Hamad Rashid: Hakuna haja ya Serikali tatu

Hamad Rashid: Hakuna haja ya Serikali tatu

Katika kipindi cha jambo tanzania leo tbc one amesema hakuna haja ya serikali 3 kikubwa kutatua kero za muungano,maana hatuna uzoefu wa serikali 3 popote duniani
akili yake imechoka kufikiri kabisa, hizo kero za muungano anazodai zitatuliwe, ni miaka mingi imepita zimeshindikana kutatuliwa ila zinaongezeka, huko ni kuchoka kufikiri
 
Watanzania, tuliishasema, hutu tuvyama twa upinzani tunatoanzishwa ni matawi ya ccm, Hamad Rashidi kaanzisha ADC kwa mgongo wa ccm, baada ya kuigawanya cuf, unategemea atakuwa kinyume na ujinga wa ccm tena akiwa TBC redio yao, kuna katawi kengine ka ccm kameanzishwa kanaitwa ka ACT, ka huyu dogo msaliti Zitto na doctor asiyejielewa Kitila, unafikiri kana msaada gani kwa watanzania zaidi ya kuwagawa watu kutoka Chadema, ili ccm iendelee kupeta, it is too late, watanzania wameelika na wanaendelea kuelimishwa, dhambi ya usaliti itawatafuna sana, ukiisaliti Chadema, umewasaliti watanzania.
 
Tangazeni Kaskazini yenu, LYIMO mbona mnatupotezea muda?
TataMadiba nyie ndiyo msiotutaka kwa sababu zenu mnazozijua, hivyo nyie ndiyo mnaopaswa KUJITENGA. Mmpendikiza CHUKI juu yetu bila ya sababu, sasa CHUKI hii na DHAMBI ya UBAGUZI haita waacha salama. Leo mnatuhukumu kwa majina yetu ndani ya nchi yetu, mkimaliza hapo mtaanza kujitafuta na nyinyi mliyotenda DHAMBI hii.
 
Tatizo mnafikiri Serikali 3 hazitakuwa na Kero! EAC yenye Serikali 5 tayari kuna kero za kufa mtu!

Hakuna kitu kisicho kuwa na kero duniani.Cha msingi tunataka Tanganyika irudi na serekali yake ili tuendelee kupambana na kero za Tanganyika kuliko kuendelea kushughulika na kero kama za akina Rashidi.
 
Uko kwenye Muungano wa Tanganyika na Zanzibar! Ni afadhali Shetani unayemjua kuliko Malaika usiyemjua!



Usingemjibu mkuu

hao watu hawawezi kufikiri mpaka wafikirishwe na akina Slaa
 
Katika kipindi cha jambo tanzania leo tbc one amesema hakuna haja ya serikali 3 kikubwa kutatua kero za muungano,maana hatuna uzoefu wa serikali 3 popote duniani

Sawa, ila ya Tanganyika lazima irudi. Sasa baada ya hapo kama itakuwa moja sawa,lakini ya TanganYika ikiwepo. Kuwepo kwa Serikali ya Tanganika hakuepukiki, sasa kama ni mbili ya Tanganyika na Muungano sawa, Ya Tanganyika na Zanyibar sawa, ila ya Tanganyika irudi, yaani katika hizo 2 au 3 ya Tanganika iwepo, kama serikali moja Watanganyika tuko tayari kuipokea, lakini zikizidi 2 tu, ya Tanganyika lazima, hatudanganyiki tena, na tumechoka na Kelele zisizoisha eti tunawanyonya. Mh M. Rashid uelewe hilo!
 
Wapemba mliomchagua huyu jamaa kuwawakilisha bungeni jueni sasa kuwa hayawakilishi maoni yenu!

Viongozi wa Zanzibar wajikite kwenye kuwakilisha madai ya wananchi wao, ya Tanganyika waachiwe Watanganyika wenyewe.
 
hakuna cha kutatulika kwa kero yoyote ya muungano kwani tumekuwa nazo enzi hadi enzi hivyo umuhimu wa kuwa na serikali 3 ni mkubwa zaidi kwani chanzo ni huku kwetu tunakandamizwa ile mbaya sana
hivyo serilkali 3 lazima iwepo watake wasitake lazima ............... itoke hapa tz
Katika kipindi cha jambo tanzania leo tbc one amesema hakuna haja ya serikali 3 kikubwa kutatua kero za muungano,maana hatuna uzoefu wa serikali 3 popote duniani
 
Mlezi wa ADC (chama cha msimu) ana bwebwe,, uzoefu wa serikali mbili na mazuri ya serikali mbili ni yapi???
 
Hamadi Rashid ni kibaraka wa CCM ndani ya CUF anahaha lakini ndio kushneyi .
 
Naunga mkono hoja...huwezi kukimbia kutatua kero za sasa za muungano kwakutengeneza kero mpya za serikali 3...!!
 
Wananchi walishatoa maoni yao sasa ole wa wabunge wakabadilishe!. Manake nasikia kila mtu anaropoka tu huku nje.
 
Ana haki ya kikatiba kutoa maoni yake..au mnadhani nyinyi ndo mnahaki miliki yakutoa mawazo yenu??
 
Katika kipindi cha jambo tanzania leo tbc one amesema hakuna haja ya serikali 3 kikubwa kutatua kero za muungano,maana hatuna uzoefu wa serikali 3 popote duniani

Sio tu kwamba hakuna haja ya serikali 3; lets call a spade a spade NOT a big spoon!! hakuna haja kabisa ya muungano kama huu wa kuendekeza Wazanzibari kwa kuwapuuza Wazanzibara!

Jambo kubwa hapa la maana na la msingi ni Kurudisha nchi na serikali yetu ya Tanganyika kwenye ramani ya dunia; Tanganyika itoke kwenye pazia, Tanganyika itoke mvunguni mwa kitanda!!
 
Wazanzibar walikua wanabeep kwa fujo sasa tunawapigia hawataki kupokea...serikali 3 ndo tunayoitaka
kama 3 haifai bac usiwepo kabisa tanganyika isimame yenyewe na zanzbar kivyake tuungane kma east africa bc
 
Wadau changieni sana hoja hii mpaka tujue ukweli upoje?
 
Sifa za wale wa serikali tatu:
1. Awe mfuasi na mwanachama wa CHADEMA
2. Awe anatoka kaskazini
3. Awe anapenda Madaraka
Njeru Kasaka na G55 wote walitoka Kaskazini!?
Sina uhakika kama kweli unajua kuwa huu ni mjadala wa muhimu kwa mustakabali wa nchi hii na wengine wanaenda mbele na kudai kuwa umasikini uliokithiri kwenye nchii hii tajiri ni sababu ya mfumo wa utawala unaozuia watu kutoa mawazo yao kwa uhalisia wake na moja ya sababu ikiwa ni 'kulinda Muungano'.
Ndio maana inaonekana kuwa wanaopigania serikali moja ni watu wastahimilivu sana na wako tayari kutoa maisha yao kuiona nchi ikienda mbele huku wanaotaka serikali tatu ni wale waoamini katika mabadiliko endelevu ya binadamu bila ya kulazimishana - yaani kuacha hali halisi ichukue mkondo wake.
 
Back
Top Bottom