvunje Muungano
Russia ilishatengana
Yugoslavia
Ujerumani
Korea
leo Tanganyika na Zanzibar miaka 50 inatosha tujiunge na Rwanda au Burundi au Malawi
Haiwezekani kila mmoja akae kivyake maana ni kunyonyana kusiko na maana POSHO POSHO , vyeo UBUNGE UWAZIRI nk
 
Serikali tatu hazikwepeki! Tumesema hivyo kwenye rasimu ya katiba na ndivyo itakavyokuwa! PERIOD!
 
Pamoja na mijadala yote mwisho wa siku zitabaki serikali mbili. Hakuna aliye tayari kuona Tanzania inamfia mikononi mwake. Hiyo laana hakuna anayetaka kuibeba. Ufumbuzi ni kuondoa kero za muungano kwa ukweli na uwazi usio na mashaka yeyote.
 
Yeye mzanzibar anasema hivyo maana wao tayari wanaserekali yao sasa na sisi tunaitaka TANGANYIKA YETU no way. Huyo Hamad hajui sera ya chama chake?

Kama kuna mkulima humu jf anafahamu maana ya mmea wa kikonyo. Ni mmea ambao hauna shina la asili. Shina la mlimao linawekewa kikonyo cha mchungwa, kikiisha mea unauua mlimao unaacha mchungwa.
Ndio huu muungano wetu, mlipandikiza Zanziba sasa mnataka kuua Tanganyika?? Zenj wamekataa, hawataki kupandikizwa. Mche wenu ushakufa huo. Hamad ametambua hasara atakayoipata Muungano ukifa, Atapata wapi posho za bunge la JMT? Atayateteaje hayo mashamba yake na vitega uchumi vyake alivyo wekeza Bara? Hayo ndio yanawasumbua hao woote wanao tetea serekali 2 yaani mfumo huu tulio nao. Ati serekali 3 hazifai, ati uliona wapi, Nasema tumekuwa na hizo mbili na migogoro ikadumu, tuwe na 3 ili kila nchi iwe na mamlaka kamili. Kama si hivyo Zanziba waache choko zao za kutaka mamlaka kamili tuwe na serekali 1 tu ya JMT. Visiwani kuwe ni mkoa na wilaya zake 2
 
Hivi kwanini tusitengane tuu
Wazazibar walishatishia sana wanataka Serikali yao hawataki MUUNGANO
Naomba huyu Mwneyekiti KIFICHO ndio awe Spika
na ili kiongezwe kipengele cha KUTENGANA
hakuna cha
  • Serikali 3
  • Serikali 2
  • Serikali 1
  • Tuuvunje Muungano
Russia ilishatengana
Yugoslavia
Ujerumani
Korea
leo Tanganyika na Zanzibar miaka 50 inatosha tujiunge na Rwanda au Burundi au Malawi
Haiwezekani kila mmoja akae kivyake maana ni kunyonyana kusiko na maana POSHO POSHO , vyeo UBUNGE UWAZIRI nk

Tuungane na mama wa jirani mkuu.
 
Tangu lini mahakama imekuwa adui? Una maana mahakama imesema asiseme? Mahakama si ndicho chombo kinacho tafsiri sheria, ulitakama useme wewe? Yeye katoa maoni yake na wewe toa maoni yako. Kama huna kaa kimya, nani kakuzuia kusema?
Mbunge wa mahakama nae aseme nini?
 
Tujaribu miaka mingine hamsini ikiwa na serikali mbili ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya watu Tanganyika ili na Watanganyika waone machungu ya muungano.
 
Wabunge wote wa mahakama ni wabunge wa ccm coz wameisaidia kuleta migogoro
ndani ya vyama vya upinzani,binafsi sitegemei mbunge yeyote wa mahakama aende kinyume na matakwa ya ccm.
 
Kama tuna nia ya dhati ya kuwaunganisha watanzania twende kwenye serikali 1 ya JMT
 
Nchi duniani kote zinatafuta kuungana na sio kutengana.Tufikirie zaidi muungano wa serikali 1.
 
Watu wote wenye akili ya kuweza kupata A+ watakuja na jibu kama lako, na wale wanaoweza kujikongoja na kupata D ndio mashabiki wakuu wa serikali mbili. Wa serikali tatu ndio wamo katikati ya hizi marks mbili. Mwenye akili na aelewe tuliposimama!


Kukata mzizi wa fitina tuwe na serikali moja tu
 
Niliwahi kusema mara nyingi, wazanzibar hawajui wanataka nini nikaambiwa nimewakashfu.
Mwenyezi mungu ananitetea kila uchao na hii ni moja ya utetezi huo.

1. Hamad Rashid alikuwa kiongozi wa CUF.
CUF ndio wa kwanza kupeleka rasimu kwa maandamano wakitaka serikali 3
Sera za chama cha CUF chini ya Maalim seif ni serikali 3
Yote hayo yamefanyika Hamad akiona kwa macho yake na kushiriki vema tu.

2. Maalimu akiwa CUF anataka serikali 3. Akiwa na uamsho anataka mkataba.
Nani anajua Maalim anataka nini?

3. Shamsa Vuai alisema muungano ni 2. Baada ya kuvuliwa uwaziri akarudi kusema anataka mamlaka kamili
Nani anajua anasimamia nini?

4. Wznz wanasema muungano hauna faida kwao. Wakimaliza hapo wanataka muungano wa mkataba.Ebo kama muungano hauna faida mkataba wa nini? Wanajua wanataka nini kweli.

5. Wznz wanasema hawataki muungano. Tume ilipoundwa wakasema wanataka uwakilishi nusu kwa nusu. Tume imetoa mapendekezo wanasema hawataki wanataka serikali 2.
Wanajua wanachokitaka hawa watu kweli?

6. Wznz wanasema muungano ni ushetani mkubwa na ulaaniwe. Majina ya wabunge wa kuteuliwa yalipotangazwa wakataka waongezwe zaidi kuja Dodoma na si kukataa kuja Dodoma.
Hivi tunapoandika wapo Dodoma wanajadili muungano ule wanaousema laanatulah, wamekaa kitako raha mstarehe. Wakipanda meli na kuteremka malindi povu linaziba pua na mdomo, hawataki muungano. Hivi wanajua wanataka nini hawa watu?
 
Wazanzibar wanachekesha!
Wao tayari wana serikali yao,
i wapi Tanganyika yetu?
 
Wazanzibar wanachekesha!
Wao tayari wana serikali yao,
i wapi Tanganyika yetu?
Hawapo Dodoma kwa minajili ya katiba! la hasha, wapo Dodoma wakiwa na fomu za kugawana madaraka na nafasi za ubalozi baasi. Vifungu hivyo vikipitisha in their favor wapo tayari bunge liahirishwe.
Kwao fomu za kazi, madaraka na nafasi wanazolilia sana za ubalozi ndizo muhimu.
 
Typing error hiyo.....

Hivi nyie mbona hamueleweki? Uchaguzi wa udiwani mmeangukia pua Leo mmnaidaka hoja ya serikali tatu vipi nyie?

Mtaweza? Chama kimebomoka mnapumulia MASHINE halafu mnataka makubwa mtayapata wapi?

poor CDM

Hivi ukitaka serikali 3 ni lazima uwe CDM, kama ni hivyo CDM inatuwakilisha watanganyika wengi sana tuliochoka kero,malalamiko na masimango ya Wazanzibar, tunao wabeba lkn hawabebeki.
 
Rashid tunajua msimamo wenu kama chama upande wa tanganyika ni serikali mbili ila bosi wenu katibu seif anataka serikali tatu na hata kwenye vikao vyenu vya siri mambo yako wazi mnataka serikali mbili
 
Hivi ukitaka serikali 3 ni lazima uwe CDM, kama ni hivyo CDM inatuwakilisha watanganyika wengi sana tuliochoka kero,malalamiko na masimango ya Wazanzibar, tunao wabeba lkn hawabebeki.

Wanaotaka serikali Tatu ni Watanzania 61% kutoka vyama vyote na wasio na vyama pia. Hiyo misimamo ya vyama kama kila Mtanzania angeachwa huru bila sijui huu ni msimamo wa chama mara ikaenda ikarudi, tungepata ukweli, lakini ngazi za juu za vyama au chama kinapotoa msimamo, mawazo huru yanakuwa yameminywa.
 
Back
Top Bottom