Halotel rekebisheni lugha yenu kwenye matangazo yenu

Tyupa

JF-Expert Member
Aug 11, 2013
802
653
Badala ya kutumia Kiswahili fasaha Halotel hupenda kutumia kiswahili cha mtaani au cha Kizaramo kama hivi: HAUNA salio la kutosha.... badala ya kiswahili fasaha cha;HUNA salio la kutosha...Hauna hutumika kama vile; Muungano huu HAUNA faida kwa upande mwingine na huwezi kusema;Muungano huu HUNA faida kwa upande mwingine.Vyombo vya mawasiliano kama Tigo, Voda,Halotel nk ni kioo cha jamii katika nyanja ya taaluma.Na hawa Tigo nao wanao vilaza wa lugha kwenye vitengi vyao.Tigo huchapia sana kwa lugha ya Kizaramo pia.Wao hutumia "Ivi "hujui kama ....badala ya ; "HIVI " hujui kama....
 
Hizo ni inshu ndogo tu kwa sababu matangazo lazima yatumie lunganinayoeleweka na wengi,onayovutia ili watu wavute makini zao.
Hilo sio suala kubwa kiivyo/kihiivyo mkuu .Cha msingi tupambane GB 1 iwe jero wiki nzima au siku 2.
Ushawahi jiuliza mtu wa kibatani anapewa ofa ya GB 1 kwa jero wakati hata mb100 zinamshinda?Halafu wewe una smartphone unapewa mb300 kama ofa sasa sijui ni haki?anyway nimetoka nje ya mada byebye!
 
Back
Top Bottom