Halmashauri ya Jiji la Arusha Chini ya CHADEMA Yafanya Kweli

Halmashauri ya Jiji la Arusha Chini ya CHADEMA Yafanya Kweli

Halmashauri ya Jiji la Arusha imeanza ujenzi wa barabara zake kwa kiwango cha Lami nzito utakaogharimu zaidi ya Sh milioni 900. Barabara zilizopo kwenye mpango huu ni zile za Kaloleni zitakazojengwa kwa Urefu wa Mita 650 na Kata ya Themi - Barabara ya Serengeti kwa urefu wa Mita 700. Kazi zimekwishaanza na zitakamilika baada ya miezi Saba.
Chanzo cha Fedha ni Mfuko wa Barabara

Tunawaomba radhi wananchi wetu wa mitaa hiyo kwa usumbufu watakaoupata na pia tuwatakekutumia barabara nyingine mpaka pale Ujenzi utakapokamilika.
Nothing new
 
Kweli mtoto yake nepi...yaani hata kupika chai mnataka mpigiwe vigelegele?
 
Kesho utasikia kuna waziri amefanya ziara kukagua maendeleo ya ujenzi huo
 
Vipi kuhusu kujiongezea posho, Napo wamefanya kweli?
Mtu anayefanyakazi kupata mshahara au posho ni wajibu wake na kama kuongezwa ni jinsi maono ya mwajiri wake alivyoona anastahili kuongezwa au hapana.
 
CHADEMA MANENO HAKUNA NI VITENDOOO
TUUUU ........
 
Halmashauri ya Jiji la Arusha imeanza ujenzi wa barabara zake kwa kiwango cha Lami nzito utakaogharimu zaidi ya Sh milioni 900. Barabara zilizopo kwenye mpango huu ni zile za Kaloleni zitakazojengwa kwa Urefu wa Mita 650 na Kata ya Themi - Barabara ya Serengeti kwa urefu wa Mita 700. Kazi zimekwishaanza na zitakamilika baada ya miezi Saba.
Chanzo cha Fedha ni Mfuko wa Barabara

Tunawaomba radhi wananchi wetu wa mitaa hiyo kwa usumbufu watakaoupata na pia tuwatakekutumia barabara nyingine mpaka pale Ujenzi utakapokamilika.
Naona inapita karibu na soko la shivazzzz[emoji126] [emoji126] [emoji126] [emoji126]
 
Pongezi sana kwa Halmashauri ya jiji la Arusha chini Meya makini Kalist Lazaro
 
Muda si mrefu Lumumba na habari ya maelezo watakuja na taarifa KUWA MKUU WA KAYA KASIMAMISHA UJENZI WA BARABARA JIJI ARUSHA.
Soma basi japo chanzo cha fedha za ujenzi huo. Halafu uulize, huo mfuko wa barabara ni kitu gani?
 
Katika Jiji zima la Arusha, kujenga kipande cha bara bara cha km1.5 unajisifia!
 
Fanyeni chap barabara zipigwe lami.jiji liwe kama las vegas
 
Back
Top Bottom