DOKEZO Halmashauri ya Mji wa Bariadi imetelekeza vifaa vilivyonunuliwa kwa fedha za Kodi za Wananchi, hawajali, hakuna anayeumia

DOKEZO Halmashauri ya Mji wa Bariadi imetelekeza vifaa vilivyonunuliwa kwa fedha za Kodi za Wananchi, hawajali, hakuna anayeumia

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

KwetuKwanza

Senior Member
Joined
Mar 13, 2023
Posts
121
Reaction score
218
179789.jpg

Kuna vitu vinafanywa na serikali ukiviangalia vinaumiza, vinatia watu hasira, na hata hakuna anayejali, au kuumia kama ambavyo Wananchi tunaumia.

Hapo juu kuna picha nne, ingawa nimeziunganisha ili zikae sehemu moja, ni picha ya gari la taka, nyingine la kukusanya uchafu na nyingine ni mashine ya kuchonga Barabara na kukusanya uchafu pia.

Hivyo, vifaa na magari vilinunuliwa na Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu, viligharimu pesa nyingi, nadhani hapo hata Bilioni moja zilifika kama sikosei.

Hizo pesa ni kodi za wananchi, ni miaka kama mitatu hivi tangu vinunuliwe, leo vimepakiwa vyote pale kwenye uzio wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi (Somanda) Karibu kabisa na Jengo la Mochwari, havifanyi kazi.

Magari yote hayo na mashine hiyo vimeharibika, havifanyi kazi ni Mwaka mmoja sasa vimewekwa hapo, hakuna Kiongozi, mtumishi au Mtendaji yeyote ambaye anahurumia kodi hizo za Wananchi, wamevitelekeza, kama hawakununua hivi, kama walipewa bure hivi, kama siyo Kodi za wananchi, hakuna mtu yeyote ambaye anajali.

Ukiangalia hivyo vifaa vyote, vilinunuliwa kwa ajili ya suala la usafi kwenye Mji wa Bariadi hasa, leo Mji ni mchafu kweli kweli, kila sehemu ukipitia uchafu umejaa.

Kwa muda wa zaidi ya miezi sita hivi, Mji wa Bariadi hakuna gari la kusomba uchafu kwenye makazi ya watu, uchafu umejaa mpaka basi, kila sehemu ukipita hali ni mbaya, uchafu umerundikwa Barabarani kwenye makazi ya watu mpaka kero na harufu Kali.

Hilo gari la maji taka lilikuja Ili kusaidia Wananchi, lilikuja kupunguza gharama ambapo awali gari lilitoka Mkoani Mwanza, tangu limeharibika changamoto zimerudi pale pale, vyoo vinajaa gari la kuchukua uchafu kulipata ni shida.

Shida zimerudi palepale, Kodi za Wananchi, Kodi zetu zinateketea. Viongozi wa Juu, tunawaomba mukamulike Halmashauri ya Mji wa Bariadi, mulikeni hizi Kodi zinazoteketea, mziokoe.

Waziri Mkuu Mwiguli Mchemba, tunakuomba wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi uje umulike hii Hali ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Kodi zetu zinateketea.

Tunakuomba uje uangalie wananchi wako tunavyoteseka na Wakati Kodi zetu zinateketea.
 
kawaida .We sifia tu nchi imeizidi USA kwa maendeleo
 
View attachment 3528541

Kuna vitu vinafanywa na serikali ukiviangalia vinaumiza, vinatia watu hasira.

Na Hata hakuna anayejali, au kuumia kama ambavyo wananchi tunaumia.

Hapo juu Kuna Picha nne, ingawa nimeziunganisha ili zikae sehemu moja.

Hizo Picha moja ni Picha ya Gari la taka, nyingine Gari la kukusanya uchafu na nyingine ni mashine ya kuchonga Barabara na kukusanya uchafu pia.

Hivyo vifaa na magari vilinunuliwa na Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu, viligharimu pesa nyingi, nadhani hapo hata Bilioni moja zilifika kama sikosei.

Hizo pesa ni Kodi za wananchi, ni miaka kama mitatu hv tangu vinunuliwe, Leo vimepakiwa vyote pale kwenye uzio wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi (Somanda) Karibu kabisa na Jengo la Mochwari, havifanyi kazi.

Magari yote hayo na mashine hiyo vimeharibika, havifanyi kazi ni Mwaka mmoja sasa vimewekwa hapo, hakuna Kiongozi, mtumishi au Mtendaji yeyote ambaye anahurumia Kodi hizi za wananchi, wamevitelekeza, kama hawakununua hivi, kama walipewa bure hivi, kama siyo Kodi za wananchi, hakuna mtu yeyote ambaye anajali.

Ukiangalia hivyo vifaa vyote, vilinunuliwa Kwa ajili ya suala la usafi kwenye Mji wa Bariadi hasa, Leo Mji ni mchafu kweli kweli, kila sehemu ukipitia uchafu umejaa.

Kwa muda wa zaidi ya miezi sita hv, Mji wa Bariadi hakuna gari la kusomba uchafu kwenye makazi ya watu, uchafu umejaa mpaka basi, kila sehemu ukipita Hali ni mbaya, uchafu umerundikwa Barabarani kwenye makazi ya watu mpaka kero na harufu Kali.

Hilo gari la maji taka lilikuja Ili kusaidia wananchi, lilikuja kupunguza gharama ambapo awali gari lilitoka Mkoani Mwanza, tangu limeharibika changamoto zimerudi pale pale, vyoo vinajaa gari la kuchukua uchafu kulipata ni shida.

Shida zimerudi pale pale, Kodi za wananchi, Kodi zetu zinateketea.

Viongozi wa Juu, tunawaomba mukamulike Halmashauri ya Mji wa Bariadi, mulikeni hizi Kodi zinazoteketea, mziokoe.

Waziri Mkuu Mwiguli Mchemba, tunakuomba wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi uje umulike hii Hali ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Kodi zetu zinateketea.

Tunakuomba uje uangalie wananchi wako tunavyot
eseka na Wakati Kodi zetu zinateketea.
Wewe hukujua lengo la kununua hayo, lilikua wao kupata gaji yao cha juu sio kufanyakazi, walisha fankisha masirahi wewe rndelea kupiga kalele wewe unadhani ni mgeni hapa tz.
 
Mkuu ukianza kufatilia mambo ya nchi hii yatakupasua kichwa bure tu!,unawaza huko wenzio huku wanaiba mabilioni na kwenda kuyaficha nnje, ni bora uhangaikie ugali wa familia yako tu nyumbani.
 
Si ndio huko yule jamaa alizawadiwa arusha baada ya kujaza mkutano
 
Mleta mada ni mbea na mchonganishi...kama una hoja na sio mnafiki ulipaswa kuwasilisha changamoto hiyo kwenye vikao vyenu vya menejimenti na mabaraza ya Halmashauri ili utatuzi uwepo.
Wapi umesikia kazi ya Waziri mkuu ni kufuatilia vifaa vya taka vya bariadi.
Hapo unataka fedha ya matengenezo itoke ili na wewe ukatafune ...dunderhead!
Hapo unataka Mkurugenzi afukuzwe ukae baa kutamba kwamba mmemuondoa.
Punguza majungu sehemu za kazi
 
Simiyu yote ni takataka, nilipata rikizo ya Tanzania nkaenda Simiyu Itilima

Hospital ya wilaya ya Itilima 80% ya waajiriwa ni vijana yaani raia hapati huduma Hadi atoe Hela,,na DMO wao nae kibaka.

Itilima is the bogus and useless district
 
Mleta mada ni mbea na mchonganishi...kama una hoja na sio mnafiki ulipaswa kuwasilisha changamoto hiyo kwenye vikao vyenu vya menejimenti na mabaraza ya Halmashauri ili utatuzi uwepo.
Wapi umesikia kazi ya Waziri mkuu ni kufuatilia vifaa vya taka vya bariadi.
Hapo unataka fedha ya matengenezo itoke ili na wewe ukatafune ...dunderhead!
Hapo unataka Mkurugenzi afukuzwe ukae baa kutamba kwamba mmemuondoa.
Punguza majungu sehemu za kazi
KAMA UNATAARIFA SAHIHI YA KUTELEKEZWA KWA VITU HVO NI BORA UKAVITOLEA UFAFANUZI HAPA ILI MTOA MADA AKOSE NGUVU.
 
View attachment 3528537

Kuna vitu vinafanywa na serikali ukiviangalia vinaumiza, vinatia watu hasira.

Na Hata hakuna anayejali, au kuumia kama ambavyo wananchi tunaumia.

Hapo juu Kuna Picha nne, ingawa nimeziunganisha ili zikae sehemu moja.

Hizo Picha moja ni Picha ya Gari la taka, nyingine Gari la kukusanya uchafu na nyingine ni mashine ya kuchonga Barabara na kukusanya uchafu pia.

Hivyo vifaa na magari vilinunuliwa na Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu, viligharimu pesa nyingi, nadhani hapo hata Bilioni moja zilifika kama sikosei.

Hizo pesa ni Kodi za wananchi, ni miaka kama mitatu hv tangu vinunuliwe, Leo vimepakiwa vyote pale kwenye uzio wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi (Somanda) Karibu kabisa na Jengo la Mochwari, havifanyi kazi.

Magari yote hayo na mashine hiyo vimeharibika, havifanyi kazi ni Mwaka mmoja sasa vimewekwa hapo, hakuna Kiongozi, mtumishi au Mtendaji yeyote ambaye anahurumia Kodi hizi za wananchi, wamevitelekeza, kama hawakununua hivi, kama walipewa bure hivi, kama siyo Kodi za wananchi, hakuna mtu yeyote ambaye anajali.

Ukiangalia hivyo vifaa vyote, vilinunuliwa Kwa ajili ya suala la usafi kwenye Mji wa Bariadi hasa, Leo Mji ni mchafu kweli kweli, kila sehemu ukipitia uchafu umejaa.

Kwa muda wa zaidi ya miezi sita hv, Mji wa Bariadi hakuna gari la kusomba uchafu kwenye makazi ya watu, uchafu umejaa mpaka basi, kila sehemu ukipita Hali ni mbaya, uchafu umerundikwa Barabarani kwenye makazi ya watu mpaka kero na harufu Kali.

Hilo gari la maji taka lilikuja Ili kusaidia wananchi, lilikuja kupunguza gharama ambapo awali gari lilitoka Mkoani Mwanza, tangu limeharibika changamoto zimerudi pale pale, vyoo vinajaa gari la kuchukua uchafu kulipata ni shida.

Shida zimerudi pale pale, Kodi za wananchi, Kodi zetu zinateketea.

Viongozi wa Juu, tunawaomba mukamulike Halmashauri ya Mji wa Bariadi, mulikeni hizi Kodi zinazoteketea, mziokoe.

Waziri Mkuu Mwiguli Mchemba, tunakuomba wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi uje umulike hii Hali ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Kodi zetu zinateketea.

Tunakuomba uje uangalie wananchi wako tunavyoteseka na Wakati Kodi zetu zinateketea.
Sisi tuna uraniam mnatuonea wivu acha kuzua taharuki.
 
Simiyu yote ni takataka, nilipata rikizo ya Tanzania nkaenda Simiyu Itilima

Hospital ya wilaya ya Itilima 80% ya waajiriwa ni vijana yaani raia hapati huduma Hadi atoe Hela,,na DMO wao nae kibaka.

Itilima is the bogus and useless district
Hili sio simiyu tu ni maeneo mengi nchini sekta ya umma imeoza imejaa na kutapakaa ubadhilifu na rushwa za wazi wazi,hii yote sababu kuu ni serikali ya chama cha mapinduzi.
 
Hapo wanasubiri waje wajiuzie wenyewe kwa bei za kuokota kwa kupitia mlango wa nyuma
 
Back
Top Bottom