Kipenzi Changu
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 57,954
- 134,032
Kinachoendelea katika halmashauri zetu ni kitu cha hatari kabisa.Ukata wa hali ya juu,ukata wa kukwamisha kwa kiwango kikubwa utoaji wa huduma kwa wananchi.
Wadau kwa wale wasio na taarifa ni kwamba halmashauri zipo kwenye hali ngumu sana ya kukosa ruzuku ya kujiendesha na ruzuku za miradi ya maendeleo.Ukata huu umefanya baadhi ya halmashauri zisizo na mapato ya ndani ya kutosha kushindwa kutoa huduma kwa wananchi.Imefikia wakati idara inakosa hata rim papers za kuandika taarifa.
Halmashauri hazikopesheki tena kwa wazabuni,wazabuni wanashinda halmashauri kudai pesa zao.Halmashauri zinaua mitaji ya wafanyabiashara
Watumishi wamekataa tamaa wamepauka hawajui kesho yao,stahiki zao hawajui hatma kutwa kuhakikiwa mara vyeti vya vyuo,mara umri mara ndoa na kadi za benki. Gharama za maisha zimepanda mishahara haijapanda. Wanaishi kwa hofu ya kutumbuliwa.
Madiwani wanakaa vikao hawana mradi wa kujadili fedha hazijaletwa,fedha zinaletwa kwa matukio tu,na sio kwa mujibu wa bajeti. Wakurugenzi wanaogopa wamejaa uwoga wa kutumbuliwa,hawana ujasiri wa kukumbushia ruzuku.
Wabunge wetu mnafanya kazi gani?nyinyi ndio mawakala wetu kwa mawaziri na rais, mbona mko kimya?
Nyie wabunge vipi,mlishindwa kuzuia serikali kuu kupokonya vyanzo vya mapato ya ndani na bado mmekaa kimya tu.Hii sio dalili ya nchi kufilisika?
Wadau kwa wale wasio na taarifa ni kwamba halmashauri zipo kwenye hali ngumu sana ya kukosa ruzuku ya kujiendesha na ruzuku za miradi ya maendeleo.Ukata huu umefanya baadhi ya halmashauri zisizo na mapato ya ndani ya kutosha kushindwa kutoa huduma kwa wananchi.Imefikia wakati idara inakosa hata rim papers za kuandika taarifa.
Halmashauri hazikopesheki tena kwa wazabuni,wazabuni wanashinda halmashauri kudai pesa zao.Halmashauri zinaua mitaji ya wafanyabiashara
Watumishi wamekataa tamaa wamepauka hawajui kesho yao,stahiki zao hawajui hatma kutwa kuhakikiwa mara vyeti vya vyuo,mara umri mara ndoa na kadi za benki. Gharama za maisha zimepanda mishahara haijapanda. Wanaishi kwa hofu ya kutumbuliwa.
Madiwani wanakaa vikao hawana mradi wa kujadili fedha hazijaletwa,fedha zinaletwa kwa matukio tu,na sio kwa mujibu wa bajeti. Wakurugenzi wanaogopa wamejaa uwoga wa kutumbuliwa,hawana ujasiri wa kukumbushia ruzuku.
Wabunge wetu mnafanya kazi gani?nyinyi ndio mawakala wetu kwa mawaziri na rais, mbona mko kimya?
Nyie wabunge vipi,mlishindwa kuzuia serikali kuu kupokonya vyanzo vya mapato ya ndani na bado mmekaa kimya tu.Hii sio dalili ya nchi kufilisika?