Hivi hawa watawala wa CCM wanadhani watadumu milele?
Hebu wajikumbushe historia, hakujawahi kutokea utawala wowote hapa duniani ambao uliwahi kudumu wakati wote.
Kwa hiyo CCM kuamini kuwa watadumu milele madarakani kutokana na namna walivyoitengeneza katiba yao waliyoipitisha Dodoma, watakuwa wanajidanganya kupita kiasi.
Wajaribu kufikiria vyama kama KANU cha Kenya, UNIP cha Zambia, MCP cha Malawi, vyama hivyo ambavyo vilikuwa vyama tawala toka nchi hizo zipate uhuru, vyama hivyo 'vimefutika' kabisa kwemye nchi zao.
Kwa hiyo CCM wasijione exceptional, na kwa njia hii wanayotumia ya mtutu wa bunduki, ili waendelee kudumu madarakani, ndiyo inazidi kuwasogeza haraka sana kwenye kaburi lao la kisiasa, kwa kuwa waTZ hivi sasa wamezidi kuichukia serikali yao maradufu, kutokana na policcm, kutumia nguvu kubwa mno kupinga wananchi wanaojitokeza kwa amani, kuelezea hisia zao, ambayo ni haki yao ya kikatiba, lakini sasa watawala wetu, wameamua kwa makusudi kabisa, kuvunja katiba, kuzuia mikusanyiko yoyote ambayo wanahisi itakuwa na mawazo kinzani na yao!