DogoWaNjombe
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 3,279
- 7,699
Katika taarifa yake ya Agosti 14, 2026, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Wakili Faraja Nakua amesema tangazo hilo limebatilishwa kwa kuwa halikutoa ufafanuzi wa kutosha kuhusu walengwa, maeneo yaliyokusudiwa, madhumuni ya ada, utaratibu wa utekelezaji na msingi wake kisheria.
“Tangazo hilo halikutoa ufafanuzi toshelevu kuhusu walengwa wa ada hizo, maeneo mahususi yaliyokusudiwa, madhumuni, utaratibu wa utekelezaji wake pamoja na msingi wake kisheria hivyo kusababisha mkanganyiko,” amesema Nakua.
Amesema halmashauri inatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria, ikiwamo Kifungu cha 93(1) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji), Sura ya 288, huku ikitaja Sheria Ndogo za Udhibiti wa Vyombo vya Usafiri Mjini, Tangazo la Serikali Na.82 la Februari 7, 2025.
“Hadi wakati huo, utekelezaji wa maelekezo ya tangazo tajwa hapo juu umesitishwa,” amesema.
Pia soma:
~ Maafisa usafirishaji wa mtandao, maarufu kama bodaboda za mtandao, wamefunga barabara katika eneo la Chuo cha Biashara (CBE) Posta - Dar
~ Walinzi wa Halmashauri wanakamata Pikipiki Kariakoo kwa kuita "wrong parking" bila utaratibu