Hamad Rashid: Hakuna haja ya Serikali tatu

Hamad Rashid: Hakuna haja ya Serikali tatu

Magembejr

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2014
Posts
618
Reaction score
75
Katika kipindi cha Jambo Tanzania leo TBC1 amesema hakuna haja ya Serikali tatu.

Kikubwa kinachotakiwa ni kutatua kero za Muungano maana hakuna uzoefu wa Serikali tatu popote duniani
 
Katika kipindi cha jambo tanzania leo tbc one amesema hakuna haja ya serikali 3 kikubwa kutatua kero za muungano,maana hatuna uzoefu wa serikali 3 popote duniani
kero hazitatuliki zilee... Tumekuwanazo tangu day one ya muungano...
 
Hawa watu ni wehu, kila siku malalamiko yalikuwa Tanganyika imeifanya Zanzibar kuwa koloni lake sasa fursa ya kujitoa kwenye hilo koloni imepatikana , wanaanza mara ohh hakuna haja ya serikali tatu......wanaangaliaa Ubunge wao tu na wala sio masilahi ya Zanzibar hawa .......
 
Yeye kama mtu alierubuniwa kuigawa CUF sasa anataka kulipa fadhira miaka yote hamsini kero hizo zimeshindikana leo ndo zitaisha !!? Kwa kuwa yeye ni mzanzibar ningempongeza kama angependekeza seikali moja kuliko kuja na porojo zake hizo huyu mwanzilishi wa ADC.
 
Ni Watanganyika ndio wanaodai Tanganyika yao,yeye Mzanzibari yanamhusu nini?

Atajibu nini iwapo ataulizwa kuwa mbona nyinyi Wazanzibari mna nchi ndani ya muungano halafu hutaki Watanganyika wapate nchi yao?

Huyu anamsaidia Pengo bila ya kujijua.
 
Katika kipindi cha jambo tanzania leo tbc one amesema hakuna haja ya serikali 3 kikubwa kutatua kero za muungano,maana hatuna uzoefu wa serikali 3 popote duniani

Wajanja wote hawawezi kuunga mkono serikali tatu kwa dakika moja.
 
Katika kipindi cha jambo tanzania leo tbc one amesema hakuna haja ya serikali 3 kikubwa kutatua kero za muungano,maana hatuna uzoefu wa serikali 3 popote duniani

Kama 2 ziliwezekana kwanini 3 zisiwezekane??uzoefu wa serikali 2 upo wapi duniani?inakuwaje mtu anaongea kwa lengo la kufurahisha watu fulani?serikali 2 ni ulaghai wa ajabu!!nchi ndani ya nchi!!mipaka ndani ya nchi!!amiri jeshi wakuu wawili ndani ya nchi!!
Suruhisho hapa ni serikali moja
 
Hamad Rashid, nilifurahi sana baada ya CUF kuusafisha uchafu wake, ndio maana leo anarambaa yale matapishi yake, ila kama anahofia yale mashamba yake ya mizabibu kule Dodoma, sisi tunamwambia kwamb Wazanzibar katu hatutauza utu wetu kwa kujali kitu!!
 
Kama 2 ziliwezekana kwanini 3 zisiwezekane??uzoefu wa serikali 2 upo wapi duniani?inakuwaje mtu anaongea kwa lengo la kufurahisha watu fulani?serikali 2 ni ulaghai wa ajabu!!nchi ndani ya nchi!!mipaka ndani ya nchi!!amiri jeshi wakuu wawili ndani ya nchi!!
Suruhisho hapa ni serikali moja

google utapata historia ya serikali 2, serikali 3 ni majanga mkuu.
 
Yeye mzanzibar anasema hivyo maana wao tayari wanaserekali yao sasa na sisi tunaitaka TANGANYIKA YETU no way. Huyo Hamad hajui sera ya chama chake?
 
Hamad Rashid, nilifurahi sana baada ya CUF kuusafisha uchafu wake, ndio maana leo anarambaa yale matapishi yake, ila kama anahofia yale mashamba yake ya mizabibu kule Dodoma, sisi tunamwambia kwamb Wazanzibar katu hatutauza utu wetu kwa kujali kitu!!

wewe ni Mzanzibari unayeishi DODOMA?
 
Wazanzibar walikua wanabeep kwa fujo sasa tunawapigia hawataki kupokea...serikali 3 ndo tunayoitaka
 
Back
Top Bottom