Halmashauri zinakufa, Wabunge mko wapi

Halmashauri zinakufa, Wabunge mko wapi

Zife tu.Yaani kama kuna institutions ambazo sizipendi ni Halimashauri.Halimashauri hazisaidii lolote kwenye maendeleo ya wananchi,kinaendelea ni ubadhirifu tu wa fedha.Nadhani tunapaswa kuzi-overhaul kabisa na tuwe na kitu kingine mbadala.
Kinachoendelea katika halmashauri zetu ni kitu cha hatari kabisa.Ukata wa hali ya juu,ukata wa kukwamisha kwa kiwango kikubwa utoaji wa huduma kwa wananchi.

Wadau kwa wale wasio na taarifa ni kwamba halmashauri zipo kwenye hali ngumu sana ya kukosa ruzuku ya kujiendesha na ruzuku za miradi ya maendeleo.Ukata huu umefanya baadhi ya halmashauri zisizo na mapato ya ndani ya kutosha kushindwa kutoa huduma kwa wananchi.Imefikia wakati idara inakosa hata rim papers za kuandika taarifa.

Halmashauri hazikopesheki tena kwa wazabuni,wazabuni wanashinda halmashauri kudai pesa zao.Halmashauri zinaua mitaji ya wafanyabiashara

Watumishi wamekataa tamaa wamepauka hawajui kesho yao,stahiki zao hawajui hatma kutwa kuhakikiwa mara vyeti vya vyuo,mara umri mara ndoa na kadi za benki. Gharama za maisha zimepanda mishahara haijapanda. Wanaishi kwa hofu ya kutumbuliwa.

Madiwani wanakaa vikao hawana mradi wa kujadili fedha hazijaletwa,fedha zinaletwa kwa matukio tu,na sio kwa mujibu wa bajeti. Wakurugenzi wanaogopa wamejaa uwoga wa kutumbuliwa,hawana ujasiri wa kukumbushia ruzuku.
Wabunge wetu mnafanya kazi gani?nyinyi ndio mawakala wetu kwa mawaziri na rais, mbona mko kimya?

Nyie wabunge vipi,mlishindwa kuzuia serikali kuu kupokonya vyanzo vya mapato ya ndani na bado mmekaa kimya tu.Hii sio dalili ya nchi kufilisika?
 
Ni kweli kweli kabisa,na hii ni uteuzi wa makada.Na nchi itakuwa hoiiii muda si mrefu
 
Kinachoendelea katika halmashauri zetu ni kitu cha hatari kabisa.Ukata wa hali ya juu,ukata wa kukwamisha kwa kiwango kikubwa utoaji wa huduma kwa wananchi.

Wadau kwa wale wasio na taarifa ni kwamba halmashauri zipo kwenye hali ngumu sana ya kukosa ruzuku ya kujiendesha na ruzuku za miradi ya maendeleo.Ukata huu umefanya baadhi ya halmashauri zisizo na mapato ya ndani ya kutosha kushindwa kutoa huduma kwa wananchi.Imefikia wakati idara inakosa hata rim papers za kuandika taarifa.

Halmashauri hazikopesheki tena kwa wazabuni,wazabuni wanashinda halmashauri kudai pesa zao.Halmashauri zinaua mitaji ya wafanyabiashara

Watumishi wamekataa tamaa wamepauka hawajui kesho yao,stahiki zao hawajui hatma kutwa kuhakikiwa mara vyeti vya vyuo,mara umri mara ndoa na kadi za benki. Gharama za maisha zimepanda mishahara haijapanda. Wanaishi kwa hofu ya kutumbuliwa.

Madiwani wanakaa vikao hawana mradi wa kujadili fedha hazijaletwa,fedha zinaletwa kwa matukio tu,na sio kwa mujibu wa bajeti. Wakurugenzi wanaogopa wamejaa uwoga wa kutumbuliwa,hawana ujasiri wa kukumbushia ruzuku.
Wabunge wetu mnafanya kazi gani?nyinyi ndio mawakala wetu kwa mawaziri na rais, mbona mko kimya?

Nyie wabunge vipi,mlishindwa kuzuia serikali kuu kupokonya vyanzo vya mapato ya ndani na bado mmekaa kimya tu.Hii sio dalili ya nchi kufilisika?

Tunatakiwa kuishi kama mashetani tu
 
Ndo kuisoma namba huko.hakuna pesa za burebure tena mjomba ndo maana nikakwambia fanyakazi zako binafsi hachana na halmashauri
we jamaa kweli pumba hivi unajua jinsi nchi inavyojiendesha !unajua maana ya serikali-sasa unapomwambia aachane na halmashauri ni sawa na kumuambia aachane na mambo ya serikali au hujui halmashauri ni serikali.dah inabidi upelekwe milembe ndungu na ifikie hatua kujiunga Jamii forum wawake limit ya kiwango cha elimu inawezekana tunaongea na watu wa darasa la 7 humu Jf
 
Wanatakiwa wawe wabunifu watafute vyanzo vipya vya mapato kulingana na mazingira waliopo ila chondechonde Serikali Kuu msije mkavichukua vyanzo hivi vipya watakavyovibuni hata kama vitakuwa vinaleta mapato makubwa kama ilivyokuwa kwa Kodi ya Majengo (Property Tax).
ubunifu upi mkuu! unaposikia Halmasahuri zinakufa maana yake mapato ya ndani ni kidogo kutokana na watu wengi kuwa kwenye umasikini wa kutupwa!
 
No Money,no cash,no fuba,no faranga,no pesa,no asali ya moyo...........................ah na ninyi elezeeeni apo nilipo ishia
 
Kama hamkusanyi kodi punguzeni wafanyakazi, eti rim hizo form mbona tunatoa photocopy wenyewe? Mumepewa ada za leseni kodi za majengo, bado naruzuku mpate? Hapana kabisa. Majaliwa halmashauri itakayoshindwa kujiendesha ifute.

Tunahitaji kujenga reli mpya tuokoe barabara zetu, tunahitaji kujenga viwanda vijana wapate ajira, mwingine anataka apelekewe ruzuku apate hela ya supu na kuhudumia nyumba ndogo. Eti ukata? Kuna mwezi hukulipwa mshahara?
we nae hivi unajua maana ya 80% ya watanzania kuishi chini ya Tshs 2200 kwa siku! watu wa namna hii utakusanya kodi gani???-jamani elimu sio lazima usome masomo yako tu unaweza kusoma na masomo mengine kama uchumi kwenye mda wa ziada haya mambo utaelewa
 
Zitaje Halmashauri zilizokosa fedha tokea mwaka wa fedha umeanza. Mie nimetembelea halmashauri 15 na sasa nipo kilwa masoko naona miradi ya barabara ikiendelea vizuri. nimepita Newala, Masasi, Tunduru kuna miradi ya maji na barabara inaendelea pia. Nimepita makete bulongwa kuelekea mbeya kuna barabara ya lami ya km 15 inajengwa. Sijui ni halmashauri zipi unazozisemea
 
10 9 8 7 6 5 4 3 2 1
Soma taratibu hapo kama huelewi kumbuka elimu bureeeee
 
we jamaa kweli pumba hivi unajua jinsi nchi inavyojiendesha !unajua maana ya serikali-sasa unapomwambia aachane na halmashauri ni sawa na kumuambia aachane na mambo ya serikali au hujui halmashauri ni serikali.dah inabidi upelekwe milembe ndungu na ifikie hatua kujiunga Jamii forum wawake limit ya kiwango cha elimu inawezekana tunaongea na watu wa darasa la 7 humu Jf
We acha uboya nan kakwambia halmashauru zimekosa pesa???.
Kama vyanzo vyao hamna kitu acha wafe njaa.lakini kimbuka pesa nyingi zinatoka serikali kuu.mfumo wa zamani na sasa ni tofauti watu walikuwa wanajizolea mapesa kwa vitenda vya ajabu ajabu.mke .mme .mtoto ndo wanapewa tenda na kaz waliofanya hamna leo Mheshimiwa kaondoa huo ujinga .sasa mkome na hapo bado.atawakomesha zaidi.mi nasema pesa hipo tena nyingi tu chamsingi pesa halali.
 
Zitaje Halmashauri zilizokosa fedha tokea mwaka wa fedha umeanza. Mie nimetembelea halmashauri 15 na sasa nipo kilwa masoko naona miradi ya barabara ikiendelea vizuri. nimepita Newala, Masasi, Tunduru kuna miradi ya maji na barabara inaendelea pia. Nimepita makete bulongwa kuelekea mbeya kuna barabara ya lami ya km 15 inajengwa. Sijui ni halmashauri zipi unazozisemea
usiumize kichwa mkuu, hawa nyumbu wa lowasa ulipo tupo ndio wanaotusumbua humu, watu majinga sana, EL mwenyewe anakula bata africa ya kusini menyewe yana mayalla humu.
 
Sina uhakika na hili.
Ukiondoa Miwani ya Mbao unaweza kuyaona mambo katika uhalisia wake....kwa Ufupi tu jiulize ..sababu ya TULIA kupewa Viti maalum hadi pale alipo..check ..alipokuwa anaongoza vikao ..ukiwa umtu wakutakari mambo utaelewa ninachoongea kwamba kule ni Muhuri tu hakuna kitu
 
Kocha Sizonje kakwapua mapato ya halmashauri zote nchini sasa zinakufa kimya kimya. Kwa jinsi wanavyomuogopa kocha Sizonje hakuna wa kukemea ukwapuzi huu.

CC: lusungo
kodi ya majengo wanakusanya TRA,halmashauri zimeachiwa kodi ya pombe za kienyeji
 
Kinachoendelea katika halmashauri zetu ni kitu cha hatari kabisa.Ukata wa hali ya juu,ukata wa kukwamisha kwa kiwango kikubwa utoaji wa huduma kwa wananchi.

Wadau kwa wale wasio na taarifa ni kwamba halmashauri zipo kwenye hali ngumu sana ya kukosa ruzuku ya kujiendesha na ruzuku za miradi ya maendeleo.Ukata huu umefanya baadhi ya halmashauri zisizo na mapato ya ndani ya kutosha kushindwa kutoa huduma kwa wananchi.Imefikia wakati idara inakosa hata rim papers za kuandika taarifa.

Halmashauri hazikopesheki tena kwa wazabuni,wazabuni wanashinda halmashauri kudai pesa zao.Halmashauri zinaua mitaji ya wafanyabiashara

Watumishi wamekataa tamaa wamepauka hawajui kesho yao,stahiki zao hawajui hatma kutwa kuhakikiwa mara vyeti vya vyuo,mara umri mara ndoa na kadi za benki. Gharama za maisha zimepanda mishahara haijapanda. Wanaishi kwa hofu ya kutumbuliwa.

Madiwani wanakaa vikao hawana mradi wa kujadili fedha hazijaletwa,fedha zinaletwa kwa matukio tu,na sio kwa mujibu wa bajeti. Wakurugenzi wanaogopa wamejaa uwoga wa kutumbuliwa,hawana ujasiri wa kukumbushia ruzuku.
Wabunge wetu mnafanya kazi gani?nyinyi ndio mawakala wetu kwa mawaziri na rais, mbona mko kimya?

Nyie wabunge vipi,mlishindwa kuzuia serikali kuu kupokonya vyanzo vya mapato ya ndani na bado mmekaa kimya tu.Hii sio dalili ya nchi kufilisika?
Mkuu umechambua vinzuri sana.....alijekaa halmashauri anaelewa sana haya mambo. Kiukweli inasikitisha sana.
 
Wakuu wilaya wamekuwa ndio wabunge,madiwani,polisi,njoo uone Arusha maajabu ya Dunia.
 
Back
Top Bottom